Msafara wa Makamu wa Rais Mbeya....

Msafara wa Makamu wa Rais Mbeya....

Asimame japo lisaa wakati anajua dhahiri hakubaliki yeye pamoja na chama chake

Ile ilikuwa kujihami. Kwa spidi ile kama gari mojawapo kwenye msafara lingepata ajali ingekuwa hatari sana tungesimulia mwengine. Katikati ya jiji kwa spidi ile?Haikubaliki
 
hii ndio halihalisi na viongozi wetu wajue wakati wa kudanganywa umepitwa na wakati. Mbeya ni chimbuko lingine la demokrasia. Alipopolewa baba Riz One, mama Riz One, Vuayi Naodha sembuse yeye. It's just a sec, minute freedom will come
 
hii ndio halihalisi na viongozi wetu wajue wakati wa kudanganywa umepitwa na wakati. Mbeya ni chimbuko lingine la demokrasia. Alipopolewa baba Riz One, mama Riz One, Vuayi Naodha sembuse yeye. It's just a sec, minute freedom will come

Maneno mazito hayo!
 
Makamu wa Rais Dk.Mohammed Bilal amepita muda si mrefu eneo la Mwanjelwa jijini Mbeya akiwa na msafara wake wenye magari kadhaa.

Kilichoshitua watu wengi ni ile kasi ya mbio za mwenge waliyopita nayo bila kujali kwamba wananchi walijipanga kwa wingi barabarani ili waweze kumsalimia kiongozi wao japo kwa kumpungia mkono.

Kasi waliyopita nayo ilipelekea wananchi kadhaa walikuwa katika vikundivikundi wabakiwakijiluiza kulikoni? Wengine walikwenda mbali zaidi na kudai "ameshauriwa na viongozi wa CCM kwamba eneo hilo ni hatari hivyo wapite kwa spidi kali kama vile wanakimbiza mwenge kwa hofu ya kupopolewa?"


MASIHIHISHO KIDOGO MKUU,

Umati wa watu pembezoni mwa barabara kati ya maeneo ya Soweto, Mwanjelwa mpaka Mafiati ulitokana na kuzuiliwa kwa magari yatokayo katikati ya jiji na yale yatokayo Iyunga na Mbalizi kwa muda mrefu bila msafara kupita na hivyo abiria wengi kuamua kutembea kwa miguu pembezoni mwa barabara kutoka Kadege, Maghorofani, Eso,na Mafiati kuelekea Mwanjelwa na Soweto ;Na ndiyo maana watu wengi walikuwa wakitembea na siyo kusimama.

Wengi wao walilalamika kwa kukwamishwa kwa muda mrefu huku wale ambao safari zao zilikaribia mwisho wakishuka kwenye daladala na kuamua kutembea kwa miguu.

Udhaifu wa polisi,

Polisi walionekana kutojipanga vizuri kimawasiliano. Kwa mfano, nikiwa eneo la Mafiati nilishuhudia baadhi ya askari wakitumia simu za mkononi kuwasiliana kwa taabu na wenzao wa maeneo mengine, hii inatokana na kusumbua kwa mawasiliano ya simu kwa muda mrefu hapa Mbeya, na hasa mtandao wa vodacom.

Mawasiliano mabovu miongoni mwa askari yalipelekea waendesha magari kuingia ingia barabara kuu hata msafara ulipokaribia.

Polisi pia waliamini katika vitisho na mbwembwe kuliko mbinu za kitaalamu, walipita mara nyingi na mbwa wao kwenye magari huku wakiwaliza kwa makusudi ili kuwatisha watu ambao hata hivyo waliishia kuwadharau.Wengine walisema 'mbona siku za vurugu za wamachinga walinywea?'

Kuhusu mwendo mkali,

Binafsi niliutarajia kwani mashushushu waliotangulizwa lazima waliisoma hali halisi kuwa hakukuwa na raia yeyote aliyekuwa na interest na msafara wa bilal zaidi ya watu kuishia kukekejeli ufungwaji wa bendera mpya za sisiemu kwenye miti ya barabarani huku kwa siku mbili mji ukijaa ma-landcruiser hardtop yenye watu wenye T-shirt 'mpya'za kijani.

Nusura mwendo ule uwatokee puani askari waliokuwa kwenye land cruiser ya mwisho(wale FFU wenye sare zenye vifundo kwenye joint zote za miili yao mithili ya nzige atakae kuruka).Wakiwa konani pale Mafiati na spidi zao '120', nusura gari limshinde dereva aliyeamua kutumia breki na hivyo gari kuserereka kwa sekunde kadhaa huku watu wa pembezoni wakishikiria pumzi zao kwani nao wangeathirika ikiwa mambo yangeenda vibaya. Baada ya msafara kupita ilihitaji sekunde 20 tu kumrudisha kila mtumiaji wa barabar mahali pake, hakuna aliyeonekana kujali wala kujiuliza kuhusu msafara.

Nilihuzunishwa na sura za wliokuwemo kwenye magari kuanzia bilal , mkewe , mpaka wapambe wengine. Walionekana wenye sura za wasiwasi sana, namini wakisubiri jiwe la kwanza kurushwa!


.........niliendelea na safari yangu kwenye daladala kurudi nyumbani na mafuta yangu ya taa, niliYOyafuata Mafiati

kutoka Block-T,KWANI VITUO VYA MAFUTA VLIVYOKO MWANJELWA, SOETO, NA MAMA JOHN HAVIYAUZI KWA

MIEZI MITATU SASA.........PALE OILCOM SOWETO TANGAZO KUUKUU LINASOMEKA...'DEAR CUSTOMER WE HAVE

NO KEROSINE, MAY BE TRY TOMORROW!......
HAPO HAKUNA ATAKAYE USUBIRI MSAFARA WOWOTE WA KIONGOZI

WA SERIKARI KWA HAMU HATA IWEJE, WATAPIGWA SANA MAWE SAFARI HII.


 
naomba wale waliobahatika kuwepo tunduma waweke habari kwa ukamilifu, mana mbeya siyo tunduma tu, pia nadhani kiongozi aliongea vyema na vijana walimsikiliza vizuri, wakuu tunasoma kwamba vijana walikuwa na hasira za kutunduliwa bendera zao pale wala siyo kwamba walikuwa na hasira na dr. Bilal bali walitaka kushirikishwa kama wanavyoshirikishwa ccm. sasa hii inavyoletwa hapa kama vile walikuwa na hasira na dr, bilal. nadhani tupeni ukwlei mana ukiacha hilo nimemuona mkuu akiuwa na sugu sasa hii ikoje, au ndio game la kupaka matope na kutuambia yale wayapendayo wengine, nadhani tuwe fair kwenye uandishi kama kweli tunapenda kuimarisha na kuboresha jamvi hili. ushabiki sidhani kama hii ni sehemu yake, tunahitaji great thinkers sio vyenginevyo. mwenye ushabiki wa kupotosha ukweli nadhani humu sio mwahali mwake.
 
NASHANGAA KULIKONI MZEE WA WATU ANAHOFIA NINI, ama ni hizo taarifa za kiinterijensia
 
MASIHIHISHO KIDOGO MKUU,

Umati wa watu pembezoni mwa barabara kati ya maeneo ya Soweto, Mwanjelwa mpaka Mafiati ulitokana na kuzuiliwa kwa magari yatokayo katikati ya jiji na yale yatokayo Iyunga na Mbalizi kwa muda mrefu bila msafara kupita na hivyo abiria wengi kuamua kutembea kwa miguu pembezoni mwa barabara kutoka Kadege, Maghorofani, Eso,na Mafiati kuelekea Mwanjelwa na Soweto ;Na ndiyo maana watu wengi walikuwa wakitembea na siyo kusimama.

Wengi wao walilalamika kwa kukwamishwa kwa muda mrefu huku wale ambao safari zao zilikaribia mwisho wakishuka kwenye daladala na kuamua kutembea kwa miguu.

Udhaifu wa polisi,

Polisi walionekana kutojipanga vizuri kimawasiliano. Kwa mfano, nikiwa eneo la Mafiati nilishuhudia baadhi ya askari wakitumia simu za mkononi kuwasiliana kwa taabu na wenzao wa maeneo mengine, hii inatokana na kusumbua kwa mawasiliano ya simu kwa muda mrefu hapa Mbeya, na hasa mtandao wa vodacom.

Mawasiliano mabovu miongoni mwa askari yalipelekea waendesha magari kuingia ingia barabara kuu hata msafara ulipokaribia.

Polisi pia waliamini katika vitisho na mbwembwe kuliko mbinu za kitaalamu, walipita mara nyingi na mbwa wao kwenye magari huku wakiwaliza kwa makusudi ili kuwatisha watu ambao hata hivyo waliishia kuwadharau.Wengine walisema 'mbona siku za vurugu za wamachinga walinywea?'

Kuhusu mwendo mkali,

Binafsi niliutarajia kwani mashushushu waliotangulizwa lazima waliisoma hali halisi kuwa hakukuwa na raia yeyote aliyekuwa na interest na msafara wa bilal zaidi ya watu kuishia kukekejeli ufungwaji wa bendera mpya za sisiemu kwenye miti ya barabarani huku kwa siku mbili mji ukijaa ma-landcruiser hardtop yenye watu wenye T-shirt 'mpya'za kijani.

Nusura mwendo ule uwatokee puani askari waliokuwa kwenye land cruiser ya mwisho(wale FFU wenye sare zenye vifundo kwenye joint zote za miili yao mithili ya nzige atakae kuruka).Wakiwa konani pale Mafiati na spidi zao '120', nusura gari limshinde dereva aliyeamua kutumia breki na hivyo gari kuserereka kwa sekunde kadhaa huku watu wa pembezoni wakishikiria pumzi zao kwani nao wangeathirika ikiwa mambo yangeenda vibaya. Baada ya msafara kupita ilihitaji sekunde 20 tu kumrudisha kila mtumiaji wa barabar mahali pake, hakuna aliyeonekana kujali wala kujiuliza kuhusu msafara.

Nilihuzunishwa na sura za wliokuwemo kwenye magari kuanzia bilal , mkewe , mpaka wapambe wengine. Walionekana wenye sura za wasiwasi sana, namini wakisubiri jiwe la kwanza kurushwa!


.........niliendelea na safari yangu kwenye daladala kurudi nyumbani na mafuta yangu ya taa, niliYOyafuata Mafiati

kutoka Block-T,KWANI VITUO VYA MAFUTA VLIVYOKO MWANJELWA, SOETO, NA MAMA JOHN HAVIYAUZI KWA

MIEZI MITATU SASA.........PALE OILCOM SOWETO TANGAZO KUUKUU LINASOMEKA...'DEAR CUSTOMER WE HAVE

NO KEROSINE, MAY BE TRY TOMORROW!......
HAPO HAKUNA ATAKAYE USUBIRI MSAFARA WOWOTE WA KIONGOZI

WA SERIKARI KWA HAMU HATA IWEJE, WATAPIGWA SANA MAWE SAFARI HII.



Ezz Chezz: Asante sana kwa nyongeza mkuu. Umekamilisha tukio zima kwa uzuri. Nimekukubali!
 
naomba wale waliobahatika kuwepo tunduma waweke habari kwa ukamilifu, mana mbeya siyo tunduma tu, pia nadhani kiongozi aliongea vyema na vijana walimsikiliza vizuri, wakuu tunasoma kwamba vijana walikuwa na hasira za kutunduliwa bendera zao pale wala siyo kwamba walikuwa na hasira na dr. Bilal bali walitaka kushirikishwa kama wanavyoshirikishwa ccm. sasa hii inavyoletwa hapa kama vile walikuwa na hasira na dr, bilal. nadhani tupeni ukwlei mana ukiacha hilo nimemuona mkuu akiuwa na sugu sasa hii ikoje, au ndio game la kupaka matope na kutuambia yale wayapendayo wengine, nadhani tuwe fair kwenye uandishi kama kweli tunapenda kuimarisha na kuboresha jamvi hili. ushabiki sidhani kama hii ni sehemu yake, tunahitaji great thinkers sio vyenginevyo. mwenye ushabiki wa kupotosha ukweli nadhani humu sio mwahali mwake.

Asante kwa maoni mazuri mkuu. Ukweli ni kwamba watu kadhaa hawakuwa na tatizo na Dk Bilal. Isipokuwa kilichowashangaza ni kile kitendo cha kuwapita kwa kasi ya mbio za mwenge. Kiiungwana angewapungia hata mkono basi akiwa katika mwendo wa kawaida. Wale ni wapiga kura wake, waajiri wake!
 
Back
Top Bottom