Msimamo wa CCM kuhusu tuhuma za kuhusika na mauaji ya wana-CHADEMA

maskini NAPE.... atakua anatoa statement kila mwezi between now na 2015 maana CDM watakua wanawalalamikia CCM kila siku
 
Nape iweje utoe tamlo leo wakati mauaji yalitokea kipindi kirefu ama kwa vile sasa yamefikia hatua ya kutisha, Iweje uisememee serikali? je ni kwa vile unatishwa na wimbi la wanaokimbia CCM,You can not fool people around, kumbuka watu wako mtaani na wanapata vitisho, lakini jua fika you cant stop it raining, watanzania wanafanya mabadiliko lazima ulikubali hili na ukombozi wa pili wa taifa letu uko mbioni, Yes few will die huku wakiwa chachu ya ukombozi wa taifa letu, iweje hadi leo wahusika hawa wasikamatwe hata kama si wafuasi wa CCM? hapa kuna maswali mengi kuliko majibu
 
Nape iweje utoe tamlo leo wakati mauaji yalitokea kipindi kirefu ama kwa vile sasa yamefikia hatua ya kutisha?Iweje uisememee serikali? je ni kwa vile unatishwa na wimbi la wanaokimbia CCM?You can not fool people around, kumbuka watu wako mtaani na wanapata vitisho, lakini jua fika you cant stop it raining, watanzania wanafanya mabadiliko lazima ulikubali hili na ukombozi wa pili wa taifa letu uko mbioni, Yes few will die na watakua chachu ya ukombozi wa taifa letu, iweje hadi leo wahusika hawa wasikamatwe hata kama si wafuasi wa CCM? Umesahau waliopigwa rissasi njenje pale Arusha wakati wa Mandamano ya CDM? unadhani kwanini mwkt wa chadema asihoji serikali yake?hapa kuna maswali mengi kuliko majibu
 
Nape iweje utoe tamlo leo wakati mauaji yalitokea kipindi kirefu ama kwa vile sasa yamefikia hatua ya kutisha?Iweje uisememee serikali? je ni kwa vile unatishwa na wimbi la wanaokimbia CCM?You can not fool people around, kumbuka watu wako mtaani na wanapata vitisho, lakini jua fika you cant stop it raining, watanzania wanafanya mabadiliko lazima ulikubali hili na ukombozi wa pili wa taifa letu uko mbioni, Yes few will die na watakua chachu ya ukombozi wa taifa letu, iweje hadi leo wahusika hawa wasikamatwe hata kama si wafuasi wa CCM? Umesahau waliopigwa rissasi njenje pale Arusha wakati wa Mandamano ya CDM? unadhani kwanini mwkt wa chadema asihoji serikali yake?hapa kuna maswali mengi kuliko majibu
 
[h=3]MSIMAMO WA CCM KUHUSU TUHUMA ZA KUHUSIKA NA MAUAJI YA WANACHADEMA[/h]
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Hivi karibuni chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kilielezea kile ilichoeleza kuwa ni kutishwa na wimbi la mauaji yanayotishia amani ya nchi kikidai kuwa jumla ya wanachama wake 15 wameuawa katika wilaya ya Igunga peke yake.


Madai hayo ya CHADEMA, pamoja na wanachama wengine na mashabiki wao, yalitolewa na Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, ambaye alidai kuwa mauaji hayo yana mkono wa serikali ya CCM, ambayo kwa madai yao imeona wazi kuwa upepo wa kisiasa umekiendea vibaya na sasa kinataka kujiimarisha katika utawala kwa kuua watu wanaoipinga.


Akifungua kikao cha Baraza Kuu la chama hicho jijini Dar es Salaam Aprili 29 mwaku huu mwenyekiti huyo alifafanua kuwa mbali na kuuawa kwa watu wanne kwa pamoja na juzi kifo cha mwenyekiti wao wa tawi huko Arumeru mkoani Arusha, jumla ya wanachama wake 15 wameuawa katika wilaya ya Igunga peke yake tangu kumalizika kwa uchaguzi mdogo wa jimbo hilo mwaka jana.


Mbowe katika maelezo yake alijaribu katika maeneo kadhaa kuihusisha CCM na au serikali yake katika matukio kadhaa yaliyowakabili baadhi ya wanachama na viongozi wa Chadema katika maeneo mbalimbali nchini likiwemo lile la Mbunge Highness Kiwia ambaye Suala lake bado Lipo mikononi mwa vyombo Vya dola likishughulikiwa.


Katika sehemu kubwa ya maelezo ya Ndg. Mbowe amejitahidi kuonesha kuwa mauaji yote yaliyoikabili na yatakayokuwa yakiikabili Chadema kupitia wafuasi wake yanafanyika kisiasa, Jambo ambalo ni la uzushi, kwani Halina ushahidi wa kisheria hata kimazingira, wa Moja kwa Moja unaoondosha ujinai au makosa hayo, na kuwa ni makosa yanayolenga muktadha wa kisiasa.


Huku akitaka kuuaminisha umma kuwa huo ndio ukweli, Ndg. Mbowe amesisitiza kuwa hilo lime kuwa likitekelezwa na CCM kwa lengo la kuwatisha wananchi kujiunga na chama hicho hoja ambayo haina msingi wowote wa kiutafiti.


Hivyo CCM kwa kutambua kuwa Suala la mauaji linabeba Kosa la jinai, na kwa kuwa Ndg. Mbowe ameshutumu Moja kwa Moja CCM na serikali yake kuihusisha na mauaji hayo, ni vema sasa nasi tukatoa msimamo wetu dhidi ya tuhuma, hiyo.


Kwanza, si busara hata kidogo kuihusisha CCM katika matukio hayo, kwani uchunguzi unaofanywa na vyombo vya dola umeshindwa mpaka sasa kuhusisha matukio hayo na siasa, badala ya kuyahusisha na makosa ya jinai ambayo hufanywa na watu kwa malengo tofauti na yale ambayo Ndg. Mbowe anataka kuwaaminisha watu.


Pili, CCM haijawai, haiwezi, na haitakuja fanya jambo lolote lenye lengo la kuvuruga Amani na Usalama wenye utulivu ndani ya taifa letu, hivyo uzushi na usingiziaji uliofanywa na Mtu Kama Ndg. Mbowe, si vema kuuacha kimya, badala yake nimetumia wasaa Huu muhimu Kujibu, na kutoa ufafanuzi ili Kuupa umma wa watanzania habari sahihi.


Ni aibu kwa Chama kama Chadema kujitahidi kwa nguvu zote kujaribu kuficha ukweli wa mauaji yanayotoa roho za watanzania wenzetu kwa kuyapa sura ya kisiasa. Hizi ni juhudi za makusudi za kutaka kuficha ukweli wa kinachotokea.


Ni aibu kwa chama kama Chadema kujaribu kutumia mauaji mabaya kama haya kutafuta mtaji wa kisiasa. Huku ni kuonyesha jinsi gani wamefilisika kisiasa mpaka wanafikia mahali pa kuamini kuwa wanaweza kutumia chochote kama mtaji wa kisiasa, vikiwemo vifo vya watanzania wenzetu. Huku si kufilisika tu ila kwakweli ni unyama unaotakiwa kulaaniwa na kila muungwana.


Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary


shame on you Nape
 
Nape: Mlijipongeza wakati mnafanya gizani sasa mambo yanaanza kuwa peupe mnaanza kujitokeza kujibu, lazima waliopanga watajulikana tu. Jueni kwamba damu ya mtu huwa haipotei itawaandama wote popote mtakapokwenda, iwe nyumbani, ofisini hata kwenye vikao vyenu lazima hili litawasumbua tu, uwe hukuhusika moja kwa moja ila kile kitendo cha kupanga na au ku-facilitate ni sawa na kuhusika.

Sisi tuna M4C nyie mna M4K.

Ushauri mzuri sana umempa autafakari mara mbilimbili
 
Nape anajua kama serikali inaongozwa na chama chake. Na anajua kwamba ni wajibu wa serikali kuhakikisha usalama wa kila raia, wa uhai na mali zake? Sasa kama serikali ya CCM imeshindwa kuwalinda watu wake na hata kuwakamata wanaohatarisha uhai wa watu wake, kumbe muuaji anakuwa ni nani hapo? Kwanini Nape asikubali kwamba kwa kushindwa kwao kukamata wauaji, kunaashiria kwamba wao wenyewe ndiyo wauaji?
 
Inashangaza kuona kada wa chama anatoa tamko linaloihusu jeshi la police,hv kinamanumba kz imewashinda.Sasa napata picha ni kweli policesisiem wanawaham wauwaji,ila kwakuwa jeshi le2 halipo huru ndo vile watoto wa mama kina nape wanadantia mambo.
 
yatasemwa mengi lakini tusisahau swali la 'KIPIMA JOTO' katika television ya ITV hapo jana tarehe 8/9/2012 linasema:

"amani bila maendeleo, je ina maana"?
 
Nape pole sana,kazi uliyopewa ya kuiita dhambi -haki,giza-nuru,uasi kuwa jema,itakuhukumu hapa duniani na mwisho utapotea na kuchomwa katika jeham ya moto.Nakuonya:hiyo kazi ikatae itakugharimu.
 
Hii Press Release imetolewa na CCM au imetolewa na serikali ya CCM?

Nape anasema hivi: ...Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe, ambaye alidai kuwa mauaji hayo yana mkono wa serikali ya CCM..."

Sasa kama madai yaliekezwa kwa serikali ya CCM, Nape anajibu kama nani? Yeye ni nani serikalini?

Bado Nape anaendelea kusema "...si busara hata kidogo kuihusisha CCM katika matukio hayo, kwani uchunguzi unaofanywa na vyombo vya dola umeshindwa mpaka sasa kuhusisha matukio hayo na siasa..."

Nape anafahamu nini kuhusu haya mauji? ana report ya uchunguzi toka Jeshi la Polisi tayari? Kama anayo report kwa nini asiweke wazi ili wanafamilia waliofiwa wajue ukweli ni upi?

Hii Press Release ni mbaya sana.

Nashukuru kwa kuliona hilo. Nia aibu kupita kiasi jinsi mambo yalivyo sasa.

Nadhani CCM wanawaza hivi; "Serikali haina idara ya propaganda na upotoshaji, CCM inayo. So Serikali inatumia mdomo wa huyu propagandist lakini kwa lengo la 'kukinusuru' chama...maana mwisho wa siku ndio mzazi wa hii Serikali"
 
Nape, is the most hopeless.

Wamajamii, japo siwezi kumtaja jina kwa sababu zinazoeleweka, lakini hivi karibuni nilikuwa nikiongea na afisa mkubwa wa Jeshi la polisi ambaye amekuwa akishughulikia masuala ya mashambulio dhidi ya viongozi/wapenzi wa CHADEMA, kwa maneno yake alisema, 'CHADEMA wana haki ya kulilaumu jeshi la polisi lakini na sisi hatuna la kufanya maana mashambulio haya yanafanywa na wafuasi wa CCM kwa maelekezo'; nilimwuliza kama yanafanywa kwa maelekezo ya viongozi wa chini wa CCM, naye aliniambia kuwa ingekuwa rahisi kushughulikia kama yangekuwa yanafanywa kwa maelekezo ya viongozi wa ngazi za chini lakini haya ni maelekezo ya viongozi wakubwa wa CCM. Na mwisho alisema kuwa jeshi la polisi halifurahishwi, haliungi mkono, halipendi lakini kwa mfumo wa sasa ni vigumu sana kutenda haki bila ya wewe polisi kudhibitiwa. Kwa hiyo ni vema watu wakajua kuwa mashambulizi haya yote yanafanywa na CCM. Na ndiyo maana hata Nape, katika huo waraka wake ameshindwa kujitetea, hajatoa utetezi wowote zaidi ya kumshambulia kwa maneno Mh. Mbowe. Wapenda mabadiliko wote, mnapoendesha harakati zenu, jihadharini na CCM maana ipo tayari hata kutoa roho za watu kwaajili ya kutetea uwepo wake.

Nami leo kuna ofisa mmoja ameniambia kitu hicho hicho. Kuwa maelekezo yanatoka juu tena yanakuwa makali! Unalazimishwa kuyatekeleza. Yana mwisho.
 
Nape,Nape mbona unazidi kupotoka na siasa zako za unafiki?!!!geuka na utubu mapema kabla hiyo dhambi kukutafuna :hat:
 
napata shida sana ninapomsikiliza au kusoma taarifa za Nape, sijui ana elimu gani? Yaani hata penye ukweli yeye hulazimisha ziwe propaganda. Kama Ccm haihusiki na mauaji ya wanaharakati, mbona hadi leo serikali ya Ccm imeshindwa kutoa tamko la mauaji ya wafuasi wa Chadema yaliyotokea Arusha? Hii serikali imekuwa ya kutetea maovu. Ifike mahali Nape awe binadamu zaidi kuliko msema hovyo! Naomba kujua Nape anajibu hizi tuhuma kama nani serikalini? Mh Mbowe alielekeza hizi shutuma serikalini iweje huyo msema hovyo aisaidie serikali kujibu? Hapa ndo huwa napata kigugumizi kumuelewa Nape.
 
........Ni aibu kwa chama kama Chadema kujaribu kutumia mauaji mabaya kama haya kutafuta mtaji wa kisiasa. Huku ni kuonyesha jinsi gani wamefilisika kisiasa mpaka wanafikia mahali pa kuamini kuwa wanaweza kutumia chochote kama mtaji wa kisiasa, vikiwemo vifo vya watanzania wenzetu. Huku si kufilisika tu ila kwakweli ni unyama unaotakiwa kulaaniwa na kila muungwana.


Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary


Tumia kiswahili fasaha!
 
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary
News realease yote ya kiswahili, lakini Nape huoni raha hadi uweke cheo chako kwa Kiingereza, sivyo?
 
Kuna uwezekano mkubwa sana kuwa chadema wanauana wenyewe kwa wenyewe ili kutafuta mtaji wa kisiasa kwa njia chafu. Wachagga wanajulikana kwa kutoana kafara hata kwa wizi tu. Lakini kuna siku watabainika.

Chadema ni chama hatari sana kwa usalama wa Tanzania.

Naishauri Serikali ikifungie hiki chama kwani kimeshakuwa na mtaji wa ukabila, ukanda na udini.

wewe pia ni muuaji tu, na kila kitu kinacho jadiliwa kufichua uovu wa ccm unatetea. Tuambie na Kolimba, aliuawa na cdm? Kigoma Malima je? Na Eduard Moringe Sokoine? CCM huua kila mtu ambaye ni hatari kwao, lakini siku si nyingi, mtalipa damu zote zisizo na hatia mlizo mwaga. Damu zenu zitamwagwa kwa njia iyo, na wengine mtamfuata Babu Seya na wanawe kule mliko wapeleka. SOON, mr ribosome, very soon.
 
Back
Top Bottom