Msaada (urgently) kuokoa hii familia

BCR

Senior Member
Mar 16, 2011
101
12
Samahani naomba msaada ndugu zangu,
* Ndugu yangu wa kike anaishi Arusha mjini, alitengana na mume wake miaka2 iliyopita kutokana na ukatili na udhalilishaji wa mumewe, alikuwa akimfanyia kila aina ya unyama, alikuwa akishtaki polisi ila jamaa alikuwa anahonga na polisi wala ustawi wa jamii hawakuwa wanachukua hatua, matokeo yake mschana akawa anaambiwa ndiye mkorofi. Kwa ukatili huo alifanyiwa opereshen na kulazwa hospitali mara kadhaa.
* Baada ya kutengana jamaa akabaki na watoto wote wa3, wakike miaka 12, mvulana miaka 9, na mvulana miaka2.
* Watoto wamekuwa wakiishi maisha ya tabu sana kwani baba ni mlevi sana na anabadilisha wanawake sana ilhali wanaish na watoto,
* Kibaya ni unyama anaowafanyia watoto, kwani watoto wamekuwa wakimweleza mama mambo baba anayowafanyia, ni aibu ndugu zangu. Ni unyama unaouma sana.
* Ninaajua kuna wataalam hapa mnaoweza kutusaidia hatua za kufanya huyu dada apatiwe watoto na huyu baba achukuliwe sheria. Alishtaki polisi na serikali za mitaa ila jamaa anahonga ivyo ikawa ngumu haki kutendeka. Natanguliza shukrani ndugu zangu,
 
Back
Top Bottom