Msanii Chiligati na kauli zake zinavyogeuka kama Kinyonga

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,014
Kutoka Gazeti la MwanaHALISI la August 26, 2009

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati aliwaambia waandishi wa habari baada ya kikao cha NEC, "Tumesema inatosha. Hapa tulipofika tusiendelee mbele. Wanaoropoka ovyo ni walevi na tumeona kuna kundi dogo ambalo linajiona kama ni wateule wa kuzungumzia ufisadi."

Kauli hii ya CCM ililenga wabunge jasiri ambao wamekuwa wakiikosoa serikali, miswada yake na kutaka watuhumiwa wa ufisadi kuchukuliwa hatua.
Kutoka Gazeti la Mwananchi la Sept 15, 2009
Jana, Chiligati alikuwa ni mtu mwenye kuunga mkono kikundi hicho wakati Mwananchi ilipotaka maoni yake kuhusu wabunge hao ambao wanaonekana kukaidi maazimio ya Nec, huku wakitamba kuwa hakuna anayeweza kuwafunga mdomo.

"CCM haina ugomvi na wabunge wake wala mtu yeyote anayejitoa mhanga kupinga ama kupambana na mafisadi," alisema Chiligati ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

"Msimamo wa chama chetu ni kwamba rushwa ni adui wa haki, usichukue, kuomba wala kutoa rushwa, huo ndio wimbo wa kila mwana-CCM.

"Hatuna ugomvi wala uadui na mtu yeyote anayepambana na rushwa, ufisadi, uporaji, wizi na ujambazi. Huo ndio msimamo wa CCM."
Tutaona na kusikia mengi sana yaliyojaa usanii wa hali ya juu katika safari hii ya kuelekea October, 2010 kutoka kwa viongozi mbali mbali ndani ya Chama Cha Mafisadi ili kuomba KULA (isomeke Kura) kutoka kwa Watanzania.
 
Last edited:
Chiligati ndio aina ya viongozi tulionao. Hawana msimamo ni wababaishaji mradi amfuraishe mkubwa wake wa kazi.
 
Huyu nu bendera tu hufuata upepo. Kwani hata ukimuuliza kuwa kuna maelezo alitoa yanayokinzana atakuambia waandishi wananiweka maneno mdomoni. Lakini ndiyo viongozi tulionao wanang'ata na kupuliza.

Kwani baada ya kusikia reaction ya watu kwa waliyofanya DOM akaja na maelezo mapya ya kuwatuliza watu. HAWA NI WASANII PURE....
 
Huyu nu bendera tu hufuata upepo. Kwani hata ukimuuliza kuwa kuna maelezo alitoa yanayokinzana atakuambia waandishi wananiweka maneno mdomoni. Lakini ndiyo viongozi tulionao wanang'ata na kupuliza.

Kwani baada ya kusikia reaction ya watu kwa waliyofanya DOM akaja na maelezo mapya ya kuwatuliza watu. HAWA NI WASANII PURE....
hata wale wapiganaji wa ufisadi kutoka CCM ni wasanii tuu kama CHILIGATI.
 
Hawa wasanii wako wengi sana.......Chiligati ni Msanii amekosea fani alitakiwa awe TOT Plus

BIG UP wapiganaji wa Mafisadi
 
Hawa wasanii wako wengi sana.......Chiligati ni Msanii amekosea fani alitakiwa awe TOT Plus

BIG UP wapiganaji wa Mafisadi


Akumaanisha kusema “Msimamo wa chama chetu ni kwamba rushwa ni adui wa haki, usichukue, kuomba wala kutoa rushwa, huo ndio wimbo wa kila mwana-CCM.

“Hatuna ugomvi wala uadui na mtu yeyote anayepambana na rushwa, ufisadi, uporaji, wizi na ujambazi. Huo ndio msimamo wa CCM.”


bali alitaka kusema “Msimamo wa chama chetu ni kwamba rushwa si adui wa haki, Chukua,omba,pokea na toa rushwa, huo ndio wimbo wa kila mwana-CCM.

tena

“Tuna ugomvi na uadui mkubwa na mtu yeyote anayepambana na rushwa, ufisadi, uporaji, wizi na ujambazi. Huo ndio msimamo wa CCM.”
 
sisi kama wapigakura kila mmoja wetu asikie aibu na nafsi yake kumpigia kura mtu wa aina hii. Anaidhalilisha kura yako
 
- Huyu chiligati hata kumjadili hapa JF ni kumpa mno heshima asiyostahili, anatia kinyaa sana!, tuwaachie darhotwire huko wamjadili.

Ahsante.

William.
 
hii ndio nchi yenye viongozi wenye busara tele kama huyu mzee, sio kama hajui kuwa anatetea ufisadi kwa moyo wake wote, kwa nguvu zake zote na kwa akili yake yote ila tu anatufanya watanzania hatuna akili, mungu ibariki tz
 
Kwani ni kitu gani cha ajabu hapa; yaani mnataka kusema kuwa mkimwona kichaa anatembea uchi mtashangaa.
 
kwani JK Alipomteua hamkujua ni mjinga mwingine ameletwa katika madaraka ya CCM, BAADA MAKAMBA NA Tambwe hiza, bila kumsahau Nchimbi.
Hivi kweli hao watu wanaweza kumshauri nini rais wa Nchi?...mimi naona ni tatizo la Mh JK
 

Date::9/16/2009 Makamba amfuata Spika Sitta Urambo, ampigia magoti
*ASEMA HANA UGOMVI NAYE, ASEMA ALIKUWA MLEZI WA NDOA ZA WANAYE

Na John Dotto, Tabora

KATIKA kile kilichoelezwa kwamba, ni kujisafisha mbele ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, CCM imesema ipo pamoja naye katika kutekeleza majukumu yake kama Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba; ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kuondoa utata uliotokana na maazimio ya Halmashauri Kuu ya chama hicho ulioonyesha kuwa wabunge wanaopiga kelele dhidi ya ufisadi, wanakichafua chama na serikali yake.

Akizungumza na viongozi wa CCM wilaya ya Urambo kwenye mkutano wa ndani uliohudhuriwa na Spika Sitta, Makamba, alitumia muda mwingi kumsifia Sitta kwamba ni mtu muelewa, asiyetetereka na wala kuyumbishwa na mtu yeyote na kwamba anachokifanya ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho.

Makamba aliwaambia wanaCCM hao kwamba, hana chuki na Sitta, kwani hata alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alimkaribisha katika ndoa za wanawe na akapewa nafasi ya kuzungumza kama baba mlezi, heshima ambayo alisema hataisahau katika maisha yake.

Alisema wana CCM wanatakiwa kupuuza maneno ya watu wanaodai chama kina mgogoro na Spika, kwasababu hakuna kitu kama hicho na yote anayoyatekeleza kwenye Bunge ni kwa niaba ya chama chake.

Hata hivyo, baada ya kikao cha NEC, Makamba alikuwa mstari wa mbele kudai kuwa kikao kile kina uwezo wa kumuhoji mbunge yoyote hata Sitta kama anakwenda tofauti na chama.

Makamba alinukuliwa akisema NEC ni mama na akina Spika ni watoto hivyo ina mamlaka ya kuhoji mienendo yao.

Mara baada ya kikao cha NEC, Sitta alifanya ziara mkoani Tabora na kulalamika kwamba, CCM makao makuu wamewakataza viongozi wa chama hicho mkoani kumpokea.

Hatua ya Makamba kwenda Urambo kuhutubia na Sitta, inatafsiriwa kama njia ya kuweka mambo sawa na kufuta makovu ya huko nyuma baina yake na Spika.

Kwa upande wake, Sitta alimshukuru Makamba kwa kutembelea jimboni kwake na mkoa wa Tabora kwa ujumla.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika baada ya kikao cha ndani kumalizika, Makamba aliwahakikishia wananchi wa Urambo kwamba CCM kipo pamoja na mbunge wao Sitta, ndiyo maana wanatekeleza ahadi zote ikiwemo ujenzi wa barabara ya Urambo Kaliua mpaka Tabora Mjini.

Akizungumzia suala la ufisadi, Makamba alisema kuwa wanaCCM wote kuanzia ngazi ya matawi wanapaswa kuungana na wabunge wanaopiga vita ufisadi, kwani vita dhidi ya rushwa ni ya wanaCCM wote.

Alisema anakerwa na watu wanaosema CCM ni chama cha mafisadi kwani ufisadi wa mtu mmoja si wa CCM na akatoa mfano kuwa dhambi ya Mkatoliki mmoja si dhambi ya Askofu Kilaini wala kanisa lote.

Makamba alimaliza ziara yake jana mkoani Tabora na juzi alipokuwa akizungumza na viongozi wa CCM wakiwemo makatibu wote wa wilaya za Tabora kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM mkoa, aliwalaumu viongozi hao kukaa kimya wakati wapinzani wanakishambulia chama hicho kwa kukipakazia maneno machafu.

Aliwataka waamke na kukipigania chama na kuacha kukaa kimya na kusubiri makao makuu ama Makamba kujibu mashambulizi.

Baada ya kikao cha Nec kilichofanyika Dodoma mwezi uliopita, Makamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chilligati kwa nyakati tofauti walisema CCM imeunda kamati ya watu watatu, inayoongozwa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kuwachunguza wabunge wenye tabia ya kuishambulia serikali nje ya vikao vya chama.

Habari za ndani ya kikao hicho ambazo baadaye zilivuja kwa vyombo vya habari, zilieleza kuwa Nec ilimweka kitimoto Spika Sitta kwa madai kuwa anaruhusu mijadala inayokichafua chama na serikali, huku baadhi ya wajumbe wakishinikiza anyang'anywe kadi ya CCM kwa madai kuwa anawapa uhuru bungeni watu wanaoishambulia serikali kwa ufisadi.

Hata hivyo, mwanzoni mwa wiki hii baada ya hotuba ya Rais, Chilligati alisema chama hicho hakina ugomvi wala uadui na wabunge wake wanaoongoza vita dhidi ya mafisadi nchini.

Kabla ya hapo, Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita ambaye alisemekana kumwandama Spika Sitta katika kikao cha NEC na akamwita faru aliyejeruhiwa anayetakiwa kumalizwa kabla hajasababisha madhara zaidi, naye alibadili msimamo na kuwaunga mkono wapiganaji wa ufisadi pamoja na Spika Sitta kwamba, wanatekeleza ilani ya CCM, hivyo wanastahili kuungwa mkono.

Mabadiliko haya ya siasa ndani ya chama hiki tawala na mfululizo wa matukio ya aina hiyo likiwemo la Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile ambaye amekaririwa katika vyombo vya habari akisema hana ugomvi na Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe, anayesemekana kuwa ni hasimu wake kisiasa.
Kuna nini huko CCM wanaogoka au? these people have no brain, leo wanafanya hili kesho wanageuka kabisa halafu bado wanajiona wanafaa kuendelea kuwa viongozi. bure kabisa hawa
 
Hiki chama sasa hakina tofauti na kundi la wacheza kamari! Huu upupu tuutafsiri vipi? ni uhuni? ubabe? usanii? au ufedhuli? Hivi kweli kiongozi wa taasisi muhimu ya Taifa anaweza kuwa kigeugeu namna hii na aliyemuweka madarakani akaendelea kumtegemea? Hivi Makamba anaweza kumshauri nini Raisi wa Nchi? Chiligati anaweza kumshauri nini raisi kikailetea manufaa nchi hii? Aibu gani hii? Na ina maana Raisi anajisikia anaonekana ana akili nyingi kwa kuendelea kuwaweka madarakani na kuzungukwa na watu kama hawa? Hivi Raisi anaona analitumikia Taifa inavyopasa kwa kuwa na kundi hili? Au anataka kutuonyesha anavyozifanya kazi za Wizara na Taasisi zote yeye mwenyewe?
Wataalam wanaamini kuwa kiongozi ambaye hawazi kuchagua watu competent kujaza nafasi za kazi na ku-delegate powers kwao na wakaiweza kazi waliyopewa, inamaanisha hata yeye mwenyewe au haijui kazi yenyewe au umuhimu wa kumuajiri au la anaiga tu! Au anatoa hongo ya cheo. Madhara yake ndiyo haya tunayoyaona.

Ninajiuliza hivi hawa jamaa wana Job Description kweli? Do they have terms of reference?? I doubt it!
 
Bora angekufa chilli kuliko kumpoteza Med Mpakanjia

Med naye kafanyiziwa na ccm baada ya kupiga vita dhidi ya madawa ya kulevya??

Naomba msinikwoti vibaya na samahani nitakao wa kwaza ila nataka kufikisha ujumbe fulani ambao nashindwa niuweke vipi?
 
Kutoka Gazeti la MwanaHALISI la August 26, 2009

Kutoka Gazeti la Mwananchi la Sept 15, 2009

Tutaona na kusikia mengi sana yaliyojaa usanii wa hali ya juu katika safari hii ya kuelekea October, 2010 kutoka kwa viongozi mbali mbali ndani ya Chama Cha Mafisadi ili kuomba KULA (isomeke Kura) kutoka kwa Watanzania.

Niliisha andika mwanzo ya kua kauli za viongozi wa CCM ni bendera kufuata upepo kauli zao hazitoki kichwani zinatoka katika ulimi itazame hii ya Makamba imekaaje

Makamba amfuata Spika Sitta Urambo, ampigia magoti

*ASEMA HANA UGOMVI NAYE, ASEMA ALIKUWA MLEZI WA NDOA ZA WANAYE

Na John Dotto, Tabora

KATIKA kile kilichoelezwa kwamba, ni kujisafisha mbele ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta, CCM imesema ipo pamoja naye katika kutekeleza majukumu yake kama Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Kauli hiyo ilitolewa jana na Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba; ikiwa ni siku chache baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kuondoa utata uliotokana na maazimio ya Halmashauri Kuu ya chama hicho ulioonyesha kuwa wabunge wanaopiga kelele dhidi ya ufisadi, wanakichafua chama na serikali yake.

Akizungumza na viongozi wa CCM wilaya ya Urambo kwenye mkutano wa ndani uliohudhuriwa na Spika Sitta, Makamba, alitumia muda mwingi kumsifia Sitta kwamba ni mtu muelewa, asiyetetereka na wala kuyumbishwa na mtu yeyote na kwamba anachokifanya ni utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho.

Makamba aliwaambia wanaCCM hao kwamba, hana chuki na Sitta, kwani hata alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alimkaribisha katika ndoa za wanawe na akapewa nafasi ya kuzungumza kama baba mlezi, heshima ambayo alisema hataisahau katika maisha yake.

Alisema wana CCM wanatakiwa kupuuza maneno ya watu wanaodai chama kina mgogoro na Spika, kwasababu hakuna kitu kama hicho na yote anayoyatekeleza kwenye Bunge ni kwa niaba ya chama chake.

Hata hivyo, baada ya kikao cha NEC, Makamba alikuwa mstari wa mbele kudai kuwa kikao kile kina uwezo wa kumuhoji mbunge yoyote hata Sitta kama anakwenda tofauti na chama.

Makamba alinukuliwa akisema NEC ni mama na akina Spika ni watoto hivyo ina mamlaka ya kuhoji mienendo yao.

Mara baada ya kikao cha NEC, Sitta alifanya ziara mkoani Tabora na kulalamika kwamba, CCM makao makuu wamewakataza viongozi wa chama hicho mkoani kumpokea.

Hatua ya Makamba kwenda Urambo kuhutubia na Sitta, inatafsiriwa kama njia ya kuweka mambo sawa na kufuta makovu ya huko nyuma baina yake na Spika.

Kwa upande wake, Sitta alimshukuru Makamba kwa kutembelea jimboni kwake na mkoa wa Tabora kwa ujumla.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika baada ya kikao cha ndani kumalizika, Makamba aliwahakikishia wananchi wa Urambo kwamba CCM kipo pamoja na mbunge wao Sitta, ndiyo maana wanatekeleza ahadi zote ikiwemo ujenzi wa barabara ya Urambo Kaliua mpaka Tabora Mjini.

Akizungumzia suala la ufisadi, Makamba alisema kuwa wanaCCM wote kuanzia ngazi ya matawi wanapaswa kuungana na wabunge wanaopiga vita ufisadi, kwani vita dhidi ya rushwa ni ya wanaCCM wote.

Alisema anakerwa na watu wanaosema CCM ni chama cha mafisadi kwani ufisadi wa mtu mmoja si wa CCM na akatoa mfano kuwa dhambi ya Mkatoliki mmoja si dhambi ya Askofu Kilaini wala kanisa lote.

Makamba alimaliza ziara yake jana mkoani Tabora na juzi alipokuwa akizungumza na viongozi wa CCM wakiwemo makatibu wote wa wilaya za Tabora kwenye ukumbi wa mikutano wa CCM mkoa, aliwalaumu viongozi hao kukaa kimya wakati wapinzani wanakishambulia chama hicho kwa kukipakazia maneno machafu.

Aliwataka waamke na kukipigania chama na kuacha kukaa kimya na kusubiri makao makuu ama Makamba kujibu mashambulizi.

Baada ya kikao cha Nec kilichofanyika Dodoma mwezi uliopita, Makamba na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chilligati kwa nyakati tofauti walisema CCM imeunda kamati ya watu watatu, inayoongozwa na Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi kuwachunguza wabunge wenye tabia ya kuishambulia serikali nje ya vikao vya chama.

Habari za ndani ya kikao hicho ambazo baadaye zilivuja kwa vyombo vya habari, zilieleza kuwa Nec ilimweka kitimoto Spika Sitta kwa madai kuwa anaruhusu mijadala inayokichafua chama na serikali, huku baadhi ya wajumbe wakishinikiza anyang'anywe kadi ya CCM kwa madai kuwa anawapa uhuru bungeni watu wanaoishambulia serikali kwa ufisadi.

Hata hivyo, mwanzoni mwa wiki hii baada ya hotuba ya Rais, Chilligati alisema chama hicho hakina ugomvi wala uadui na wabunge wake wanaoongoza vita dhidi ya mafisadi nchini.

Kabla ya hapo, Mwenyekiti wa Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita ambaye alisemekana kumwandama Spika Sitta katika kikao cha NEC na akamwita faru aliyejeruhiwa anayetakiwa kumalizwa kabla hajasababisha madhara zaidi, naye alibadili msimamo na kuwaunga mkono wapiganaji wa ufisadi pamoja na Spika Sitta kwamba, wanatekeleza ilani ya CCM, hivyo wanastahili kuungwa mkono.

Mabadiliko haya ya siasa ndani ya chama hiki tawala na mfululizo wa matukio ya aina hiyo likiwemo la Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile ambaye amekaririwa katika vyombo vya habari akisema hana ugomvi na Mbunge wa Kyela, Dk Harrison Mwakyembe, anayesemekana kuwa ni hasimu wake kisiasa.
 
duh eti ndo viongozi wanoongoza nchi,ni malimbukeni wa kutupilia mbali,wanapima pressure,wakaona Six na kundi lake wamepata support kila kona ya nchi,JK nae akajikanyaga kusifia japo alifichaficha sasa wale mbwa koko ndo wanajikomba upande wa kina six,sasa hawa wana mchango gani kwa maendeleo ya nchi? je watakuwa madarakani hadi lini?haohao wanawaleta watoto wao na ndugu zao kuwarithi,je tutabadilika lini sisi watanzania?au ndo imetoka till mwisho wa dunia?
 
Wanajua wafanyacho, kuwadanganya watz. Wameshaona watz wengi wanapinga ufisadi hivyo lazima wabadili rangi kama kinyonga. Ngoja muwachgue muone musiki wake.

Angalau kikao cha nec ccm kilituonyesha sura halisi za baadhi ya tunaowaita viongozi, dawa ni kuwachinjia baharini ******o zao.
 
Back
Top Bottom