Msekwa: CCM imepoteza sifa asili

MKWEPA KODI

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2015
Posts
28,700
Reaction score
71,114
Ameyasema hayo kwenye kitabu chake cha kuadhimisha miaka 39 tangu kuzaliwa kwa ccm. Amesema ccm imepoteza asili yake ya kutetea wanyonge

Chanzo: Magazeti ya leo

 
Wakati terehe 5 mwezi wa pili ni siku ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuadhimisha miaka 39 tangu kuzaliwa kwake, kada mkongwe na muasisi wa Chama hicho, Pius Msekwa amechambua uwezo na udhaifu wake, akibainisha kuwa Chama hicho (CCM) KIMEPOTEZA SIFA YA ASILI YA KUWA CHAMA CHA WANYONGE.

Yaliyoathiri taswira ya Chama (CCM)
a. Migogoro baina ya viongozi, makundi yanayohasimiana.

b. Tuhuma za ufisadi kwamba CCM inakumbatia mafisadi

c. Wafanyabiashara kujipenyeza kwa kasi katika vikao vya Chama

d. Chama kupoteza sifa ya asili ya kuwajali WANYONGE.

chanzo: MWANANCHI
 

Attachments

  • IMG_20160204_071139.jpg
    341 KB · Views: 61
  • IMG_20160204_071030.jpg
    222.1 KB · Views: 64
Mzee msekwa namuheshimu sana huyu mzee

WAFANYABIASHARA KUJIPENYEZA KWA SPEED YA 4G KATIKA VIKAO VYA CHAMA
AHAAA connet dots.... ndo maana hata wakikwepa kodi tunawaomba walipe badala ya kuwashurutisha na kuwapeleka kwenye vyombo vya kutafsiriwa sheria km mahakama
CCM ni ile ile ooh ni ile ile
 
WATAMWAMBIA MZEE MSALITI NA ANAKARIBIA KUFA
 
Angetia neno kwenye haya yanayoendelea Zanzibar. Waishinikize chama Chao kitafute njia za kibusara zaidi kuliko kushinikiza uchaguzi. Vinginevyo kaongelea sifa za kawaida kabisa ambazo kila mtu anazijua kuhusu CCM.
 
Aisee juzi tu Pius amewasaliti wanyonge wa Unguja na Pemba.
 
Angetia neno kwenye haya yanayoendelea Zanzibar. Waishinikize chama Chao kitafute njia za kibusara zaidi kuliko kushinikiza uchaguzi. Vinginevyo kaongelea sifa za kawaida kabisa ambazo kila mtu anazijua kuhusu CCM.
kuhusu hali ya zenj wanagwaya kulisemea ila ikipatikana suluhu utaona watakapo jitokeza na kulitolea ufafanuzi sio kwa wanasiasa wakongwe pekee yao ni mpaka kwa wasomi na viongozi wa dini.
 
Mzee msekwa kaisha yupo kama kubenea tu mda wote kuwanza shanga na kuhangaika na mambo yasiyo ya msingi.
hahahahahaaa..kiukweli mzee kasema ukweli kama wanaccm wenyewe ndio nyie mzee ana haki ya kusema ukweli. ccm kimekuwa chama na pango la wanafiki na wazadiki.
 
Ameyasema hayo kwenye kitabu chake cha kuadhimisha miaka 39 tangu kuzaliwa kwa ccm. Amesema ccm imepoteza asili yake ya kutetea wanyonge

Chanzo: Magazeti ya leo

Waliosambaratisha azimio la Arusha ambalo ndilo lilikuwa msingi mkuu wa kutetea wanyonge na yeye Msekwa alikuwemo .Baada ya kusambaratisha akawa kwenye bodi ya kampuni ya kibepari ya vodacom kama mkurugenzi AKAINGIA KWA SPIDI YA 4G kwenye kampuni hiyo ya kibepari .Hawa wazee sio siri ndio wauaji wakubwa wa CCM Ile iliyokuwa ya wanyonge.

Azimio LA zanzibar MSEKWA alikuwemo na alihusika na liliua hasa asili ya CCM kuwa ya wanyonge.Hicho kitabu kaandika wengine kasahau kujiweka na yeye kama mhusika
 
Oooh ni ile ile!
Viongozi ni wale wale!
ooh ni wale wale!
 
Kingine alichosahau si tu wafanyabiashara kujipenyeza kwenye vikao vya CCM kuliharibu chama lakini pia viongozi waliokuwa wa juu kama yeye kujipenyeza kwenye vikao vya bodi vya wafanyabiashara kama Vodacom AMBAKO YEYE ALIKUWA board member.Kujipenyeza huko kwa viongozi wa juu kama yeye kuliwapa GO ahead WAFANYABIASHARA NAO KUJIPENYEZA VIKAO VYA CCM kwa sababu ya hiyo kukaibuka UNHOLY ALLIANCE kati ya viongozi wa juu wa CCM na Wafanyabiashara wakubwa kwa pamoja wakaitengeneza CCM isiyojali wanyonge.

Msekwa kachangia hiyo hali
 
Oooh ni ile ile!
Viongozi ni wale wale!
ooh ni wale wale!
Tumeuziwa mbuzi kwenye gunia

Hata malaika Mbinguni WANAJUA kuwa ccm haina na haijawahi kuwa na nia ya kumkomboa mtanzania
We mwenyewe fikiria jitu fisadi linapewa uenyekiti wa bunge
 
Tumeuziwa mbuzi kwenye gunia

Hata malaika Mbinguni WANAJUA kuwa ccm haina na haijawahi kuwa na nia ya kumkomboa mtanzania
We mwenyewe fikiria jitu fisadi linapewa uenyekiti wa bunge

lile fisadi lingine la CHADEMA lililohukumiwa na bunge kuwa fisadi la kutupwa CHADEMA mkalipa ugombea Uraisi unalisemeaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…