Msaada tafadhali, Dar-Mwanza

Msaada tafadhali, Dar-Mwanza

ELAFU

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2014
Posts
410
Reaction score
151
Habari jamani wanajamvi! Leo mnyonge mimi kampuni ya mabasi ya ZUBERI imenionea kwa kunibadilishia gari bila taarifa ya msingi wala samahani ni kuniambia abiria wote tutasafiri na KISESA EXPRESS. Nikaitazama gari yenyewe kwa bahati nzuri nikaridhika nayo, sikuleta shida tena. Sasa kazi ipo kwenye hili basi. Huku mwanzo tu dereva ameanza kuovertake vibaya, speed ya ubungo-kibaha tu inaonesha mbele ni balaa. Pia sikuwa nalijua hili bus wala rekodi zake za safari. Naomba nisaidiwe namba za polisi wa usalama barabarani kwa njia hii ili kukiwa na lolote niweze kuchukua hatua mapema zaidi ya kulalamika tu. Natanguliza shukrani.
 
Chukua nambari ya Ustaadh Kova 0754034224.

Pia ya Ustaadh Mpinga yule wa usalama barabarani hii hapa 0754360046
 
Chukua nambari ya Ustaadh Kova 0754034224.

Pia ya Ustaadh Mpinga yule wa usalama barabarani hii hapa 0754360046

Huu utaratibu ni mzuri sana wa ku update mwendokasi wa basi ukiwa safarini haswa kwenye jf.Wakuu wa jeshi huwaga wanaingia humu,inaweza kuleta impact fulani.
 
Humo humo kweny basi kuna namba SUMATRA ambazo unapiga bure ba kuwaeleza mwendo wa basi au mpigie Mpinga kwa hiz namba 0754 360 046
 
Jamani nashukuru sana kwa namba, nazisave zote na kutumia muda wowote. Nahofia sana usalama wetu, na madereva wengi huwa hawajali kelele za abiria so mimi ni moja kwa moja polisi. Ahsanteni sana
 
Jamani nashukuru sana kwa namba, nazisave zote na kutumia muda wowote. Nahofia sana usalama wetu, na madereva wengi huwa hawajali kelele za abiria so mimi ni moja kwa moja polisi. Ahsanteni sana
 
Trafick akisimamisha akauliza vp safar sema mbaya uone abiria wenzako watavyokuzodoa lkn mkipata ajali wanalalamika dereva alikua anakimbia sn
 
Kuhusu kufaulishwa ni kwamba Zuberi na Kisesa ni mali ya mtu mmoja.Kuhusu mwendo jaribu namba hizo ulizopewa na wadau.
 
Mkuu tupe updates za safari,,mmefika wapi mpaka sasa na hali ya safari ikoje

Sasa tunaendelea na safari baada ya kupata lunch hapa Dodoma mjini. Nipo siti #1 , so nilimuambia konda aongee na dereva wake watuendeshe vizuri kwani wakizidisha speed nawapigia simu polisi nikawaonesha na namba nilizopewa humu. So far sijaona tatizo lolote, nawashukuru sana ndugu zangu wa Jf!
 
Sasa tunaendelea na safari baada ya kupata lunch hapa Dodoma mjini. Nipo siti #1 , so nilimuambia konda aongee na dereva wake watuendeshe vizuri kwani wakizidisha speed nawapigia simu polisi nikawaonesha na namba nilizopewa humu. So far sijaona tatizo lolote, nawashukuru sana ndugu zangu wa Jf!

mkuu we kweli abiria mnoko,
unamfundisha dereva kuendesha Gari?,
watu wana haraka zao,wewe unawalostisha!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom