loykeys
JF-Expert Member
- Feb 19, 2014
- 1,175
- 908
Habari wakuu!
Naomba nipate muongozo wa nini cha kufanya, kuna frame ya biashara nilipata Mjini Morogoro mwaka huu kodi ya pango ilikuwa ni laki mbili kwa mwezi, sasa kwa kuwa nilikuwa na uhitaji wa haraka wa kupata hiyo frame nililipia shilingi laki sita halafu pesa iliyobaki tukakubaliana nitaimalizia mwisho wa mwezi wa tatu.
Lakini mwenye frame alikataa kunikabidhi frame mpaka nitakapolipa pesa iliyobaki so frame ikawa ipo mikononi mwake.
Hapo katikati nikapata majanga ambayo yalikuwa nje ya uwezo wangu sikuweza kupata pesa kwa wakati kulipia so juzi nikawa nimepata kiasi kilichobaki nikaenda kulipia maelezo niliyopata ni kuwa frame imepangishwa mtu mwingine.
Wakuu kikawaida hapa si natakiwa nirudishiwe pesa yangu kwa sababu yeye ameamua kupangisha mtu mwingine na mimi frame hakunikabidhi na wala hakutuandikiana mkataba zaidi ya risiti ya malipo ya frame inayosomeka malipo ya awali ya frame.
Naomba msaada wenu wakuu.
Nawasilisha
Mfano wa risiti yenyewe..
Naomba nipate muongozo wa nini cha kufanya, kuna frame ya biashara nilipata Mjini Morogoro mwaka huu kodi ya pango ilikuwa ni laki mbili kwa mwezi, sasa kwa kuwa nilikuwa na uhitaji wa haraka wa kupata hiyo frame nililipia shilingi laki sita halafu pesa iliyobaki tukakubaliana nitaimalizia mwisho wa mwezi wa tatu.
Lakini mwenye frame alikataa kunikabidhi frame mpaka nitakapolipa pesa iliyobaki so frame ikawa ipo mikononi mwake.
Hapo katikati nikapata majanga ambayo yalikuwa nje ya uwezo wangu sikuweza kupata pesa kwa wakati kulipia so juzi nikawa nimepata kiasi kilichobaki nikaenda kulipia maelezo niliyopata ni kuwa frame imepangishwa mtu mwingine.
Wakuu kikawaida hapa si natakiwa nirudishiwe pesa yangu kwa sababu yeye ameamua kupangisha mtu mwingine na mimi frame hakunikabidhi na wala hakutuandikiana mkataba zaidi ya risiti ya malipo ya frame inayosomeka malipo ya awali ya frame.
Naomba msaada wenu wakuu.
Nawasilisha
Mfano wa risiti yenyewe..