jjimmy.jjose
Member
- Dec 12, 2012
- 35
- 4
Wajameni ndo kusema watu wa kanda ya ziwa wanamthamini mtu huyu kwa nafasi ya juu kabisa (Urais) hata kabla ya uchaguzi 2015 ?
Story nzima hapa chini, kazi twende!
MSAFARA wa Waziri wa Ujenzi, John Mgaufuli umeacha maswali jijini Mwanza baada ya kuwa na magari 26,viongozi mbalimbali wa mkoa na kusindikizwa na kuongozwa na pikipiki inayoongoza msafara wa viongozi wa kitaifa akiwa Rais.
Magufuli ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi mkoani Mwanza kwa ajili ya kuangalia barabara ya kutoka uwanja wa Ndege kwenda Igombe ambayo inapaswa kufungwa kupisha ujenzi wa upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza, mbali na kusindikizwa na gari la kamanda wa polisi wa mkoa, pia kila alipopita kulikuwa na askari wa usalama barabarani ambao walikuwa wakizuia magari kuruhusu msafara wake kupita.
Msafara huo ulianzia ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza na kuelekea Igogo saa 3:14 asubuhi kwa ajili ya kukagua ujenzi wa barabara zilizojengwa kwa mawe, kwanza ulitanguliwa na pikipiki ya Jeshi la Polisi iliyokuwa ikisafisha njia na kufuatiwa na gari la Kamanda wa Polisi ambalo lilikuwa limewasha taa na kufuatiwa na gari la Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na nyuma yake gari la Waziri Magufuli na kisha magari mengine ambayo idadi yake ilikuwa zaidi ya 26.
Mbali na kutanguliwa na magari, pikipiki hiyo ya kingora pia katika makutano ya Barabara ya Nyerere na Bungando walikuwa wameandaliwa askari wa usalama barabarani kuzuia magari ili msafara huo kupita pamoja na njia nyingine zinazoingia katika barabara hiyo.
Source : Mwananchi, 12 January 2013
Story nzima hapa chini, kazi twende!
MSAFARA wa Waziri wa Ujenzi, John Mgaufuli umeacha maswali jijini Mwanza baada ya kuwa na magari 26,viongozi mbalimbali wa mkoa na kusindikizwa na kuongozwa na pikipiki inayoongoza msafara wa viongozi wa kitaifa akiwa Rais.
Magufuli ambaye alikuwa katika ziara ya kikazi mkoani Mwanza kwa ajili ya kuangalia barabara ya kutoka uwanja wa Ndege kwenda Igombe ambayo inapaswa kufungwa kupisha ujenzi wa upanuzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza, mbali na kusindikizwa na gari la kamanda wa polisi wa mkoa, pia kila alipopita kulikuwa na askari wa usalama barabarani ambao walikuwa wakizuia magari kuruhusu msafara wake kupita.
Msafara huo ulianzia ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mwanza na kuelekea Igogo saa 3:14 asubuhi kwa ajili ya kukagua ujenzi wa barabara zilizojengwa kwa mawe, kwanza ulitanguliwa na pikipiki ya Jeshi la Polisi iliyokuwa ikisafisha njia na kufuatiwa na gari la Kamanda wa Polisi ambalo lilikuwa limewasha taa na kufuatiwa na gari la Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na nyuma yake gari la Waziri Magufuli na kisha magari mengine ambayo idadi yake ilikuwa zaidi ya 26.
Mbali na kutanguliwa na magari, pikipiki hiyo ya kingora pia katika makutano ya Barabara ya Nyerere na Bungando walikuwa wameandaliwa askari wa usalama barabarani kuzuia magari ili msafara huo kupita pamoja na njia nyingine zinazoingia katika barabara hiyo.
Source : Mwananchi, 12 January 2013