Msaada wa Ujenzi wa Nyumba

Sina pa kwenda

Senior Member
Nov 18, 2010
113
15
Habari zenu wanajamvini, kwanza kabisa nimezunguka kutafuta viwanja kila sehemu bei juu yaani kila kitu siku hizi kimepanda, msadaa wa kwanza nataka kununua kiwanja nielekezeni ni mitaa ya wapi nitapata kiwanja ambacho bei yake iko pouwa kwa hali ya mtanzania kama tujuanavyo halafu pili nikitaka kujenga nyumba ya kawaida yaani, vyumba vitatu vya kulala, sitting rum, dinning, jiko na choo inaweza ikacost howmuch?
 
Habari zenu wanajamvini, kwanza kabisa nimezunguka kutafuta viwanja kila sehemu bei juu yaani kila kitu siku hizi kimepanda, msadaa wa kwanza nataka kununua kiwanja nielekezeni ni mitaa ya wapi nitapata kiwanja ambacho bei yake iko pouwa kwa hali ya mtanzania kama tujuanavyo halafu pili nikitaka kujenga nyumba ya kawaida yaani, vyumba vitatu vya kulala, sitting rum, dinning, jiko na choo inaweza ikacost howmuch?

viwanja vipo vingi sana unataka wapi na unakiasi gani? kama uko Dar masaky, knyama, mbezi beach viwanja vizuri vinaanzia 50M ila maeneo kama mbagala mwisho, chanika, kongowe, mvumoni, goba kuanzia 2M unapata. ujenzi wa nyumba inategemea na mateial na quality ya nyumba kama fance nk ukiwa na 25M waweza jenga kigumu.
 
viwanja vipo vingi sana unataka wapi na unakiasi gani? kama uko Dar masaky, knyama, mbezi beach viwanja vizuri vinaanzia 50M ila maeneo kama mbagala mwisho, chanika, kongowe, mvumoni, goba kuanzia 2M unapata. ujenzi wa nyumba inategemea na mateial na quality ya nyumba kama fance nk ukiwa na 25M waweza jenga kigumu.

haya maeneo niliyo ya-bold yana-utata tosha
1- masaki, knyama mbezi beach etc... hakuna viwanja vya bei hizo... bei inaanzia 100m kwa maeneo ya mbezi na knyama ila masaki inaanzia usd 300,000- usd 3,000,000. kama huamini soma matangazo kwenye magazeti utakubali mwenyewe
2- kiwanja cha 2m hupati mitaa ya goba na mivumoni labda mbagala
3- nyumba ya 25m 3-bedrooms sio kweli labda ajenge asiweke milango, madirisha, umeme, maji etc...iwe amejenga banda na kulivunika bati..tena bati zenyewe ziwe zileee za kizamani..kitaalamu zinaitwa corrugated iron sheets na sio hizi mnazoita za south afrika au migongo mipana kitaalamu Industrial trough sheets... ni mtazamo wangu wa kitaalamu na kijamii zaidi.
 
Habari zenu wanajamvini, kwanza kabisa nimezunguka kutafuta viwanja kila sehemu bei juu yaani kila kitu siku hizi kimepanda, msadaa wa kwanza nataka kununua kiwanja nielekezeni ni mitaa ya wapi nitapata kiwanja ambacho bei yake iko pouwa kwa hali ya mtanzania kama tujuanavyo halafu pili nikitaka kujenga nyumba ya kawaida yaani, vyumba vitatu vya kulala, sitting rum, dinning, jiko na choo inaweza ikacost howmuch?

Kuwa mwangalifu sana unapotafuta kiwanja na wapi kunafaa.
Mosi wakijua kwamba unatafuta kiwanja kwa nguvu zote kila mmoja atapandisha dau utashtukia mtaji wako unaishia kununua kiwanja.
Yalinipata hayo yanayokupata leo nilitaka kuingia kichwa kichwa wakati bongo nilikuwa nimeaiacha mika kadhaa kumbe kumebadilika sana, nikaamua kutuliza kichwa kwanza na kujifanya kama mdadisi na mwenye kutaka kujua biashara ya viwanja inavyoenda, nakuambia sikuchukua hata wiki nikapata nyumba ya kununua iliyo kuukuu kwa bei chini ya kiwanja na kuharakisha kubadilisha hati miliki wizara ya ardhi hadi le, nikaibomoma na kujenga yangu upya, namshukuru Mungu.

  • Mambo ya msingi unapotafuta kiwanja cha kujenga kama ni nyumba ya kuishi na familia yako, kwanza angalia mambo ya msingi katika maisha kama usafiri, umeme na maji hayo kwangu ni kipaumbele kwanza.
  • Isije kuwa taabu kwako kuvuta umeme toka maili tano ikakuingizia hasara isiyozibika haraka.
  • Usafiri nao ni muhimu kwani haitaingia akilini uwe unaliacha gani kwa jirani akutunzie kwa vile barabara ya kufikia uishika haipitiki hata kwa mkokoteni.
  • Kama eneo unalotaka kujenga linauwezekano wa kuchimba (drill) kisima kwa ajili ya kujitegemea maji maana tunajua wazi huduma ya maji toka huduma za kijamii ni kitendawili tega.
Ukishajiridhisha yaho kati ya viwanja kadhaa ulivyopata, unaweza chagua kimoja ambacho unaona kinakidhi mahitaji yako, ndo maana usiende papara kupata kiwanja fanya uchunguzi wa kutosha na hati miliki kabla hujagawa madafu.
Kisha fanya tadhmini ya ujenzi wa nyumba yako kutokana na ramani yako ambayo na hakika mchoraji atakuwa ameshakufanyia makadirio yake, na kama hujafanya hayo soma paragraph ifuatayo.

Kwa vile gharama za uchoraji ni ghali, jaribu kupunguza gharama kwa kuwaona maofisa wa mipango miji idara ya ujenzi wana ramani nyingi tu hivyo wanaweza kukumegea moja unayoipenda kwa gharama nafuu ukaitumia kufanya makadirio ya gharama za ujenzi wa nyumba yako. Kukuambia kwamba ujenzi wa nyumba yako ni milioni 30 tutakudanganya maana kuna mengi ambayo yanatakiwa kupitia katika kupata mahesabu sahihi kutokana na eneo, hali ya ardhi, mwinuko au tambalare, vifaa utakavyotumia kujenga, na mtindo wa nyumba utakaojenga. Ndio maana utafiti ni muhimu kufanya kabla hujafanya hayo.

Cha msingi hangaikia kupata kiwanja kwanza na baada ya kupata utaweza saidiwa na wazoefu hapa gharama za makadirio ya ujenzi wa nyumba yako.
 
haya maeneo niliyo ya-bold yana-utata tosha<br />
1- masaki, knyama mbezi beach etc... hakuna viwanja vya bei hizo... bei inaanzia 100m kwa maeneo ya mbezi na knyama ila masaki inaanzia usd 300,000- usd 3,000,000. kama huamini soma matangazo kwenye magazeti utakubali mwenyewe<br />
2- kiwanja cha 2m hupati mitaa ya goba na mivumoni labda mbagala<br />
3- nyumba ya 25m 3-bedrooms sio kweli labda ajenge asiweke milango, madirisha, umeme, maji etc...iwe amejenga banda na kulivunika bati..tena bati zenyewe ziwe zileee za kizamani..kitaalamu zinaitwa corrugated iron sheets na sio hizi mnazoita za south afrika au migongo mipana kitaalamu Industrial trough sheets... ni mtazamo wangu wa kitaalamu na kijamii zaidi.
<br />
<br />
Ni kweli kabisa kupata kiwanja kwa milioni mbili maeneo ya goba sio rahisi na kama utapata kitakua ni kidogo sana na kitakua kipo ndani sana porini huko ambapo hata umeme na barabara hamna,mie nilipokuwa natafuta kiwanja kinachoeleweka na karibu na barabara kubwa ya lami walikua wanaanzia milioni 30,kadri unavyoingia ndani kutoka barabara ya lami bei inazidi kupungua,lakini niliweza kubahatisha cha shilingi milion 10, km 2 from barabara ya lami ilikua last year.
Kuhusu garama ya ujenzi hata ukitumia bati za kawaida iko juu sana kwa sasa hivi,ukiwa na milioni 25 hutafika popote itaisha yote.
 
Mkuu nenda kigamboni kuna viwanja vilivyopimwa tofauti vile vya mradi wa mji wa kigamboni, milioni 5 unapata kiwanja unajenga nyumba yako ya kawaida!
Mwakani NSSF wanajenga daraja dakika 30 mzee umefika mjini
 
kigamboni 25km from ferry acre 1 = 1.6mil.
hamna umeme,maji unachimba kwa 2mil. solar unaweka ya 1mil.
 
Mkuu nenda kigamboni kuna viwanja vilivyopimwa tofauti vile vya mradi wa mji wa kigamboni, milioni 5 unapata kiwanja unajenga nyumba yako ya kawaida!
Mwakani NSSF wanajenga daraja dakika 30 mzee umefika mjini

Mkuu ni eneo gani hilo la Kigamboni? Maana kwa sasa nako viwanja bei iko juu mno. Kwamfano huko Tuangoma viwanja vilivyopimwa vinaaznia 10mil na kwenda juu.

NB: Mods unganisheni hii thread na ile yenye kichwa cha habari "Gharama za kujenga nyumba Tanzania" iliyoanzishwa na Guantanamo Bay tarehe 24 Sept. 2010 ambako watu wamechangia sana, mawazo, utaalamu na uzoefu wao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom