Msaada Wakuu, Vipimo Vya Ekari!


Swali la kimfumo wa elimu........why Metric and not Imperial?

Where is relevance?/ coheretion?
 
ekar lazima upate 4900metre square(4900m2) , haijalishi ina upana au urefu au umbo gani!

Inaweza kuwa 70m x 70m au 100m x 49m huo ni mfano
 
Yuko sahihi, ekari moja ni 70 × 70 sq. M.

Kwa kuwasaidia kuna tofauti ya eka na hecta. Eka sana sana ni vipimo vya kiingereza " imperial system" ambayo in yadi 70 x 70 = 4900. Yadi moja ni futi 3. Futi moja ni sentimeta 30 na meta moja ni sentimenta 100. Hizi zinaitwa metric system. Hecta moja in meta 100×100. Kwa ufupi ukitaka kubadili eka kuwa hekta gawanya kwa 2.5 and vice versa.
 
Kwa mazoea ekari inapimwa hatua 70×70. Maana yake halisi ni kwamba inakadiriwa hatua ya mtu mzima ni futi 3 yaani yadi moja. Kwa wenye simu za android mnaweza kutumia apk ya "area measure" ambayo ni free, kuhakiki maeneo. Apk hii inatumia GPS na unaweza kupima kwa eka au hekta.
 

Mkuu naomba ufafanuzi namna ya kutumia hiyo Apk
 
umeingia chaka mbaya.
 

Usipotoshe..! Tuko kwenye digital age mkuu..! wewe bado unatumia vipimo vya kupima eneo kwa kutumia tambo za miguu na ku-determine nyakati kwa kuangalia alama za kivuli ??
 
Soma hapo kwenye Vipimo vya Metriki. Kimsingi,70 kwa 70 ni hekta. Ekari ni 70 kwa 35.
Mkuu unapotosha uma. Hiyo 70 kwa 35 ni kama nusu heka tu. Kipimo sahihi ni 4046sqm sasa ukitaka kupata vipimo vya urefu wa pande zote na ukiona lazima 70 iwepo basi weka 70m x 57.8m. Kuondoa usumbumbufu nawashauri wakulima wapime 70 kwa kwa 58. Ila kwa wanaopima kwakutumia hatua za miguu ni bora wakapima hatua 70 kwa 65.
 
BTW, Nini kiswahili sahihi cha maneno ''ACRE'' & ''HECTARE'' ? Mara tunasikia eka, heka, hekari, hektari, ekta, etc. so kiswahili sahihi ni ipi kwa maneno hayo mawili ya kiingereza ?
 
Swali la kimfumo wa elimu........why Metric and not Imperial?

Where is relevance?/ coheretion?

Metriki ndio mfumo uliokubaliwa kimataifa. Ni 'mrahisi' kunyumbulika na kuufanyia kazi kwenye nyanja nyingi. Imperial ni wa kiingereza na makoloni yake. Pamoja na metriki kukubaliwa kimataifa, bado baadhi ya nchi wanatumia Imperial mfn. Marekani. Uingereza wenyewe wamekua wakihamia metriki japo si kwa kasi kubwa.

Wanahisabati au wataalamu wa vipimo na mizani watadadavua zaidi kama wamo humu.
 
ekar lazima upate 4900metre square(4900m2) , haijalishi ina upana au urefu au umbo gani!

Inaweza kuwa 70m x 70m au 100m x 49m huo ni mfano

Siyo 4900 sq metre bali 4900 sq yards na yard moja futi 3 sawa na 0.9144m.
 
Mkuu naomba ufafanuzi namna ya kutumia hiyo Apk

Naomba tuwasiliane "kyarluta@gmail.com"
 
Masuke yupo sahihi sana. Ekari mara zote unatumia kipimo cha yadi na siyo mita! ekari ni yadi 70 kwa 70 na kwa kurahisisha mara nyingi hutumika hatua za miguu ambazo kiukweli ni ndogo kidogo ya mita (kwa watu wengi hatua moja ni kati ya 0.8 mpaka 0.9 ya meta). Ukitumia mita 70 kwa 70 kwa ekari moja huwa inazidi kidogo hivyo ni faida kwa mnunuaji wa eneo na hasara kwa muuzaji wa eneo.

Ukiweka Hekta tu basi hapa unagusa mita, ambapo mita 100 kwa 100 ndio Hekta moja (humo unapata kama ekari 2.4 mpaka 2.5)

Changamoto kubwa katika upimaji wa hatua kutoutiana kati ya mtu mrefu sana au mfupi sana.
 

Nikweli 70×70 Ndio kipimo
 
Ndugu yangu,mambo ya vipimo huwa yanabadilika kutokana na nyakati,matharani vipimo vya Yard vilikuwa ni vya zamani sana lkn sasa tunaenda kwa mita,pale tunapopima urefu.Ukija kwenye ishu ya eneo nijuavyo mimi Ekari moja ni metre square 4000,Wakati hekta moja ni metre square 10,000;Ambapo tunasema hekta moja ni sawa na ekari mbili na nusu.

Sent from my TECNO WX3 using JamiiForums mobile app
 
70 kwa 70 ni fair kabisa kiwanja Cha mpira hicho... Njoo kyela upimiwe heka moja utalia
 
Nimepitia baadhi ya comments bado kuna makosa ya kimsingi. Tunachanganya sana ekari, hekta, yards etc.
1. Ekari 1 ni sawa 4,046.8 sqm na wala sio sqm 4,000 hapo unapunjika 46.8sqm. Na wala sio sqm 4,900 au 70m x 70m hapo unamuibia muuzaji dhambi.
2.Msingi wa mita 70 x 70 unatokana na vipimo vya yards sbb ekari 1 ni sawa na yards 4,840 tukarahisisha miguu 70 kwa 70 na wala sio mita 70 kwa 70. Ktk hali ya kawaida ukipima kwa miguu 70 x 70 haiwezi kuwa sawa na mita 70 x 70 sbb ni vigumu kutembea hatua ya mita 1 mara 70 utachoka na hatua zitapungua urefu hatimae kubaki mule mule kwenye yards 70. Nadhan yards ni kipimo kilichotumika zaidi kipindi cha ukoloni
3.Hekta 1 ni karibu sawa na eka 2.5.
Nipo tayari kusahihishwa
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…