Msaada Wakuu, Vipimo Vya Ekari!

Msaada Wakuu, Vipimo Vya Ekari!

Second Fiddle

JF-Expert Member
Joined
Dec 9, 2014
Posts
469
Reaction score
122
Nilitumia mtu kununua shamba la ekar 30, akilin mwangu nilifikiri nimepata shamba lenye urefu wa meta 1000 na upana wa meta 300 kwa kipimo cha ekar moja ni meta 100 kwa meta 100! Lakn shamba ninalooneshwa ni urefu meta 700 na upana meta 210 kwamba kipimo cha ekar moja ni meta 70 kwa meta 70!? Je ni kweli ekar moja ni 70m¤70m na sio 100m¤100m? Msaada tafadhali!
 
Hekari (hector) na ekari (acres) zinachanganya sana nami sijui ipi ni ipi. Moja vipimo vyake ni 70mx70m
 
Nilitumia mtu kununua shamba la ekar 30, akilin mwangu nilifikiri nimepata shamba lenye urefu wa meta 1000 na upana wa meta 300 kwa kipimo cha ekar moja ni meta 100 kwa meta 100! Lakn shamba ninalooneshwa ni urefu meta 700 na upana meta 210 kwamba kipimo cha ekar moja ni meta 70 kwa meta 70!? Je ni kweli ekar moja ni 70m¤70m na sio 100m¤100m? Msaada tafadhali!

Yuko sahihi, ekari moja ni 70 × 70 sq. M.
 
Nilitumia mtu kununua shamba la ekar 30, akilin mwangu nilifikiri nimepata shamba lenye urefu wa meta 1000 na upana wa meta 300 kwa kipimo cha ekar moja ni meta 100 kwa meta 100! Lakn shamba ninalooneshwa ni urefu meta 700 na upana meta 210 kwamba kipimo cha ekar moja ni meta 70 kwa meta 70!? Je ni kweli ekar moja ni 70m¤70m na sio 100m¤100m? Msaada tafadhali!
Ni sahihi kabisa bila chenga....700*210=147,000sq meter ambayo ukigawanya kwa 30 unapata sq.m 4900 ambayo ni ekari 1
 
Yupo sawa mkuu. Ekari(Acre) 1 ni 70sqM.

Suala la hekta na eka ni mambo ya vipo tu(yaani Imperial na Metric) Acre 1=0.404685642 hector.
 
Second Fiddle, ekari (eka) kwa vipimo vya metriki ni 4,046meta mraba. Yani 63.61 kwa 63.61 ukitaka ekari iliyo mraba.

Hiyo 70 kwa 70 (4,900meta mraba) sijui hata ilipotoka! Labda kurahisisha mahesabu au ilikua ni kipimo cha miguu 70 kwa 70 (miguu kawaida ni pungufu kidogo ya meta).

Hekta ni meta mraba 10,000 yaani meta 100 kwa 100 kwa hekta iliyo mraba. Hekta ni kubwa karibu mara 2 na nusu ya ekari (kwa usahihi ni mara 2.47).
 
Last edited by a moderator:
This is not fair! Hakika ni ngumu kumeza hii! Kama ndo ukweli sina budi kukubaliana nao, lakn why mashulen vipimo vya METRIC vipewe kipaumbele wakat uraian vinatumika vya EMPERIAL? Hakika nafsi yangu itachukua muda kulikubali hili! Kwa vipimo hivi (acre, foot, yard, pounds, ounce, etc) wengi tutaibiwa! Ahsanteni.
 
Ngoja nikaangalie kwenye daftari langu kwa nyuma.

Nitarudi mkui
 
Ni kitu kidogo ww ulichanganya tu,acre ni 100m kwa 40m au vyovyote shida ikupe 4000m za eneo na hecta ni 10,000m za eneo ambapo ni sawa na acre mbili na nusu.
Hilo la sabini kwa sabili ni uwizi tu wa wanunuz maana inakupa 70m kwa 70m sawa na 4900m za eneo ambapo inakua zaidi ya ekari moja
 
Nilitumia mtu kununua shamba la ekar 30, akilin mwangu nilifikiri nimepata shamba lenye urefu wa meta 1000 na upana wa meta 300 kwa kipimo cha ekar moja ni meta 100 kwa meta 100! Lakn shamba ninalooneshwa ni urefu meta 700 na upana meta 210 kwamba kipimo cha ekar moja ni meta 70 kwa meta 70!? Je ni kweli ekar moja ni 70m¤70m na sio 100m¤100m? Msaada tafadhali!

Vipimo ya ekari moja kwa kawaida ni yard 70 kwa yard 70, kwa eneo ambalo ni mraba na kwa eneo ambalo ni mstatili itakuwa ni yard 35 kwa yard 140. Ukitaka kupeleka kwenye vipimo vya kimetriki, yard moja ni sawa na meta 0.9144.
 
Second Fiddle, ekari (eka) kwa vipimo vya metriki ni 4,046meta mraba. Yani 63.61 kwa 63.61 ukitaka ekari iliyo mraba.

Hiyo 70 kwa 70 (4,900meta mraba) sijui hata ilipotoka! Labda kurahisisha mahesabu au ilikua ni kipimo cha miguu 70 kwa 70 (miguu kawaida ni pungufu kidogo ya meta).

Hekta ni meta mraba 10,000 yaani meta 100 kwa 100 kwa hekta iliyo mraba. Hekta ni kubwa karibu mara 2 na nusu ya ekari (kwa usahihi ni mara 2.47).

Upo sahihi kaka.
 
Last edited by a moderator:
Nilitumia mtu kununua shamba la ekar 30, akilin mwangu nilifikiri nimepata shamba lenye urefu wa meta 1000 na upana wa meta 300 kwa kipimo cha ekar moja ni meta 100 kwa meta 100! Lakn shamba ninalooneshwa ni urefu meta 700 na upana meta 210 kwamba kipimo cha ekar moja ni meta 70 kwa meta 70!? Je ni kweli ekar moja ni 70m¤70m na sio 100m¤100m? Msaada tafadhali!

Yaani hapo km amekupimia kwa kutumia mita basi wewe ndo umefaidi!,maana ni kwamba EKARI MOJA ina Square metre 4000.Sasa watu wengi bila kujua hujikuta wakiwauzia maeneo kwa kipimo cha Square metre 4900(yaana mita 70 kwa 70),kitu ambacho wao wanajipunja.Kwenye Hekta moja kuna Square metre 10000,ambapo kuakuwa na Ekari mbili na nusu,sasa ili kuhakikisha nilisema chukua 10000,halafu ugawanye kwa 4000,uone km hautapata Mbili na nusu(2.5).km amekupimia 70*70,basi umefaidi,tena jinyamazie kimya wala usimwambie atakuja kukupunguzia.
 
Eka ni sawa na Sq meta 4000. Hiyo 70x70 ni Yadi sio meta..eka moja ni sawa na yado mraba 4900....hekta moja ni meta mraba 10,000. Tusichanganye vipimo..SI na Vile Imperical..
 
Nilichogundua kwenye hii mada ni kwamba vijana wa siku hizi kwenye vipimo mko sifuri kabisa, sijui huko kwenye shule zenu za kata mnafundishwaje kuhusu vipimo. Haya mambo tulikuwa tunayajua tangu tuko shule za msingi miaka hiyo ya '80! Sasa hapa utakuta mtu amesoma chuo kikuu lakini hajui vipimo, jamani hii ni haki kweli? Kwa ufupi ekari ni mita 70 kwa 70 na hekta ni mita 100 kwa 100 (yaani 4900 msq na 10,000 msq), hivi ndo vipimo tulivyovijua tangu zamani. Hata kwenye hesabu za kujua plant population iwe kwenye ekari au hekta ndivyo vipimo vinavyotumika. hatujawahi kutumia vipimo vya 4046 msq!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom