Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Mwigizaji wa filamu nchini, Sajuki alidondoka jukwaani juzi wakati akijaribu kuwasalimia mashabiki wake waliofurika kumtazama kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abedi, Arusha. Sajuki ambaye jina lake halisi ni JUMA Saidi Kilowoko alikua akisumbumbuliwa na matatizo ya kupungukiwa na damu na kulazimika kwenda kutibiwa nchini India.
Mwigizaji huyo alipanda jukwaani katika tamasha lililowahusisha wasanii wa filamu na muziki lakini ndoto yake ya kuwasalimia mashabiki wake haikuwezekana. Mara baada ya kukabidhiwa kipaza sauti Sajuki alitamka neno moja ''ahhh'' na kudondoka chini na wasanii wenzake walimsaidia kuinuka na kumuondoa jukwaani hapo.