Msajili Hazina: Watumishi wa Umma wako busy kuomba uhamisho kwenda TRA, EWURA, TANESCO na TPA kufuata maslah makubwa

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Msajili wa Hazina Nehemiah Mchechu amesema kuwa kuna wimbi la watumishi ambao wanakimbilia kuomba uhamisho kutoka katika taasisi zao kwenya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Umeme nchini (Tanesco), Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) na Mamlaka ya Udhibiti Nishati na Maji (EWURA).

Akizungumza katika Kikao Kazi cha Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa Taasisi za Umma, Mchechu amesema kumekuwa na ‘Mafuriko’ ya maombi kwenda taasisi hizo akisisitiza kuwa “watu wanataka kwenda huko kwa kuwa mapato ni mazuri.”

Amewataka Watendaji kusaidia kuboresha taasisi zao ili kuwezesha mashirika hayo kusimama.

Hata hivyo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Charles Kichere amesema baadhi ya Taasisi zimekuwa zikipelekewa watumishi ambao hawana uwezo akishauri kufanyike uchambuzi ili watu wanaohamishwa wawe na sifa zinazohitajika katika taasisi husika.

“Unakuta kuna taasisi inaletewa watu ambao hata haiwahitaji kwa sababu tu ni watumishi wa umma, nadhani hili nalo lifanyiwe kazi,” ameshauri CAG.
 
Halafu wakifika kwenye hizo taasisi hawawezi kazi.

Wamezoea kuingia na kutoka na sherehe sherehe huko walikotoka kuoiga mzigo hawawezi.

Yaani unaambiwa hadi aibu kwamba wamefikajefikaje?

Ni afadhali kila taasisi iajiri yenyewe kuliko kupelekewa watumishi mizigo.
 
Hata maswala ya teuzi za wakuu wa idara na vitengo hupelekea kupata watumishi wasio mahiri na ufanisi.

Mtu anakuwa meneja wa idara au kitengo fulani kwa kuteuliwa kwa kujuana,

Ukimuuliza tuambie uko hapo kufanya nini hajui, je maana ya kitengo chako ni nini?!

Hajui.
 
Dawa ni scale za serikali zitumike across regardless uko wapi. Hapa Hata walimu watanufaika. Kwa mfumo huu serikali imetengeza taasisi muhimu na taasisi mkafie mabli au Bora liende. Ukitoka hapo unataka matokeo chanya na uwajibikaji. Subutu.
 
Wanapokuja external auditors na hasa wale wanaoagizwa kutoa taarifa Kwa Wafadhili imekuwa ikielekezwa kuwa nafasi za CEOs Na HDOs na Sections zitangazwe

Hata zikitangazwa internally ndani ya taasisi husika iwapo iko na population kubwa inakubalika,

Ufanyike usaili huru Na wa uwazi.
 
Pana taasisi hazizalishi kabisa lakini maslai Bora kabisa.
Magufuli alitaka kuweka rate moja.
Wote ni watumishi wa umma kwann wengine chai ofisi wengine wakakope mama ntilie hii si sawa.
 
Back
Top Bottom