Nadhani kuna shida ya kuelewa maana ya ilani na mpango mkakati. Uandikaji wa ilani unaangalia mambo mengi sana ikiwemo marejeo ya mikataba ya kimataifa, ya kimkoa(East Africa customs union), sera za nchi kama sera ya afya,sera ya madini n.k.Ilani pia inaanglia vipaumbele vya wananchi. Ilani inaweza kuondoa hata vision za nchi, mikataba ya kimataifa na hata baadhi ya sheria kama siyo vya manufaa kwa wananchi. Ilani ni bidhaa ya chama kwa kipindi husika na bidhaa hii inapelekwa sokoni kupitia kampeni. Wanachi wakiridhika na hii bidhaa wanainunua kwa kupitia sanduku la kura.