Msigwa: Kabla ya kuzungumzia mfumo wa uchaguzi, Bashiru na Magufuli wakifufue kwanza kile chama cha siasa kilichokuwa kinaitwa CCM

Hizi ni porojo kama porojo zingine tu,ilimradi siku zinakwenda,litaibuka lingine,hili litapita,namshauri katibu mkuu wa ccm kwamba siasa za majikwaani haziepukiki,awe makini na kauli zake,kuna kundi kubwa la wanasiasa linaishi kwa kuvizia matamko,yaani watafuta kiki,atachokonolewa sana,hii ni mwanzo tu,kila tafsiri ya kauli zake itapatikana kwa mtazamo wa kila mmoja achukuliavyo

Mkuu sio kuwa makini na kauli zake, sema asiseme ukweli. Huyo Bashiru ukimwangalia ni muisilamu safi, na hajawahi kujihusisha na siasa za ulaghai. Magufuli alimpa cheo kikubwa akidhani kila mtu huwa anashiriki uovu. Kwa bahati mbaya huyo Bashiru sio mwanasiasa wa kufumbia macho ouvu kutokana na ucha Mungu wake, hivyo hicho kinachoendelea kwenye box la kura ambalo yeye anaamini linatoa kiongozi halali anaona dhahiri linachezewa na chama ambacho yeye ni kiongozi. Hili linaitesa dhamiri yake.

Kila mara huwa nasema hapa ccm imechokwa na hiyo ni kawaida ya binadamu yoyote. Magufuli kuamua kutumia madaraka yake vibaya kuihujumu cdm ni kwakuwa anajua kabisa cdm ndio inayopendwa kutokana na wakati, hivyo anawatumia tiss, vyombo vya dola na tume ya uchaguzi kuipa uhai ccm kitu ambacho hawezi na hatokaa aweze. Ukitaka kujua binam huchoka angalia ccm inafanya mikutano yenyewe, inatangaza maendeleo, inawahujumu cdm na kuwadhalilisha lakini bado haipati mvuto. Na sasa watu kudhihirisha wameichoka ccm wanatumia njia ya amani ya kususia uchaguzi. Na hawa akina Bashiru ni watu wanaosoma nyakati na ndio maana anajikuta automatic anaongea ukweli. Hiyo ni nature, kwamba wakati ni ukuta.
 
Nimemsikia Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM. Kauli yake inajaribu kujenga dhana potofu kuwa CCM imekuwa ikishinda kihalali lakini kwa kura kidogo, kwasababu eti wananchi hawana imani na mfumo wa uchaguzi.

Ukweli ni kwamba CCM ya Bashiru na Magufuli haijawahi kushinda kihalali katika uchaguzi wowote ule.Si wa kura kidogo wala kwa kura nyingi, CCM ya Bashiru na Magufuli haijawahi kushinda popote kihalali.

Wakati CCM ya kina Kikwete na Kinana, ilihangaika kutafuta ushindi kwa kutumia rushwa na wizi wa kura;CCM ya Magufuli na Bashiru hata kwa kutumia rushwa na wizi wa kura, bado haina uwezo wa kupata ushindi! Ni CCM iliyofikia kilele cha juu kabisa cha kuchokwa na kukataliwa na umma!

Kitu pekee ambacho CCM ya Magufuli na Bashiru inafanya ni kuitumia Tume ya Uchaguzi na Jeshi la Polisi kuzuia mawakala wa Chadema wasiingie vituoni kwa wakati, kujijazia kura kwenye masanduku, kujiandikia matokeo ya kughushi kwenye fomu za matokeo na kuhakikisha kuna mitutu ya bunduki ya kutosha ya kuwawezesha Wakurugenzi wa Halmashauri (Wateule wa Magufuli) kutangaza ushindi feki.

Kwa maneno mengine, ushindani uliopo hivi sasa, si baina ya vyama vya upinzani na CCM kama ilivyozoeleka huko nyuma; bali ni baina vyama vya upinzani na vyombo vya dola hususan Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa na wengineo waliokubali kuchukua nafasi ya CCM iliyoshindwa siasa.

Kwa hiyo, kimsingi, CCM anayoizungumzia Bashiru hata haipo.Ni kweli mfumo wetu wa uchaguzi una mapungufu na dosari nyingi. Lakini kabla ya kuzungumzia mfumo, namshauri Bashiru na Magufuli watafute namna ya kufufua kile "chama cha siasa" kilichokuwa kinaitwa "CCM", ili tushindane kwa sera na mikakati, na sio kwa mitutu ya bunduki.

Mfumo wa uchaguzi upo kwaajili ya vyama vya siasa, na si kwaajili ya Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola vilivyojipa kazi ya kuisaidia CCM iliyokufa.

Na hata maboresho yoyote yanayohitaji kufanyika katika mfumo wetu wa uchaguzi yanapaswa kulenga vyama halali vya kisiasa vinavyoshindana na sio majeshi ya nchi.

Rev. Peter Msigwa the MP for iringa Urban.

My take:
Niliwahi andika hapa JF hivi:

BM aliitoa "sisiem" mtaani akaipeleka hospitali (wodini). Jk, kwa upande wake, aliitoa wodini na kuipeleka ICU, na JPM anaitoa wodini na kuipeleka mortuary (kaburini).

Msigwa anaongea mithili ya mtu mwenye kichaa cha mbwa.
 
Nimemsikia Bashiru Ally, Katibu Mkuu wa CCM. Kauli yake inajaribu kujenga dhana potofu kuwa CCM imekuwa ikishinda kihalali lakini kwa kura kidogo, kwasababu eti wananchi hawana imani na mfumo wa uchaguzi.

Ukweli ni kwamba CCM ya Bashiru na Magufuli haijawahi kushinda kihalali katika uchaguzi wowote ule.Si wa kura kidogo wala kwa kura nyingi, CCM ya Bashiru na Magufuli haijawahi kushinda popote kihalali.

Wakati CCM ya kina Kikwete na Kinana, ilihangaika kutafuta ushindi kwa kutumia rushwa na wizi wa kura;CCM ya Magufuli na Bashiru hata kwa kutumia rushwa na wizi wa kura, bado haina uwezo wa kupata ushindi! Ni CCM iliyofikia kilele cha juu kabisa cha kuchokwa na kukataliwa na umma!

Kitu pekee ambacho CCM ya Magufuli na Bashiru inafanya ni kuitumia Tume ya Uchaguzi na Jeshi la Polisi kuzuia mawakala wa Chadema wasiingie vituoni kwa wakati, kujijazia kura kwenye masanduku, kujiandikia matokeo ya kughushi kwenye fomu za matokeo na kuhakikisha kuna mitutu ya bunduki ya kutosha ya kuwawezesha Wakurugenzi wa Halmashauri (Wateule wa Magufuli) kutangaza ushindi feki.

Kwa maneno mengine, ushindani uliopo hivi sasa, si baina ya vyama vya upinzani na CCM kama ilivyozoeleka huko nyuma; bali ni baina vyama vya upinzani na vyombo vya dola hususan Jeshi la Polisi, Usalama wa Taifa na wengineo waliokubali kuchukua nafasi ya CCM iliyoshindwa siasa.

Kwa hiyo, kimsingi, CCM anayoizungumzia Bashiru hata haipo.Ni kweli mfumo wetu wa uchaguzi una mapungufu na dosari nyingi. Lakini kabla ya kuzungumzia mfumo, namshauri Bashiru na Magufuli watafute namna ya kufufua kile "chama cha siasa" kilichokuwa kinaitwa "CCM", ili tushindane kwa sera na mikakati, na sio kwa mitutu ya bunduki.

Mfumo wa uchaguzi upo kwaajili ya vyama vya siasa, na si kwaajili ya Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola vilivyojipa kazi ya kuisaidia CCM iliyokufa.

Na hata maboresho yoyote yanayohitaji kufanyika katika mfumo wetu wa uchaguzi yanapaswa kulenga vyama halali vya kisiasa vinavyoshindana na sio majeshi ya nchi.

Rev. Peter Msigwa the MP for iringa Urban.

My take:
Niliwahi andika hapa JF hivi:

BM aliitoa "sisiem" mtaani akaipeleka hospitali (wodini). Jk, kwa upande wake, aliitoa wodini na kuipeleka ICU, na JPM anaitoa wodini na kuipeleka mortuary (kaburini).
Upo sawa kabisa msigwa. Kuna watu huku mtaani mimi huwa nawaambia ccm haijawahi kushinda,lakini walivyo watupu kichwani hawaelewi,ila naamini ipo siku wataelewa,
 
Huwasipendiupumbavukamahuuunaouoneshahapatumiaakiliyakovizurisiyokutumiakichwakufugianywelepekee.

Kweli nimeamini ukweli unauma, jinsi Magufuli anavyotumia madaraka yake vibaya kuihujumu upinzani watu bado wameshikilia msimamo wao hawaikubalii ccm. Matokeo yake nyie watetezi kwa kizidiwa na nguvu ya ukweli mmebaki kuongea upuuzi humu jukwaani. Huko kwenye box la kura mbona hatuoni hao watu wanaokwenda kuunga mkono kasi ya Magufuli? Badala yake tunaona nguvu ya tiss, jeshi la polisi, tume ya uchaguzi na vikundi vya kihalifu kuhakikisha ccm inashinda. Sasa kama rais huyu anatumia madaraka yake vibaya kuihujumu cdm, je akiingia rais mwingine akapambana kihalali ccm itaendelea kuwepo?
 
Kauli hii naona imewapa nguvu vijana wa chadema. Ni kama mtu mwenye kansa kupewa dawa ya kutuliza maumivu wakati akisubiri ahadi ya Mungu kutimia.
 
Back
Top Bottom