Siyo Nape tu, ukweli ni kwamba vyakula tunavyokula vina madhara makubwa sana mwilini haswa kwenye flexibility ya mwili. Wengi watakubaliana na mimi kuwa hawa jamaa wa Asia misosi yao iko calculated vizuri, wengi wao wako njema sana kiafya kuliko hii mijitu ya ulaya na marekani.
Waafrica wengi tunaponea kwenye hizi kazi ngumu ngumu kama za shamba nk, lakini ukimkuta mtu aliyejimwaga ofisini na ukimfuatilia misosi anayokula ni hatari kwa afya. Wengi hawataki kuandaa misosi yao wenyewe, utakuta mtu anakula misosi yenye mafuta kibao ukijumlisha na huduma mbovu za maji basi yale mafuta yanageuka sumu ndo unakuta mtu hawezi kukaa kwenye mkeka akakunja miguu kuelekea kwa ndani.
Wito wangu, tubadilikeni, kula misosi ambayo ni natural zaidi (ambayo haijapikwa sana au isiyotiwa mafuta itasaidia kujenga afya zetu).