Msaada: Toka May 2023 hadi sasa sijapata passport, nimeambiwa mimi sio mtanzania

Jicholamwewe

JF-Expert Member
Jan 2, 2021
307
348
Waheshimiwa, habari ya kazi na pole kwa majukumu.

Waheshimiwa, mwaka jana 2023, nilibahatika kupata ufadhili wa kwenda masomoni nje ya nchi hivyo nililazimika kutafuta passport. May 2023, nilifika ofisi za uhamiaji Kurasini na viambatanisho vyangu vyote kufanya ombi la passport. Nilifanikiwa kukamilisha ombi langu na kulipia gharama zote.

Waheshimiwa, toka May 2023, hadi sasa sijapata passport. Nilipojaribu kufatilia niliambiwa siwezi kupata passport kwa sababu mimi sio Mtanzania.

Waheshimiwa, mimi nimezaliwa, kukua na kusoma ndani ya mipaka ya Tanzania kama viambatanisho vyangu vinavyoonyesha. Wazazi pamoja na babu zangu ni watanzania.

Waheshimiwa, nimefanya jitihada zote pamoja na kuleta wazazi kutoka kijijini na kwenda nao uhamiaji bila mafanikio. Nimeingia gharama kubwa sana kufuatilia hili swala ukizingatia mimi ni kijana niliyemaliza chuo na bado sijabahatika kupata kazi. Kadhalika kuna uwezekano nikapoteza ufadhili niliobahatika kuupata kama sitapata passport kwa wakati; ndoto na maisha yangu kiujumla yataharibika kwani elimu ndio tegemeo langu kujikwamua kiuchumi.

Waheshimiwa nimekuwa ni MTU wa mawazo sana pamoja na misongo. Naombeni msaada wenu kutokomeza ukosefu wa haki katika nchi hii.

Ni mimi kijana mwenzenu Mwenyezi Mungu awabariki mnapoendelea na majukumu ya ujenzi wa taifa.
 
Sasa hapo ndo shangaa utakuta ambaye sio MTANZANIA na anapewa PASSPORT (mimi namjua mrwanda) alipewa passport na anayo mpaka sasa lakini NIDA walimkatalia kumpa kitambulisho ila PASSPORT anayo ndio jiuilize jijibu mwenyewe.

Sasa hapo MTANZANIA halisi FIGISU kibao dah! ROHO mbaya sana
 
Ungejaribu kwanza kuondoa mikosi uliyonayo au kupunguza ujuaji au kuacha kutukana mamba kabla hujavuka mto au kujaribu kuwa msiri.
Malizana na hizo au mambo yatakaa sawa usisahau za kuambiwa + na za kuzaliwa.

Ndio maana nasema chuo mnaendaga kusomea. Ujinga mambo ya kutumia akili wewe unaenda vijijini kuleta wazazi. Unatakiwa kusoma upepo .

Ya kaisari mpe kaisari, kuna muda wa kuomba haki na kuna muda wa kudai haki!! Kuna muda unamtongoza mke wako wa ndoa
 
Pole sana, mimi nilihangaika sana kupata hapa Mwanza nikaombwa hadi rushwa ya ngono nikakataa, nikasema kama kupata passport ni kazi hivi basi siitaki.

Nikapata kazi Dodoma nikaomba migration ya Dodoma nikaunganishwa na baba mmoja hivi hapo Migration hakuniomba chochote niliombwa Doc za sababu ya kusafiri, G akanitumia barua ya mwaliko na passport copy yake ndani ya wiki mbili nikapata passport, nikasema nimpe asante yule baba aliikataa kata kata akasema nimekusaidia tu.

Tafuta mtu akuunganishe utaipata haraka tu
 
Waheshimiwa, habari ya kazi na pole kwa majukumu.

Waheshimiwa, mwaka jana 2023, nilibahatika kupata ufadhili wa kwenda masomoni nje ya nchi hivyo nililazimika kutafuta passport. May 2023, nilifika ofisi za uhamiaji Kurasini na viambatanisho vyangu vyote kufanya ombi la passport. Nilifanikiwa kukamilisha ombi langu na kulipia gharama zote.

Waheshimiwa, toka May 2023, hadi sasa sijapata passport. Nilipojaribu kufatilia niliambiwa siwezi kupata passport kwa sababu mimi sio Mtanzania.

Waheshimiwa, mimi nimezaliwa, kukua na kusoma ndani ya mipaka ya Tanzania kama viambatanisho vyangu vinavyoonyesha. Wazazi pamoja na babu zangu ni watanzania.

Waheshimiwa, nimefanya jitihada zote pamoja na kuleta wazazi kutoka kijijini na kwenda nao uhamiaji bila mafanikio. Nimeingia gharama kubwa sana kufuatilia hili swala ukizingatia mimi ni kijana niliyemaliza chuo na bado sijabahatika kupata kazi. Kadhalika kuna uwezekano nikapoteza ufadhili niliobahatika kuupata kama sitapata passport kwa wakati; ndoto na maisha yangu kiujumla yataharibika kwani elimu ndio tegemeo langu kujikwamua kiuchumi.

Waheshimiwa nimekuwa ni MTU wa mawazo sana pamoja na misongo. Naombeni msaada wenu kutokomeza ukosefu wa haki katika nchi hii.

Ni mimi kijana mwenzenu Mwenyezi Mungu awabariki mnapoendelea na majukumu ya ujenzi wa taifa.
CCM hoyeee
 
Oh sawa twanzie hapo walipokwambia we si mtanzania
nataka kufahamu haya
  1. Umezaliwa mkoa gani
  2. Kabila lako
  3. Umesoma shule ya msingi ipi kwa jina na iliyopo mkoa gani na wilaya.
  4. Wazazi wako wapo wapi.
Hebu jibu kwanza haya then tuone njia ipi itafunguka
 
Pole sana ,mim nilihangaika sana kupata hapa Mwanza nikaombwa hadi rushwa ya ngono nikakataa nikasema kama kupata passport ni kazi hivi basi siitaki,
nikapata kazi Dodoma nikaomba migration ya Dodoma nikaunganishwa na baba mmoja hivi hapo Migration hakuniomba chochote niliombwa Doc za sababu ya kusafiri G akanitumia barua ya mwaliko na passport copy yake ndani ya wiki mbili nikapata passport ,nikasema nimpe asante yule baba aliikataa kata kata akasema nimekusaidia tu
Tafuta mtu akuunganishe utaipata haraka tu
hela tenaaa
ngono tenaaaaa
mmmh
 
Waheshimiwa, habari ya kazi na pole kwa majukumu.

Waheshimiwa, mwaka jana 2023, nilibahatika kupata ufadhili wa kwenda masomoni nje ya nchi hivyo nililazimika kutafuta passport. May 2023, nilifika ofisi za uhamiaji Kurasini na viambatanisho vyangu vyote kufanya ombi la passport. Nilifanikiwa kukamilisha ombi langu na kulipia gharama zote.

Waheshimiwa, toka May 2023, hadi sasa sijapata passport. Nilipojaribu kufatilia niliambiwa siwezi kupata passport kwa sababu mimi sio Mtanzania.

Waheshimiwa, mimi nimezaliwa, kukua na kusoma ndani ya mipaka ya Tanzania kama viambatanisho vyangu vinavyoonyesha. Wazazi pamoja na babu zangu ni watanzania.

Waheshimiwa, nimefanya jitihada zote pamoja na kuleta wazazi kutoka kijijini na kwenda nao uhamiaji bila mafanikio. Nimeingia gharama kubwa sana kufuatilia hili swala ukizingatia mimi ni kijana niliyemaliza chuo na bado sijabahatika kupata kazi. Kadhalika kuna uwezekano nikapoteza ufadhili niliobahatika kuupata kama sitapata passport kwa wakati; ndoto na maisha yangu kiujumla yataharibika kwani elimu ndio tegemeo langu kujikwamua kiuchumi.

Waheshimiwa nimekuwa ni MTU wa mawazo sana pamoja na misongo. Naombeni msaada wenu kutokomeza ukosefu wa haki katika nchi hii.

Ni mimi kijana mwenzenu Mwenyezi Mungu awabariki mnapoendelea na majukumu ya ujenzi wa taifa.
Sasa ili wakuthibitishe Kuwa wewe ni Mtanzania unatakiwa uwapelekee Tunu kadhaa za Taifa ambazo ni currencies za kitanznia (Fedha halali) ili waamini kweli wewe ni mtanzania..
Vinginevyo hutaweza kupata unachokitaka
 
Tanzania rushwa haikwepeki, hizo gharama ulizotumia kusafirisha wazazi mpaka Dar ungezitumia kuhonga, issue Yako ingekuwa solved.

Tafuta afisa mmoja hapo uhamiaji, muelezee scenario Yako omba akusaidie issue Yako, huku uliahidi kumlinda.

Passport huwa haizidi siku 21, na upo uwezekano wa kuipata ndani ya wiki 1, itategemeana na mazingira Yako.
 
Back
Top Bottom