viporo vya asubuhi ni hatari Kwa afya yako ya ubongo
Kwa kweli hawa ccm wanatatizo la ugonjwa wa amnesia
1.mwaka 1995 walikuwa kila siku kwenye magazeti,radio na mikutano ya bunge na hadhara ni kumsema mrema anauroho wa madaraka,walipommaliza siku hizi Lukuvi anamsema waziri mkuu mstaafu na mafao yake atayapigania,ni mpinzani halisi na mrema bila kujielewa amekuwa ndondocha ya ccm
2.mwaka 2000, Seif na Lipumba waliitwa majangili ,chama chao cha kiislamu kinapiga kampeni mskitini hadi 2005 kikaitwa chama cha kigaidi ,mara waarabu wenye imani kali watatuumiza watanzania tusikiunge mkono chama hiki,seif hadi akaondoka kwenda nje
3.mwaka 2010 chadema kilipoanza tu kampeni,na nchi ikageukia kwenye chama alichokiona kina nguvu, ccm kama kawaida yenu mkamshambulia Dr slaa kuwa hana mke,aliyenae ni mke wa mtu,mzinzi,mara alifukuzwa upadri kwa kuiba hela za kanisa,maaskofu walipozijibu hoja zenu,mkahamia Arumeru chama cha wachagga,chama cha kikiristo ,waroma walipowakomalia,mkabadili ni chama cha ukanda ikashindikana maana kipo kila mkoa na wanachama na viongozi hutoka kila dhehebu mkabadili
Ni chama cha kigaidi ,kesi kibao za kuchonga ili kife mkafeli,sasa Mh.Membe akawakumbusha kuwa 2015 tunaenda kupambana na chadema kubwa na imara aaah
Mmeona mbinu zimefeli mkaamua kuunda chama kwa kuchukua wanachama CUF na Chadema ( maana hakuna ubishi rangi ya bendera ya chama cha ACT, na viongozi wake ni wote waliofukuzwa toka vyama hivi viwili ,mmeweka na alama ya nyota itumiwayo na wenzetu waislamu ili kumega waislam na wakristo)
Niwashauri hebu muwe mnarejea historia kwa nini kanisa la Rome liligawanyika pande mbili,mashariki Orthodox na magharibi Catholic church inatead of universal one?
Ccm tatueni matatizo ya wananchi si kuwafundisha wanachadema kuwa viongozi hawa wanafaa,wale hawafai!!
Eti tumewachoka
Ni lini jirani amekuwa msemaji wa familia ya mwenzake kuwa watoto mkataeni baba yenu tumemchoka?
Leteni jipya,mnajidharirisha tu ,au mleteni makamba anaetetea kutoa rushwa kwenye uchaguzi wa kura za maoni,mimi naona alikuwa bora kuliko msomali na timu yake ya waropokaji