Siku za Juma
Juma au wiki moja huwa na siku saba. Yafuatayo ni majina ya siku za juma. Kwa kuwa asili yake ni Kiarabu na Kiislamu, Jumamosi ndiyo siku ya kwanza ya wiki; nayo Ijumaa ndiyo siku ya saba.
SIKU YA JUMA
KIINGEREZA
Jumatatu
Monday
Jumanne
Tuesday
Jumatano
Wednesday
Alhamisi
Thursday
Ijumaa
Friday
Jumamosi
Saturday
Jumapili
Sunday
Siku Zikilinganishwa na Leo
Haya ni majina tunayotumia kurejelea siku zinazokaribiana na leo.
SIKU
MAELEZO
MFANO
juzi
siku iliyotangulia jana
ikiwa leo ni Jumatano, juzi ilikuwa Jumatatu.
jana
siku iliyotangulia leo
ikiwa leo ni Jumatano, jana ilikuwa Jumanne.
leo
siku ambayo tuko sasa hivi
kesho
siku inayofuata
Ikiwa leo ni Jumatano, kesho itakuwa Alhamisi.
kesho kutwa
siku itakayokuja baada ya kesho
ikiwa leo ni Jumatano, kesho kutwa itakuwa Ijumaa.
mtondogoo
siku itakayokuja baada ya kesho kesho kutwa. siku tatu kutoka leo
ikiwa leo ni Jumatano, kesho kutwa itakuwa Jumamosi.
Miezi ya Mwaka
Jedwali lifuatalo linaonyesha majina ya miezi katika mwaka, na idadi ya siku katika kila mwezi.
#
JINA
MWEZI WA:
SIKU
1
Januari
kwanza
31
2
Februari
pili
28
3
Machi
tatu
31
4
Aprili
nne
30
5
Mei
tano
31
6
Juni
sita
30
7
Julai
saba
31
8
Agosti
nane
31
9
Septemba
tisa
30
10
Oktoba
kumi
31
11
Novemba
kumi na moja
30
12
Disemba
kumi na mbili
31
Masaa ya Siku
Yafuatayo ni mafungu ya masaa au nyakati mbalimbali za siku.
WAKATI
MAELEZO
MASAA
mchana
wakati wa siku wenye jua. kutoka saa kumi na mbili asubuhi hadi saa moja jioni hivi
6am - 7pm
usiku
wakati wa siku usiokuwa na jua. kutoka saa moja jioni hadi saa kumi na mbili siku inayofuatia
7pm - 6am
alfajiri
kati ya saa tisa na saa kumi na moja asubuhi
3am - 5am
macheo
saa kumi na moja hadi saa kumi na mbili hivi jua linapochomoza
3am - 5am
asubuhi
kutoka saa kumi na mbili hadi saa sita za mchana
6am - 12pm
adhuhuri
saa sita za mchana hadi saa nane
12pm - 2pm
alasiri
saa nane hadi saa kumi na moja hivi
2pm - 5pm
jioni
saa kumi na moja hadi saa moja jioni
5pm - 6pm
machweo/magharibi
saa kumi na mbili hadi saa moja jioni; jua linapotua
6pm - 7pm
usiku mchanga
kati ya saa moja jioni na saa sita za usiku
7pm - 12am
usiku wa manane
kutoka saa sita za usiku hadi alfajiri
12am - 3am
Kusoma Saa
Tunaweza kusoma saa tukitumia: Mfumo wa Kiswahili
katika mfumo wa Kiswahili/Kibantu, siku huanza saa kumi na mbili asubuhi. Kwa hivyo, saa moja ya asubuhi inakuwa ndiyo saa ya kwanza(1) ya siku.
Mfano:
5:00 asubuhi ⇒ saa tano kamili asubuhi
9:15 usiku ⇒ saa tisa na robo usiku.
11:30 jioni ⇒ saa kumi na moja unusu jioni
2:45 alasiri ⇒ saa tatu kasorobo au saa mbili na dakika arubaini na tano alasiri
10:23 alfajiri ⇒ saa kumi na dakika ishirini na tatu alfajiri
Mfumo wa Kimataifa/Kiingereza
Huu ndio mfumo unaokubalika kirasmi katika mataifa na lugha mbalimbali. Kulingana na mfumo huu, siku huanza saa sita za usiku. Hivyo basi, saa saba ya usiku inakuwa saa ya kwanza(1) ya siku.
Mfano:
6:00 macheo ⇒ saa kumi na mbili asubuhi kamili macheo
12:15 adhuhuri ⇒ saa sita na robo adhuhuri.
3:30 alasiri ⇒ saa tisa na nusu alasiri
6:45 jioni ⇒ saa moja kasorobo au saa kumi na mbili na dakika arubaini na tano jioni
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.