Msaada tafadhali: Jinsi ya kupata hati ya nyumba

Msaada tafadhali: Jinsi ya kupata hati ya nyumba

yutu

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2013
Posts
1,778
Reaction score
1,226
Miaka miaka iliyoipita niliondokewa na baba yangu kipenzi, baada ya kumaliza matanga wazee wangu wa ukoo waliniita na kunikabidhi nyumba ya marehemu baba kama mmiliki halali.

Nilipojaribu kufatilia hati ya kiwanja au offer sikufanikiwa kuvipata na nyumba yenyewe iko pembezoni ya mji kwahiyo sina hakika kama vilipimwa.

Hivi majuzi baada ya kurudi likizo alikuja mzee mmoja akaniambia kwamba hiki kiwanja alimuuzia mshua na hakummalizia hela hivyo amekuja kuchukua chake.

Sasa hali hiyo imenitisha ikizingatiwa nimekabidhiwa kienyeji (kimila) bila maandishi yoyote, pili sijui nianzie wapi mahakamani au ardhi na nikiitaji mkopo toka benki bila hizo naweza pata?

Nitashukuru kwa msaada wenu asante
 
Uliuliza swali la msingi sana na ni siku nyingi. Nimelikuta hapa na kushangaa JF iliyojaa weledi wa kila fani wameshindwa kukusaidia kwa muda mrefu namna hii? Au kwa vile nawe huku insisit kutafuta majibu ya swali lako?
 
Hivi hati ya nyumba si ndiyo hati ya kiwanja?
 
Hivi hati ya nyumba si ndiyo hati ya kiwanja?






We nawe.........sasa umeshataja hati za vitu viwili tofauti.....inakuwaje vifanane........kiwanja na nyumba ni kitu kimoja kwani...........hizo ni hati mbili tofauti.......hati ya nyumba inawakilisha nyumba......hati ya kiwanja inawakilisha kiwanja........wanatoa tofauti kwasababu unaweza ukawa na kiwanja but kisiwe na nyumba so kitahitaji cheti cha umiliki.........
 
Ndugu kamilisha kwanza taratibu za mirathi mahakamani kisha ofisi za ardhi za manispaa kilipokiwanja husikawatakupa taratibu za kufuata
 
Habari wapendwa, natumai muwazima. Nawapenda sana ingawa sijawahi kuwaona.

Sasa jamani nahitaji muongozo kuhusu namna ya kupata hati ya nyumba. Nina ndugu yangu amefiwa na baba yake miezi michache iliyopita, anaishi na mama yake.

Sasa wana nyumba ipo hapa Dar na ameagizwa na bi mkubwa wake kufuatilia documents za nyumba, yaani hati ya mjengo, sasa hajui pa kuanzia nikaona nililete hapa hili swala maana sijajua namshaurije kuhusu wapi aanzie kufuatilia.

Maana hili jiji sasa hivi linanuka utapeli na ufisadi.Haya, kwa wale wazalendo mnaofahamu kuhusu haya maswala naomba mje fasta tuzungumze tusaidie huyu mtu.
 
We nawe.........sasa umeshataja hati za vitu viwili tofauti.....inakuwaje vifanane........kiwanja na nyumba ni kitu kimoja kwani...........hizo ni hati mbili tofauti.......hati ya nyumba inawakilisha nyumba......hati ya kiwanja inawakilisha kiwanja........wanatoa tofauti kwasababu unaweza ukawa na kiwanja but kisiwe na nyumba so kitahitaji cheti cha umiliki.........

Nijuavyo mimi hati ya kiwanja hubeba na vitu vyote vilivyopo juu ya kiwanja husika.
Sasa kama kiwanja kina nyumba, hati ya kiwanja ndio huitwa hati ya nyumba!
 
We nawe.........sasa umeshataja hati za vitu viwili tofauti.....inakuwaje vifanane........kiwanja na nyumba ni kitu kimoja kwani...........hizo ni hati mbili tofauti.......hati ya nyumba inawakilisha nyumba......hati ya kiwanja inawakilisha kiwanja........wanatoa tofauti kwasababu unaweza ukawa na kiwanja but kisiwe na nyumba so kitahitaji cheti cha umiliki.........

Mwenye kiwanja ndo mwenyenyumba...in otherwords...kiwanja ni nyumba
 
Taratibu zipo 3. Kwanza ni eneo lipo kwenye mchoro wa Mipango Miji? Na hicho kiwanja kipo sahihi kwenye mchoro, Pili limepimwa na kupewa namba ya Kiwanja? Utakapokuwa na vitu hivi viwili ndio unaweza kuandaa hati. Ila kama vyote ha vipo
 
Navyojua kama eneo alijapimwa lazima ulipie kupimiwa au mji organize watu wa eneo hilo mpimiwe as a block ila kama ni ww peke yako mpunga utakuwa mrefu...kwanza kamilisha taratibu za mirathi then uendee ofisi za arthi kwa maelezo zaidi ila uandae kama kilo tano ivi coz mpaka upate ile hati original sio mchezo ambayo huwa ni karatasi gumu ivi la kijani...
 
Ok, kwanza kiwanja kiwe kimepimwa aanzie hapo kwanza
 
Jamani mambo vipi?
Nina shamba langu la hekari 5. Naitaji kupata Hati au document yoyote ya umiliki ya serikali.

Kuna yeyote anayejua mchakato wake anisaidie?
 
Ah ah ah uhii; illegal migrant; nimecheka alone
nini tena mkuu
1467700933989.jpg
jamaa alinisaidia nikapata hati
 
nategemea amenunua au amemiliki/kishwa kihalali ambapo lazima atakuwa na nyaraka ya serikali ..sasa kama una shamba ambalo halina nyaraka sijui atakuwa amelipataje.....aende serikali za mtaa wa eneo husika watampa utaratibu .....@divine nitake radhi mkuu
 
nategemea amenunua au amemiliki/kishwa kihalali ambapo lazima atakuwa na nyaraka ya serikali ..sasa kama una shamba ambalo halina nyaraka sijui atakuwa amelipataje.....aende serikali za mtaa wa eneo husika watampa utaratibu .....@divine nitake radhi mkuu
There ua; alihitaji muongozo kama huo jmn. Sasa ww fastaa ukarusha No ya simu. Dunia haiaminiki.

Ok nisamehe bure if ulikwazika
 
Back
Top Bottom