Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
WanaJF,
Kwa wale walifuatilia mdahalo wa Jmosi uliomhusisha Mzee Pius Msekwa watakumbuka hoja mojawapo ya mzee huyo ilikuwa ni kutenganisha kati ya katiba na utendaji. Mzee Msekwa anataka kutuaminisha kuwa kazi ya katiba ni kuwezesha vyombo kuundwa, basi. Kinachofuata baada ya hapo, siyo kazi ya katiba. Eti ni mambo ya utekelezaji ambayo ufanisi wake unategemea uadirifu wa wanaongoza vyombo hivyo. Kwa hiyo, kwa mtazamo wangu, angekuwa mzee huyu ana uwezo angekataa katakata kubadili katiba iliyo kwa imani kwamba vipengele vyake vingi bado ni relevant. Alitolea mfano wa tume ya maadili kwamba nayo imeundwa kwa mujibu wa katiba lakini maadili yapo palepale.
Mimi binafsi naona huo ni mojawapo ya udhaifu wa katiba yetu ya sasa. Katiba lazima iende mbele zaidi. Isiishie kujenga mazingira ya chombo kuundwa (serikali, bunge na mahakama, n.k). Lazima iingie kwenye utendaji na ku-address masuala yanayotokana na utendaji. Na zaidi ya yote ianishe mfumo mzuri usiotiliwa shaka wa kupata viongozi wa ngazi zote kuanzia chini hadi juu. Ninachotaka kusema hapa ni kuwa, chini ya katiba mpya, wananchi wasiofaa kuwa viongozi wasiote hata ndoto ya kugombe uongozi.
Kwa wale walifuatilia mdahalo wa Jmosi uliomhusisha Mzee Pius Msekwa watakumbuka hoja mojawapo ya mzee huyo ilikuwa ni kutenganisha kati ya katiba na utendaji. Mzee Msekwa anataka kutuaminisha kuwa kazi ya katiba ni kuwezesha vyombo kuundwa, basi. Kinachofuata baada ya hapo, siyo kazi ya katiba. Eti ni mambo ya utekelezaji ambayo ufanisi wake unategemea uadirifu wa wanaongoza vyombo hivyo. Kwa hiyo, kwa mtazamo wangu, angekuwa mzee huyu ana uwezo angekataa katakata kubadili katiba iliyo kwa imani kwamba vipengele vyake vingi bado ni relevant. Alitolea mfano wa tume ya maadili kwamba nayo imeundwa kwa mujibu wa katiba lakini maadili yapo palepale.
Mimi binafsi naona huo ni mojawapo ya udhaifu wa katiba yetu ya sasa. Katiba lazima iende mbele zaidi. Isiishie kujenga mazingira ya chombo kuundwa (serikali, bunge na mahakama, n.k). Lazima iingie kwenye utendaji na ku-address masuala yanayotokana na utendaji. Na zaidi ya yote ianishe mfumo mzuri usiotiliwa shaka wa kupata viongozi wa ngazi zote kuanzia chini hadi juu. Ninachotaka kusema hapa ni kuwa, chini ya katiba mpya, wananchi wasiofaa kuwa viongozi wasiote hata ndoto ya kugombe uongozi.