Msemaji wa Rais, hakuna kitu kinaitwa "kwanza" katika uandishi wa matukio mfululizo

sopinta

Member
May 28, 2020
46
93
Mara nyingi ukisoma taarifa za Ndugu Msigwa ambaye ni msemaji wa Rais Ikulu akielezea juu ya maamuzi yaliyotolewa na Ikulu kwa wakati mmoja, Msigwa na timu yake wakiandika TAARIFA KWA UMMA, utaona anaanza na neno "Kwanza , Rais amemteua......"

Nimshauri tu kuwa neno kwanza lipo katika kundi la comanding (lazimisha) yani lugha ya kulazimisha jambo. Pili, neno hili limebeba ubinafsi na dharau lakini pia linaleta ukakasi; wakati wa kulisoma halileti ushirikiano mzuri kimantiki na kisaikolojia.

Nikushauri tumia neno Mosi au Moja. Unaweza kuandika, mfano: Moja, Rais ametengua nafasi ya..... au ukaandika neno, Mosi, Rais amemteua Bwana .... lakini sio neno "KWANZA".

BARUA.jpg
 
Huyu siyo mwandishi wa Rais ni kada wa CCM, kwenye chama hilo neno Mwenyekiti wetu analipenda sana. Sasahivi taaluma pembeni ukada kwanza.
 
Back
Top Bottom