BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,140
Posted Date::6/17/2008
Huu ulikuwa ni mradi mwingine wa fisadi Mkapa alioufanya akiwa amebakisha miezu mitatu kumaliza awamu yake. Wakala alikuwa ni yule yule mhindi aliyelipwa 'commission' ya $12 million katika ununuzi wa rada iliyogharimu $42 million
Msemaji wa Ikulu aikingia kifua ndege ya Raisi
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
WAKATI wasomi na baadhi ya wabunge wakitaka ndege ya kifahari ya Rais iuzwe, Ikulu imeikingia kifua ikisema ndege hiyo haiwezi kuuzwa kwani bado inatumiwa na mkuu huyo wa nchi.
Kauli hiyo ya Ikulu imekuja wakati wasomi na baadhi ya wabunge, wametaka ndege hiyo iliyonunuliwa kwa sh 42 bilioni ipigwe mnada, kwani imekuwa ni hasara kwa serikali kwa kuchangia matumizi mabaya ya fedha za umma.
Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Salva Rweyemamu, alisema ndege hiyo bado ni muhimu kwa matumizi ya safari za Rais.
Rweyemamu alifafanua kwamba, siyo kwamba ndege hiyo haitumiki kabisa bali inatumika wakati ikibidi kutumika.
''Ndege ya Rais inatumika inabidi si kwamba haitumiki kabisa kama inavyoelezwa. kwa mfano juzi juzi aliitumia katika safari ambayo ilimfikisha hadi Kampala,'' alisema Rweyemamu.
Rweyemamu alisisitiza kwamba, Rais ana hadhi yake hivyo ni lazima anaposafiri awe na ndege kama hiyo.
Mkurugenzi huyo wa Ikulu alifafanua kwamba, ndege hiyo ilinunuliwa kwa makusudi ya matumizi ya Rais ikiwa ni salama.
Alipoulizwa vipi ndege hiyo imekuwa haitumiki sana lakini inafanyiwa matengenezo ya mara kwa mara tena nchini Marekani, ambako hutumia fedha nyingi, alisema matengenezo pia yanafanyika ikibidi si kila siku.
Alisema ndege hiyo haifanyiwi matengenezo bila sababu za msingi kama inavyoelezwa, bali hufanyiwa ikibidi.
''Rais ana hadhi yake, msafara wake na yeye mwenyewe lazima uwe salama, kwa hiyo matengenezo pia tukumbuke ni kwa ajili ya usalama wa Rais na msafara wake," alisema na kuongeza:
''Ndege inayo mbeba Rais lazima iwe salama, yeye na msafara wake wanahitaji usalama wakati wa kisafiri.''
Wiki iliyopita wasomi na wachumi waliohudhuria mkutano ulioandaliwa na Kampuni ya Ernst&Young, walitaka serikali kupunguza matumizi yasiyo na msingi, ikiwa ni pamoja na kuuza ndege hiyo.
Baadhi ya wasomi ambao ni wahadhiri kutoka Chuo cha Kilimo Sokoine (Sua) na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), walisema licha ya ndege hiyo kutotumiwa na Rais bado imekuwa ikifanyiwa matengenezo mara kwa mara nchini Marekani.
Katika hatua nyingine, Ikulu imesema ingependa kuona duru ya pili ya uchaguzi mkuu wa wa Zimbabwe hapo Juni 27, unakuwa huru na haki.
Rweyemamu alisema ni wakati wa kuomba Zimbabwe isiingie katika machafuko, akasisitiza kwamba Tanzania ingependa kuona haki na matakwa ya raia katika kuchagua yanazingatiwa bila kukiukwa.
Duru ya pili ya uchaguzi nchini Zimbabwe inatarajiwa kufanyika Juni 27, hata hivyo tayari kumekuwa na hali ya hatari baada ya Rais Robert Mugabe kutangaza kuingia msituni iwapo upinzani utashinda, huku Katibu Mkuu wa Chama cha Movement For Democratic Change (MDC) Tendai Biti, akikamatwa kwa tuhuma za uhaini.
Huu ulikuwa ni mradi mwingine wa fisadi Mkapa alioufanya akiwa amebakisha miezu mitatu kumaliza awamu yake. Wakala alikuwa ni yule yule mhindi aliyelipwa 'commission' ya $12 million katika ununuzi wa rada iliyogharimu $42 million
Msemaji wa Ikulu aikingia kifua ndege ya Raisi
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi
WAKATI wasomi na baadhi ya wabunge wakitaka ndege ya kifahari ya Rais iuzwe, Ikulu imeikingia kifua ikisema ndege hiyo haiwezi kuuzwa kwani bado inatumiwa na mkuu huyo wa nchi.
Kauli hiyo ya Ikulu imekuja wakati wasomi na baadhi ya wabunge, wametaka ndege hiyo iliyonunuliwa kwa sh 42 bilioni ipigwe mnada, kwani imekuwa ni hasara kwa serikali kwa kuchangia matumizi mabaya ya fedha za umma.
Akizungumza ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Salva Rweyemamu, alisema ndege hiyo bado ni muhimu kwa matumizi ya safari za Rais.
Rweyemamu alifafanua kwamba, siyo kwamba ndege hiyo haitumiki kabisa bali inatumika wakati ikibidi kutumika.
''Ndege ya Rais inatumika inabidi si kwamba haitumiki kabisa kama inavyoelezwa. kwa mfano juzi juzi aliitumia katika safari ambayo ilimfikisha hadi Kampala,'' alisema Rweyemamu.
Rweyemamu alisisitiza kwamba, Rais ana hadhi yake hivyo ni lazima anaposafiri awe na ndege kama hiyo.
Mkurugenzi huyo wa Ikulu alifafanua kwamba, ndege hiyo ilinunuliwa kwa makusudi ya matumizi ya Rais ikiwa ni salama.
Alipoulizwa vipi ndege hiyo imekuwa haitumiki sana lakini inafanyiwa matengenezo ya mara kwa mara tena nchini Marekani, ambako hutumia fedha nyingi, alisema matengenezo pia yanafanyika ikibidi si kila siku.
Alisema ndege hiyo haifanyiwi matengenezo bila sababu za msingi kama inavyoelezwa, bali hufanyiwa ikibidi.
''Rais ana hadhi yake, msafara wake na yeye mwenyewe lazima uwe salama, kwa hiyo matengenezo pia tukumbuke ni kwa ajili ya usalama wa Rais na msafara wake," alisema na kuongeza:
''Ndege inayo mbeba Rais lazima iwe salama, yeye na msafara wake wanahitaji usalama wakati wa kisafiri.''
Wiki iliyopita wasomi na wachumi waliohudhuria mkutano ulioandaliwa na Kampuni ya Ernst&Young, walitaka serikali kupunguza matumizi yasiyo na msingi, ikiwa ni pamoja na kuuza ndege hiyo.
Baadhi ya wasomi ambao ni wahadhiri kutoka Chuo cha Kilimo Sokoine (Sua) na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), walisema licha ya ndege hiyo kutotumiwa na Rais bado imekuwa ikifanyiwa matengenezo mara kwa mara nchini Marekani.
Katika hatua nyingine, Ikulu imesema ingependa kuona duru ya pili ya uchaguzi mkuu wa wa Zimbabwe hapo Juni 27, unakuwa huru na haki.
Rweyemamu alisema ni wakati wa kuomba Zimbabwe isiingie katika machafuko, akasisitiza kwamba Tanzania ingependa kuona haki na matakwa ya raia katika kuchagua yanazingatiwa bila kukiukwa.
Duru ya pili ya uchaguzi nchini Zimbabwe inatarajiwa kufanyika Juni 27, hata hivyo tayari kumekuwa na hali ya hatari baada ya Rais Robert Mugabe kutangaza kuingia msituni iwapo upinzani utashinda, huku Katibu Mkuu wa Chama cha Movement For Democratic Change (MDC) Tendai Biti, akikamatwa kwa tuhuma za uhaini.