Msaada wa kiushauri tafadhali naomba kwa aliye tayari

adataro

Member
Aug 15, 2012
36
0
Mimi ni kijana nina hamu sana ya kufanya kilimo maeneo ya Bungu - Rufiji lakini kwa kujikongoja. Nina ekari zaidi ya 10 ambazo ninaweza kuanzisha kilimo fulani kizuri. Nakuwa na wakati mgumu sana wa kuamua ni kilimo gani kinaweza kufanyika sababu ya mazingira ya shamba. Shamba lipo eneo ambalo hakuna watu karibu na pia jipya lililoanza kuandaliwa hivi karibuni. Ugumu wenyewe hasa ni kuwa namna nionavyo wanyama hatari wa mazao kama nyani, ngedere na pia naambiwa kuna kima. Mwenye uelewa namna ya kupambana na hiyo hali anisaidie kwa ushauri tu. Natanguliza shukrani zangu za dhati
 
Back
Top Bottom