Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 16,099
- 24,335
JE,INAWEZEKANA KUJENGA UTAJIRI WA VIZAZI KWA MSHAHARA WA SERIKALI?.
Ndiyo! Inawezekana kabisa. Hapa, tunaamini kujenga utajiri hakutegemei pekee ukubwa wa mshahara unaoingiza mwisho wa mwezi,bali nidhamu yako ya kifedha, mipango ya muda mrefu na mkakati thabiti wa kuwekeza.
Hebu tuangalie mchanganuo huu kwa mtumishi anayeingiza TZS 1,000,000 (Take-home) kwa mwezi
KANUNI ZA KIFEDHA ZA KUJENGA MTAJI.
Ili kutoboa lazima uwe na nidhamu
🎯 Jilipe Kwanza (Pay Yourself First)
Tenga hela ya uwekezaji kabla ya matumizi mengine yoyote!
🎯Kanuni ya 50/30/20 Gawanya mshahara wako hivi:
• 50% (TZS 500,000) ➡️ Mahitaji ya msingi.
• 30% (TZS 300,000) ➡️ Matumizi binafsi.
•20%(TZS 200,000)▶️ Uwekezaji Hili ndilo fungu la utajiri wa vizazi!.
📌 WAPI PA KUWEKEZA HIYO LAKI 2?
Ili kushinda mfumuko wa bei ambao NBS inaonyesha ni wastani wa 3% - 4%,wekeza kwenye
🎯Hati Fungani za Serikali (BOT)
Zinatoa faida ya 12% mpaka 15% kwa mwaka.
Usalama ni wa uhakika!
🎯Soko la Hisa (DSE)
Fanya Quality Investing kwenye makampuni yenye misingi imara yanayotoa gawio Mfano Sekta za Benk na Mawasiliano.
Utapata faida ya ongezeko la thamani na gawio.
🎯NGUVU YA RIBA JUMUISHI,COMPOUND INTEREST.
Kama utawekeza ile TZS 200,000 kila mwezi kwa miaka 20 kwenye uwekezaji unaokupa 12% kwa mwaka
💰Pesa uliyotoa mfukoni mwako kwa miaka 20 = TZS 48,000,000 tu!
🔥 Faida iliyozalishwa na soko = TZS 149,850,000
🎯 JUMLA KUU = TZS 197,850,000
Karibu Milioni 198!
Huu ni mtaji mkubwa unaotosha kuanzisha miradi mikubwa katika sekta zisizo za kibenk,non-banking investments na kuwarithisha wanao mali zisizohamishika! Unaweza pia kuharakisha safari hii kwa kuwa na vyanzo vya ziada vya mapato vinavyosimamiwa kwa tija kama vile kilimo au ufugaji makini nk.
Tushare Tujifunze pamoja.
Copied.
Ndiyo! Inawezekana kabisa. Hapa, tunaamini kujenga utajiri hakutegemei pekee ukubwa wa mshahara unaoingiza mwisho wa mwezi,bali nidhamu yako ya kifedha, mipango ya muda mrefu na mkakati thabiti wa kuwekeza.
Hebu tuangalie mchanganuo huu kwa mtumishi anayeingiza TZS 1,000,000 (Take-home) kwa mwezi
KANUNI ZA KIFEDHA ZA KUJENGA MTAJI.
Ili kutoboa lazima uwe na nidhamu
🎯 Jilipe Kwanza (Pay Yourself First)
Tenga hela ya uwekezaji kabla ya matumizi mengine yoyote!
🎯Kanuni ya 50/30/20 Gawanya mshahara wako hivi:
• 50% (TZS 500,000) ➡️ Mahitaji ya msingi.
• 30% (TZS 300,000) ➡️ Matumizi binafsi.
•20%(TZS 200,000)▶️ Uwekezaji Hili ndilo fungu la utajiri wa vizazi!.
📌 WAPI PA KUWEKEZA HIYO LAKI 2?
Ili kushinda mfumuko wa bei ambao NBS inaonyesha ni wastani wa 3% - 4%,wekeza kwenye
🎯Hati Fungani za Serikali (BOT)
Zinatoa faida ya 12% mpaka 15% kwa mwaka.
Usalama ni wa uhakika!
🎯Soko la Hisa (DSE)
Fanya Quality Investing kwenye makampuni yenye misingi imara yanayotoa gawio Mfano Sekta za Benk na Mawasiliano.
Utapata faida ya ongezeko la thamani na gawio.
🎯NGUVU YA RIBA JUMUISHI,COMPOUND INTEREST.
Kama utawekeza ile TZS 200,000 kila mwezi kwa miaka 20 kwenye uwekezaji unaokupa 12% kwa mwaka
💰Pesa uliyotoa mfukoni mwako kwa miaka 20 = TZS 48,000,000 tu!
🔥 Faida iliyozalishwa na soko = TZS 149,850,000
🎯 JUMLA KUU = TZS 197,850,000
Karibu Milioni 198!
Huu ni mtaji mkubwa unaotosha kuanzisha miradi mikubwa katika sekta zisizo za kibenk,non-banking investments na kuwarithisha wanao mali zisizohamishika! Unaweza pia kuharakisha safari hii kwa kuwa na vyanzo vya ziada vya mapato vinavyosimamiwa kwa tija kama vile kilimo au ufugaji makini nk.
Tushare Tujifunze pamoja.
Copied.