Msaada Tv yangu haitoi sauti kwa channel moja tu.

Msaada Tv yangu haitoi sauti kwa channel moja tu.

Mupirocin

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
1,763
Reaction score
819
Wakuu habari za sasa hivi, poleni na misiba ya maaskofu wetu.
Wadau nina TV aina HISENSE na natumia decoder ya Dstv. Sasa hii decoder nimeunganisha Tv mbili moja chumbani na nyingine sebuleni. Ya sebuleni ni Hisense na inachukua matangazo direct from decoder, wakati ya ndani inatumia indirect. Sasa TV ya chumbani haina shida ila hii ya sebuleni haitoi sauti kwa channel moja tu ya TBC ila channel nyingine zinatoa sauti vizuri tu, kasoro hii channel tu, nimejaribu kuset as factory setting lakini bado imegoma. Sasa sijui shida ni nini isije ikaanza kugoma na channel nyingine baadaye naomba msaada wadau sijui nifanyeje. Natanguliza shukrani
 
Ingekuwa startimes ningekusaidia .. Subiri wadau
 
ingekuwa channel nyingine ningekusaidia ila sio tbc ccm.
 
Mkuu hebu jaribu kuangalia sound subcarrier iliyokuwa selected na TV kwa channel ya TBC ni ya system gani? Inapaswa kuwa system I na sio B/G au K.
 
jaribu kuseti kwenye remote ile semu ambayo inaweza kusikilza redio inawezekana kuna mtu alijaribu kubonyeza imehama frequency mara nyingi hiyo sehemu husababisha sauti ispatikane km bado julisha
 
kwenye remote bonyeza button ya AUDIO nenda sehemu ya audio mode then select and change till the sound comes do not forget to increase volume before that ili sauti ikipatikana uisikie
 
kwenye remote bonyeza button ya AUDIO nenda sehemu ya audio mode then select and change till the sound comes do not forget to increase volume before that ili sauti ikipatikana uisikie

Shukurani na mimi nina tatizo hilo pia
 
Back
Top Bottom