Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 485
Ndugu wanajamii nimekuwa mara nyingi nasikia kuna uchawi, huyu kamloga yule! Ama huyu kalogwa au kapigwa juju na mengi mengineyo yanayofanana na hayo.
Hebu nijuzeni maana nashidwa kabisa kuelewa hii ni kitu gani.
Kuna watu siku hizi naambiwa wanautajiri wa kichawi, hii ndo nini.
Kuna mama mmoja nilikuwa nampa ushauri, alikuwa mgonjwa na wanawe wanaishi Dar. Watoto walitaka wampeleke Dar akatibiwe alikataa kwenda huko kwa madai kuwa akienda huko atarudi kwenye Jeneza. Nilipomdadisi zaidi anadai watoto wa siku hizi wanawachukua wazazi na kuwatoa kafara ili watajirike. Akatoa zaidi ya mifano 3 na kudai kuwa watoto hao wanafedha nyingi kwa sababu ama wameua ama wazazi ama watoto ili kupata mali. Nimefanya kautafiti kadogo juu ya madai hayo, nimegundua kuwa baadhi ya vijana ( hasa wa huku uchagani ndiko nilikofanyia huo utafiti mdogo) wana utajiri wa ghafla na wa haraka haraka. Baadhi yao wazazi/mzazi amekufa ama wana watoto mataahira na inasadikika kuwa ni kwa dhana za kichawi. Je huo unaoitwa uchawi ni nini?
Hebu nijuzeni maana nashidwa kabisa kuelewa hii ni kitu gani.
Kuna watu siku hizi naambiwa wanautajiri wa kichawi, hii ndo nini.
Kuna mama mmoja nilikuwa nampa ushauri, alikuwa mgonjwa na wanawe wanaishi Dar. Watoto walitaka wampeleke Dar akatibiwe alikataa kwenda huko kwa madai kuwa akienda huko atarudi kwenye Jeneza. Nilipomdadisi zaidi anadai watoto wa siku hizi wanawachukua wazazi na kuwatoa kafara ili watajirike. Akatoa zaidi ya mifano 3 na kudai kuwa watoto hao wanafedha nyingi kwa sababu ama wameua ama wazazi ama watoto ili kupata mali. Nimefanya kautafiti kadogo juu ya madai hayo, nimegundua kuwa baadhi ya vijana ( hasa wa huku uchagani ndiko nilikofanyia huo utafiti mdogo) wana utajiri wa ghafla na wa haraka haraka. Baadhi yao wazazi/mzazi amekufa ama wana watoto mataahira na inasadikika kuwa ni kwa dhana za kichawi. Je huo unaoitwa uchawi ni nini?