Msaada wa kuandaa yaliyomo kwenye document

Msaada wa kuandaa yaliyomo kwenye document

Mulimila dole

JF-Expert Member
Joined
Jul 15, 2016
Posts
226
Reaction score
267
WAKUU.

Ninaandaa document muhimu ambayo inahitaji kuweka yaliyomo (Table of contents). Nikiri kuwa mimi ni mtumiaji wa kiwango cha kawaida cha Ms office hivyo napata tabu kidogo katika hili.

Changamoto yangu ni kuwa natamani kuweka yaliyomo juu ya makala husika lakini nikijaribu kuweka najikuta maandishi ya ukurasa wa kwanza huhamia wa pili kadri maandishi ya table of contents yanapokuwa mengi.

Je kuna njia ya ku-fix yasi-move?
Nilichofanya kwa sasa nimehamishia ukurasa wa mwisho (Yaliyomo) japo najua sio proper. Naomba muongozo wenu wajuzi wa haya mambo.

Asanteni kabla

SHUKURANI
Wakuu nimekubali kuwa JF ni kisima cha maarifa.
Napenda kutoa shukurani za dhati kwa wale walonisaidia kuweza kuweka yaliyomo (table of contents) kwenye makala yangu. Ni jana tu niliweka post yenye kuomba msaada wa namna ya kutenganisha yaliyomo na makala kuu (main body). Shukurani zangu za pekee ziwaendee Comrades Mediocrist, Mudhyd na Chief Mkwawa kwa ushauri wao ambao umefanikisha kufanya kazi yangu iwe nafuu. Nawatakia wanaJF wote tuwe na moyo huo ili kuijenga jamii yenye uelewa.nawasilisha
 
inatakiwa uelekezwe ukiwa na document, maana ina kamlolongo kidogo
au kama vipi ingia youtube then search tutorials utapata majibu!
 
kwa lugha nyengine unataka namba 1 isitokee yaliyomo sio?

unaweza ukatumia roman numbers kwenye yaliyomo, utangulizi nk halafu pale kazi inapoanzia ndio ukaanza na namba 1

kuyazuia yasimove tumia break nenda page layout halafu chagua section break

kueka roman na namba za kawaida nenda hapa

Numbering Front Matter (Ribbon)
 
kwa lugha nyengine unataka namba 1 isitokee yaliyomo sio?

unaweza ukatumia roman numbers kwenye yaliyomo, utangulizi nk halafu pale kazi inapoanzia ndio ukaanza na namba 1

kuyazuia yasimove tumia break nenda page layout halafu chagua section break

kueka roman na namba za kawaida nenda hapa

Numbering Front Matter (Ribbon)
Asante sana Chief Mkwawa umenipa elimu ya kutosha. Ngoja nitulie mbele ya keyboard bila shaka nitakupa mrejesho. Shukuran
 
Wakuu nimekubali kuwa JF ni kisima cha maarifa.
Napenda kutoa shukurani za dhati kwa wale walonisaidia kuweza kuweka yaliyomo (table of contents) kwenye makala yangu. Ni jana tu niliweka post yenye kuomba msaada wa namna ya kutenganisha yaliyomo na makala kuu (main body). Shukurani zangu za pekee ziwaendee Comrades Mediocrist, Mudhyd na Chief Mkwawa kwa ushauri wao ambao umefanikisha kufanya kazi yangu iwe nafuu. Nawatakia wanaJF wote tuwe na moyo huo ili kuijenga jamii yenye uelewa.nawasilisha
 
Back
Top Bottom