Msaada wa haraka tecno K9 plus

Msaada wa haraka tecno K9 plus

Hakikwanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2010
Posts
4,043
Reaction score
1,012
Ndugu zangu nilinunua simu tecno k9 plus wiki hili, nikawa nimeichaji na imejaa, nikaiwasha na kuanza kuitumia. Cha kushangaza nikacheza video toka youtube ikiwa wima, baada ya muda nikailaza ili iwe full screen, ghafla nikaona screen imekuwa na michirizi ya imekuwa na michirizi ya wima na ulalo na video haina quality. Imenitisha sana kwani nimetumia siku moja. Nilichofanya ni kuwarudishia wenye duka. Naomba wazoefu na mafundi simu hii ni shida gani? Kwani nimetumia tecno matoleo tofauti kwa muda mrefu sana bila shida. Chief Mkwawa na wengine wote msaada wenu. Asanteni
 
Mkiambiwa tecno sio cm hamsikii.
Mimi kiukweli nilianza kutumia tecno mwanzo kabisa kutoka na ufinyu wa bajeti hivyo nimezitumia kwa muda sasa bila shida yeyote mpaka napo amua kuiuza au kugawa. Ila hili toleo limeniacha hoi.
 
Achaneni na simu za hovyo kabisa tecno. Kila siku mtakuwa mnapishana kwa mafundi simu
 
Nini c5 ina miaka miwili na nusu na mwanzo nilikaa na h6 miaka miwili nadhani kutumia tecno inapendeza sana
 
Natumia tecno w5 ina mwaka mmoja na haijawai nisumbua.

Nini c5 ina miaka miwili na nusu na mwanzo nilikaa na h6 miaka miwili nadhani kutumia tecno inapendeza sana
Km unaitumia kwakupiga na kupokea utadumu nayo mda mrefu ila we km ni mtu wa net na YouTube mda wote tecno sio cm. Ingawa kuna baadhi zina betri Nzuri zinadumu. Mwisho wa tecno ni miezi 8 baada ya hapo angalia kwa makini kamera, uwezo wa touch, uwezo wa betri nk, hayo mambo hufifia polepole kwa hakika. Simu mbovu usidhani mpaka ianze kuzima ndo iitwe mbovu, feki Mchina mjanja unaitumia cm bila we kuelewa kuwa sasa imeanza kufifia uwezo wa mambo madogo ambayo ili utambue ni lazima uwe na cm kampuni nyingine km iPhone au Samsung. Tuchukue mfano wa iPhone 4 ya zamani Alafu ufungue kamera au YouTube utakuta pic zake zina ubora wa juu kuliko tecno cx ya sasa
 
Nina Tecno Y2 ni balaa,ilianza kuzingua siku ya tatu tangu nilipoinunua.
Ghafra inazimika yenyewe kuiwasha tena mpaka utoe betri kwanza,na ikijizima utakuta chaji imepungua kishenzi.
Baada yakufuatilia sana nimegundua ni tatizo la kiwandani kwa toleo la Y2,kwani mmiliki yeyote wa simu hii anakumbana na kadhia hiyo.
Kwa ufupi simu za Tecno ni pasua kichwa.
 
Nina Tecno Y2 ni balaa,ilianza kuzingua siku ya tatu tangu nilipoinunua.
Ghafra inazimika yenyewe kuiwasha tena mpaka utoe betri kwanza,na ikijizima utakuta chaji imepungua kishenzi.
Baada yakufuatilia sana nimegundua ni tatizo la kiwandani kwa toleo la Y2,kwani mmiliki yeyote wa simu hii anakumbana na kadhia hiyo.
Kwa ufupi simu za Tecno ni pasua kichwa.
Pole sana mkuu vipi hukuwarudishia?
 
Back
Top Bottom