Msaada: Wapi nitapata kiwanja MIllion15?

Zasasule

JF-Expert Member
Aug 12, 2009
1,001
103
Habari zenu wana jf.. Je ni wapi nitapata kiwanja kwa 15million, kiwanja ambacho kimepimwa...

Natarajia ushirikiano wenu..
 
Mimi ninacho Chanika ni robo eka kiko kwenye process ya kupimwa kuna umeme na nyumba nipigie 0715 597591
 
Mie ninacho MVOMELO ni heka moja bei ni mil2,kingine kiko VUNJO bei ni mil2.7,kingine kipo HEDALU kina jaruba moja la mpunga bei 1.5,kingine kipo Mwanakweleke znz bei ni laki 7.5.
Aya sema umepapenda wapi?
 
nahitaji kiwanja DAr es salaam... Na kama kuna uwezakano kiwe karibu na mjini....
 
Mie ninacho MVOMELO ni heka moja bei ni mil2,kingine kiko VUNJO bei ni mil2.7,kingine kipo HEDALU kina jaruba moja la mpunga bei 1.5,kingine kipo Mwanakweleke znz bei ni laki 7.5.
Aya sema umepapenda wapi?

Mvomelo? ndo wapi huko>?? mkoa gani huo?
 
Mvomelo? ndo wapi huko>?? mkoa gani huo?
Ha ha ha ha ha!
Hujui mvomelo weye!
Ok ni morogoro,aya sema sasa,umepapenda eeeeh!

Siku nyingine unapoleta request humu ndani jitahidi kuwa muwazi,usiwe unafichaficha mambo kama dr Slaa bhana!
 
Ha ha ha ha ha!
Hujui mvomelo weye!
Ok ni morogoro,aya sema sasa,umepapenda eeeeh!

Siku nyingine unapoleta request humu ndani jitahidi kuwa muwazi,usiwe unafichaficha mambo kama dr Slaa bhana!
mimi nataka cha vunjo. ila vunjo kubwa kuwa muwazi-vunjo sehemu gani?
 
umepata kiwanja nitafute kwa sms 0659197822 nikuonyeshe viwanja tofautitofauti ujichagulie wewe mwenyewe
 
umepata kiwanja nitafute kwa sms 0659197822 nikuonyeshe viwanja tofautitofauti ujichagulie wewe mwenyewe GOBA aresalaam upande wa karibu na ilipo mbezbeach
 
Ni pale karibu na kwa mh mbunge Lyatonga Mrema,pembeni yake sasa kama unaelekea kwenye duka la mangi,maeneo wanayopikaga mtori pale!
Mzee acha uswahili watu tuko serious. Huyo Lyatonga namsikia tu na huko kiraracha kwao wala sijafika. Hebu fafanua vizuri ninahitaji hicho cha vunjo.Kiko wapi, kimepimwa au shamba na ukubwa wake vipi?
 
Mzee acha uswahili watu tuko serious. Huyo Lyatonga namsikia tu na huko kiraracha kwao wala sijafika. Hebu fafanua vizuri ninahitaji hicho cha vunjo.Kiko wapi, kimepimwa au shamba na ukubwa wake vipi?
Unataka kwa ajiri ya nini kwani?au kwa ajiri ya noah?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom