dubu
JF-Expert Member
- Oct 18, 2011
- 3,496
- 3,461
Salaam wakuu,
Nasikitika kuwapa taarifa kwamba ndege yetu pendwa iliyopokelewa hivi karibuni, imegongwa.
Haiwezi kufanya kazi hadi matengenezo yafanyike.
Kwa ninavyojua, hii inaondoka na watu kuanzia juu, sababu imegongwa na ground handling company ambayo haijawa certified na IATA au ISO.
Ndege yetu tunahojivunia imegongwa na Kampuni ya NAS. Mbaya zaidi baada ya kogongwa imefichwa. Sio rahisi kuiona kwamba uipige picha, ila tumejitahidi kupata picha.
Inadaiwa kuwa NAS wamekubali kulipia gharama za matengenezo yake.
NAS ground handling company, Makao makuu yake yapo Mwanza ndo wakaletwa Dar. Kumbuka Swissport hairuhusiwi kuhandle Ndege za ATC.
SERIKALI ya Tanzania ilipokea Boeing 787-8 Dreamliner hii siku Jumapili Julai 8 mwaka 2018 ambapo Viongozi wakuu wa serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) wakiongozwa Rais John Magufuli, walikuwepo kiwanjani wakati ndege hiyo yenye uwezo wa kuchukua abiria 262 ilipowasili.
Bei ya ndege hii inakadiriwa kuwa $224.6 milioni (Sh512 bilioni za Tanzania) kwa mujibu wa taarifa kwenye tovuti ya kampuni ya Boeing.
Ndege hii ilianza safari za nje kwa kubeba shehena ya nyama ya Mbuzi kutoka Mwanza kuelekea Dubai.
Hivi karibuni SERIKALI ilisema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada. Ilisema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).
Ndege hizo zilinunuliwa na serikali zikiwa na uwezo wa kubeba abiria 76.
MY TAKE:
Biashara ya ndege ni Gharama sana.. Matengenezo yake ni ghali ukilinganisha na hela inayoingia. Ndo maana watu wanashangaa Mtu mwenye akili timamu kunua ndege huku Hospital haizina Madawa.
"Mtu ananunua ndege badala ya vifaa vya Zahanati, hii ni akili au matope.?" by Mhe. Halima James Mdee.
UPDATES;
Waliogonga ndege wameshikiliwa na vyombo vya dola kwa kile kilichodaiwa kwamba ni wahaini.
Habari zaidi, soma=>Ukweli kuhusu "kugongwa" kwa Dreamliner ya ATCL,ushindani wa kibiashara na siasa za kutakiana mabaya - JamiiForums
Nasikitika kuwapa taarifa kwamba ndege yetu pendwa iliyopokelewa hivi karibuni, imegongwa.
Haiwezi kufanya kazi hadi matengenezo yafanyike.
Kwa ninavyojua, hii inaondoka na watu kuanzia juu, sababu imegongwa na ground handling company ambayo haijawa certified na IATA au ISO.
Ndege yetu tunahojivunia imegongwa na Kampuni ya NAS. Mbaya zaidi baada ya kogongwa imefichwa. Sio rahisi kuiona kwamba uipige picha, ila tumejitahidi kupata picha.
Inadaiwa kuwa NAS wamekubali kulipia gharama za matengenezo yake.
NAS ground handling company, Makao makuu yake yapo Mwanza ndo wakaletwa Dar. Kumbuka Swissport hairuhusiwi kuhandle Ndege za ATC.
SERIKALI ya Tanzania ilipokea Boeing 787-8 Dreamliner hii siku Jumapili Julai 8 mwaka 2018 ambapo Viongozi wakuu wa serikali na Chama cha Mapinduzi (CCM) wakiongozwa Rais John Magufuli, walikuwepo kiwanjani wakati ndege hiyo yenye uwezo wa kuchukua abiria 262 ilipowasili.
Bei ya ndege hii inakadiriwa kuwa $224.6 milioni (Sh512 bilioni za Tanzania) kwa mujibu wa taarifa kwenye tovuti ya kampuni ya Boeing.
Ndege hii ilianza safari za nje kwa kubeba shehena ya nyama ya Mbuzi kutoka Mwanza kuelekea Dubai.
Hivi karibuni SERIKALI ilisema ndege mbili aina ya Bombardier Dash Q400 zilizonunuliwa mwaka 2016, zitapelekwa kufanyiwa ukarabati Canada. Ilisema ukarabati huo unatarajiwa kugharimu Dola za Marekani milioni sita (Sh. bilioni 13.860).
Ndege hizo zilinunuliwa na serikali zikiwa na uwezo wa kubeba abiria 76.
MY TAKE:
Biashara ya ndege ni Gharama sana.. Matengenezo yake ni ghali ukilinganisha na hela inayoingia. Ndo maana watu wanashangaa Mtu mwenye akili timamu kunua ndege huku Hospital haizina Madawa.
"Mtu ananunua ndege badala ya vifaa vya Zahanati, hii ni akili au matope.?" by Mhe. Halima James Mdee.
UPDATES;
Waliogonga ndege wameshikiliwa na vyombo vya dola kwa kile kilichodaiwa kwamba ni wahaini.
Habari zaidi, soma=>Ukweli kuhusu "kugongwa" kwa Dreamliner ya ATCL,ushindani wa kibiashara na siasa za kutakiana mabaya - JamiiForums