Msajili abariki Mbatia na Wenzake kusimamishwa NCCR Mageuzi

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,024
1,612
1653481670433.png

Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, leo Mei 25 imebariki Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia na Sekretarieti yake yote kusimamishwa na kuwataka kutojihusisha na siasa ndani ya chama hicho hadi uamuzi huo utakapoamuliwa vinginevyo.

Mnamo Mei 21, Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi ilimsimamisha Mbatia na makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi mkutano mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma zinazowakabili.

Pia soma:
- NCCR Mageuzi yamsimamisha James Mbatia kufanya shughuli za Chama
 

Mbatia azungumzia kauli ya Magufuli​

Wednesday January 22 2020​

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia amempongeza Rais wa Tanzania, John Magufuli baada ya kiongozi mkuu huyo wa nchi kusema uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 utakuwa wa amani, uhuru na haki.

Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia amempongeza Rais wa Tanzania, John Magufuli baada ya kiongozi mkuu huyo wa nchi kusema uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 utakuwa wa amani, uhuru na haki.

Dar es Salaam. Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia amempongeza Rais wa Tanzania, John Magufuli baada ya kiongozi mkuu huyo wa nchi kusema uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 utakuwa wa amani, uhuru na haki.

Mbatia ametoa kauli hiyo leo Jumatano Januari 22, 2020 baada ya kuulizwa na Mwananchi kuhusu kauli ya Magufuli aliyoitoa jana Jumanne katika hafla ya chakula cha jioni aliyowaandalia mabalozi na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam.

Magufuli amesema shughuli ya uchaguzi ni muhimu kwa nchi yoyote inayofuata misingi ya kidemokrasia kama Tanzania, hivyo Serikali imejipanga kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika katika mazingira ya amani.

Katika maelezo yake, Mbatia ambaye pia ni mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) amemtaka Rais Magufuli kutekeleza ndoto yake hiyo
 
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, leo Mei 25 imebariki Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia na Sekretarieti yake yote kusimamishwa na kuwataka kutojihusisha na siasa ndani ya chama hicho hadi uamuzi huo utakapoamuliwa vinginevyo...
Mbatia tulimuonya kwamba Kushirikiana na shetani kutamgharimu , siku zote SHETANI HANA RAFIKI , walimtumia wakati wa Uchaguzi sasa wanambwaga
 
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, leo Mei 25 imebariki Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia na Sekretarieti yake yote kusimamishwa na kuwataka kutojihusisha na siasa ndani ya chama hicho hadi uamuzi huo utakapoamuliwa vinginevyo.
-
Mnamo Mei 21, Halmashauri Kuu ya Chama cha NCCR-Mageuzi ilimsimamisha Mbatia na makamu Mwenyekiti Bara, Angelina Mtahiwa kutojihusisha na shughuli zozote za chama hadi mkutano mkuu utakapoitishwa ili wajieleze kuhusiana na tuhuma zinazowakabili.
Mbowe amekubali kunusuru chama chake lakini Mbatia amekaidi sasa hichi kinachotokea ndio malipo yake.

Tunahitaji upinzani wenye nguvu zaidi Tanzania na usiotetereka kwa vyovyote vile., bado tuna struggle,
Tutamkumbuka na kumuenzi Jemedari Maalim Seif Sharif Hamad
 
Mbowe amekubali kunusuru chama chake lakini Mbatia amekaidi sasa hichi kinachotokea ndio malipo yake.,
Tunahitaji upinzani wenye nguvu zaidi Tanzania na usiotetereka kwa vyovyote vile., bado tuna struggle,
Tutamkumbuka na kumuenzi Jemedari Maalim Seif Sharif Hamad
je wakiungana?
 
Ila Mbatia hana namna pale ,maana wanaposema akidi haijatosha si kweli,ile nyomi ilikuwa kubwab,inawezekana watu walishajiorganize chini kwa chini ikabaki kumdondosha tu.
Ofisi ya msajili ilihusika katika haya mapinduzi na huyo Nyahoza alikuwepo kwenye mapinduzi hayo na ndo alibariki hiyo akidi kuwa imetimia. Haya mambo ya ofisi ya msajili kuwa mpanga safu kwa vyama badala ya kuwa mlezi sijui yanatupeleka wapi kiukweli na sijui wanafanya hivyo kwa manufaa ya nani?
 
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, leo Mei 25 imebariki Mwenyekiti wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia na Sekretarieti yake yote kusimamishwa na kuwataka kutojihusisha na siasa ndani ya chama hicho hadi uamuzi huo utakapoamuliwa vinginevyo...
Ifike mahala nchi iwe na vyama viwili tu. Mi ningekuwa msajiri ningefula act, nccr, chauma, umoja pary nk na kubaki na chadema na ccm tu.

Kwa upande wa dini ningefuta madhebu yote ya ukristu nikabaki na katoliki na uislamu tu. Waliobaki watachagua wakajoin wapi. Vinginevyo ni kero na vurugu.
 
Msajili anarudia yale yale aliomfanyia Maalim Seif na CUF yake na huwa anafanya haya kwa maelekezo ya Wakubwa.
Kosa la Mbatia ni kukataa kufika mbele ya ile task force ya Rais akiungana na Chadema
Kwa nguvu alizo nazo sitashangaa akimtambua Halima Mdee kuwa mwenyekiti wa CHADEMA na kuagiza ruzuku zote walizo zisusia kina Mbowe apewe
 
Back
Top Bottom