Msaada: Solar powered water pump

Ruge Opinion

JF-Expert Member
Mar 22, 2006
1,838
701
Heshima wanaJF, Naomba msaada/ushauri. Kijijini kwangu kuna shida sana ya maji salama kwa matumizi ya binadamu. Nimekuwa nikifikiri sana namna ya kupambana na hili tatizo bila kungoja serikali na ahadi zake ambazo uchukua miaka kuzitimiza. Bahati nzuri tuko karibu na mto ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo chanzo cha maji tunayotumia. Ila maji yenyewe si salama kwa sababu unatumiwa na wanyama pia, kuna shughuli za kilimo zinzoingiza uchafu (pamoja na madawa ya kilimo) kwenye mto, hata kwa rangi yanaonekana kabisa ni machafu. Suluhisho nililonalo ni kujenga bwawa au matenki kwa ajili ya kuifadhai maji baada ya kuyachuja na kuyasafisha kisha kuyasukuma (pump) mpaka kwenye makazi. Kazi ya kujenga bwawa au matenki siyo ngumu. Ngumu ni njia rahisi ya kuyasukuma maji. Baada ya kutafakari sana nimeona kuwa itakuwa ni gharama nafuu na rafiki kwa mazingira ikipatikana pump inayotumia nguvu ya jua (solar power). Tatizo sijui kama hapa TZ zinapatikana pump za namna hiyo. Mwenye info kuhusu solar powered water pumps, bei zake, zinapatikana wapi, na technical/performance zake anisaidie.
 
Mkuu
Solar water pump zipo japo zina gharama kidogo...nitakupa mfano kidogo
Grundfos submersible pump ya kW 1 inauzwa karibu sh 4.8m kabla ya VAT(hizi pump ni imara na zina performnce nzuri) zinapatikana Davis and Shirtliff pale kamata
Ili kuendesha pump hiyo unahitaji kama Watts 1100 za kuiendesha ambapo ukipata panel za watts 80 utahitaji pc 14 hivi ama za Watts 85 kama 12 hivi.gharama ya panel moja ni wastani wa 650,00-800,000 kutegemeana na make yake(solar panels hazina VAT)
Viunganishi kama contol unit,drop cable,earhrod,earth wire nk vitahitajika..uzuri wa system hii ni kuwa haihitaji battery kama zilivyo solar system nyingine
Kama ulishaandaa chanzo na matenki hapo ukipata hivyo vifaa umemaliza kazi
kama unahitaji kuvuta na kusukuma utatumia pump ya nje badala ya submersible ikiwa na vifaa vya kuchuja taka kabla ya kuvuta maji
More inf cheki na ho jamaa wa Davis & Shirtlif wapo KAMATA,ama Merry water pale Victoria,Pale CRDB Holland House na pia wapo jamaa opp na Continental Hotel Nkrumah
 
Sina uhakika kama solution unayotoka kutumia ni feasible.

  • Economicaly inaweza kuwa ni feasible solution
  • Socialy pia ni fesible kwa wanavijiji
  • Maintanability operational and ease of use ndo naona kuna issue
Wasi wasi wangu usije ukaweka system nzuri tu lakini ikitokea issue fulani au tatizo tiatizo dogo likahitaji mtaalamu kutoka dar kwenda kijijini.

Nakushauri usijilimi t na wazo lako tu. uliza wataalamu wengine uzuri na ubaya wa njia nyingine kama za kutumia upepo

Wazo zuri sana nakupoengeza kwa hilo. hope ukikamilisha utatijuza nasi tuje tucopy
 
Mkuu
Solar water pump zipo japo zina gharama kidogo...nitakupa mfano kidogo
Grundfos submersible pump ya kW 1 inauzwa karibu sh 4.8m kabla ya VAT(hizi pump ni imara na zina performnce nzuri) zinapatikana Davis and Shirtliff pale kamata
Ili kuendesha pump hiyo unahitaji kama Watts 1100 za kuiendesha ambapo ukipata panel za watts 80 utahitaji pc 14 hivi ama za Watts 85 kama 12 hivi.gharama ya panel moja ni wastani wa 650,00-800,000 kutegemeana na make yake(solar panels hazina VAT)
Viunganishi kama contol unit,drop cable,earhrod,earth wire nk vitahitajika..uzuri wa system hii ni kuwa haihitaji battery kama zilivyo solar system nyingine
Kama ulishaandaa chanzo na matenki hapo ukipata hivyo vifaa umemaliza kazi
kama unahitaji kuvuta na kusukuma utatumia pump ya nje badala ya submersible ikiwa na vifaa vya kuchuja taka kabla ya kuvuta maji
More inf cheki na ho jamaa wa Davis & Shirtlif wapo KAMATA,ama Merry water pale Victoria,Pale CRDB Holland House na pia wapo jamaa opp na Continental Hotel Nkrumah
Inkoskaz, nakushukuru sana kwa information hizi muhimu. Samahani sikuweza kurespond mara moja kwa sababu nilikuwa mahali remote kidogo. Thanks a lot. Umenipa pa kuanzia.
 
Sina uhakika kama solution unayotoka kutumia ni feasible.


  • Economicaly inaweza kuwa ni feasible solution
  • Socialy pia ni fesible kwa wanavijiji
  • Maintanability operational and ease of use ndo naona kuna issue

Wasi wasi wangu usije ukaweka system nzuri tu lakini ikitokea issue fulani au tatizo tiatizo dogo likahitaji mtaalamu kutoka dar kwenda kijijini.

Nakushauri usijilimi t na wazo lako tu. uliza wataalamu wengine uzuri na ubaya wa njia nyingine kama za kutumia upepo

Wazo zuri sana nakupoengeza kwa hilo. hope ukikamilisha utatijuza nasi tuje tucopy
Mkuu nakushukuru kwa ushauri wako. Nitatafuta expert advise itakayotoa optimal solution. Thanks a lot.
 
NOW GREAT THINKERS AT WORK.....napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwenu wote.....kwani hii sasa ndo maana halisi ya GREAT THINKERS...ambao hukuna na kusugua vichwa kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya jamii yao na taifa kwa ujumla na si vinginevyo
...bravo jf....BRAVO JF......bravoooooooo
 
Heshima wanaJF, Naomba msaada/ushauri. Kijijini kwangu kuna shida sana ya maji salama kwa matumizi ya binadamu. Nimekuwa nikifikiri sana namna ya kupambana na hili tatizo bila kungoja serikali na ahadi zake ambazo uchukua miaka kuzitimiza. Bahati nzuri tuko karibu na mto ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo chanzo cha maji tunayotumia. Ila maji yenyewe si salama kwa sababu unatumiwa na wanyama pia, kuna shughuli za kilimo zinzoingiza uchafu (pamoja na madawa ya kilimo) kwenye mto, hata kwa rangi yanaonekana kabisa ni machafu. Suluhisho nililonalo ni kujenga bwawa au matenki kwa ajili ya kuifadhai maji baada ya kuyachuja na kuyasafisha kisha kuyasukuma (pump) mpaka kwenye makazi. Kazi ya kujenga bwawa au matenki siyo ngumu. Ngumu ni njia rahisi ya kuyasukuma maji. Baada ya kutafakari sana nimeona kuwa itakuwa ni gharama nafuu na rafiki kwa mazingira ikipatikana pump inayotumia nguvu ya jua (solar power). Tatizo sijui kama hapa TZ zinapatikana pump za namna hiyo. Mwenye info kuhusu solar powered water pumps, bei zake, zinapatikana wapi, na technical/performance zake anisaidie.
Mkuu je ulifanikiwa?
 
Back
Top Bottom