informer 06
Senior Member
- May 11, 2024
- 122
- 111
Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, David Misime amesema kwamba tayari Jeshi hilo limechua hatua kuhusu magari yaliyokuwa na namba za usajili SSH2530 ambapo amesema kwamba kwa sasa magari hayo hayataonekana.
Amesema kwamba baadhi ya magari yenye namba hizo yamekamatwa huku akitoa wito kwa Wananchi watakaoziona gari zenye namba hizo kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ili hatua ziweze kuchukua.
Amefafanua kuwa kama 'plate number' hazipo kwenye mfumo rasmi uliohalilishwa na Serikali hizo zinakuwa sio sahihi.
Hayo ameyasema leo Agost 29, 2025, katika mdahalo wa Kitaifa kuhusu usalama wa waandishi wa Habari kuelekea uchaguzi Mkuu 2025 ambao umewakutanisha waandishi wa habari na wadau wa vyombo vya habari.
Ikumbukwe kumekuwepo na mjadala katika mitandao ya kijamii hususani JamiiForums kuhusu uhalali wa gari zinazotomia namba hizo.
Pia soma