chitambikwa
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 3,941
- 903
Wabaya wa Rage watanywea , lakini binafsi nimefurahi sana
Acheni kuandika kama sio ma-great thinkers basi. Neno "KUFURU" inaweza ikawa ni "RELATIVE TERM')".
Career ya Mrisho Ngassa ni mcheza mpira,na nchi atokayo ni Tanzania, hili halina ubishi. Hivi tukiorodhesha wachezaji wote wa Tanzania na Mishahara hao, huyu hayupo top-10??
Mnamlinganisha Ngassa asie na hata Diploma moja labda na Engineer aliesota miaka kibao akikesha kwenye mbu ndio mnasema sio kufuru??
Kwa alichowekeza Ngassa mpaka kuja kupata hizo 6Mil ni hela nzuri tu tofauti na wengine wailliowekeza kwenye elimu, tena kwa kusotea kutoboa usiku, boom linachelewa mwezi mzima, unatumia akili nyingi kufikiri leo unakuja kujitapa eti unamzidi Ngassa mshahara!!!!
Tuna kina Felix Sunzu na Emanuel Okwi ambao ndio professional wetu hapa, wanalamba hizohizo, tena kwenye timu kama Simba ambayo naamini ni ndogo kuliko El Mereikh, why tusione kwamba kiwango hicho ni kikubwa kwa Mtanzania kupokea??
Fikirieni kwa umakini tena