Ni vyema kuacha kazi ili kwenda kujitolea kwenye ofisi ambayo itakusaidia kupata kazi nzuri.
ishu ni kwamba mi ni mwalimu wa sekondari nafanya kazi serikalini kwa muda wa miaka 5,niliamua kijiendeleza kwa sasa ninashahada ya maendeleo ya jamii na uchumi, nimetafuta kazi muda mrefu kwa ngazi ya shahada sijabahatika, kuna siku niliona tangazo la kuvolunteer kwenye NGO inayoitwa africa volunteer corps. niliomba nikafanya nao interview nimeitwa nikafanye nao kazi watanilipa kiasi kidogo cha fedha, chakula na malazi ni juu yao.Lengo langu ni kupata uzoefu kwenye hii kazi ya maendeleo ya jamii.