Msaada: Pesa yangu inapotea bila kujua inaenda wapi!

Msaada: Pesa yangu inapotea bila kujua inaenda wapi!

incredible terminator

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2016
Posts
2,533
Reaction score
4,290
Wakuu naombeni msaada kwa anaeweza kunisaidia hili au ambae anajua hii inatokana na nini ni vizuri anishauri,

Nimeanzisha biashara yangu ndogo ila cha kushangaza naweza kuchukua mzigo wa kuuza elfu ishirini na nikaumaliza ndani ya masaa mawili au matatu maana huwa nazungusha ila cha ajabu nikifika nyumban najikuta mfukoni nina elfu mbili (2000) au elfu tatu (3000)

Bila kujua huwa hela inaenda wapi siwezi kusema kama ninapoteza hela maana mifuko yangu iko imara sana afu ukilinganisha kwanini zisipotee hela zote? Zinapungua? Tatzo hili limenitokea takriban siku tatu zilizopita na leo nikajaribu kuzungusha mzigo nikiwa makini sana nilichukuwa mzigo wa elfu kumi na baada ya kuumaliza ndani ya lisaa limoja nikarudi geto na kukagua hela nikajikuta nina elfu mbili mia saba (2700)

Wakuu naombeni Msaada wenu kwa anaejua anaweza kunisaidia namna ya kuthibiti hali hii,

Niko dodoma.
 
Pole sana,Chuma ulete huyo (anakuja na 2000/=,anahitaji kitu cha 500.. ukimrudishia chenji tu na pesa aliokupa ukachanganya pamoja imekula kwako)
 
kila ukiuza nenda kwa wakala mwambie antumie hyo hela niwe nakushikia
 
Pole sana,Chuma ulete huyo (anakuja na 2000/=,anahitaji kitu cha 500.. ukimrudishia chenji tu na pesa aliokupa ukachanganya pamoja imekula kwako)
Mkuu naomba ufafanuzi namna gani ya kumkamata huyo mtu chuma ulete maana nikimdaka nitampa kiminyo ambacho hajawai kupewa tangu auone uso wa dunia maana siwezi kumwangaikia
 
True aende kwa wakala kila akiuza azitupie humo mahesabu Jion.
Mkuu hujanielewa yaani nauza biashara ya kukusanya mia, mia mbili etc ndio maana natembeza kwa hyo niuze mia mbili nitupe mpesa? Na tatzo lipo hivi nikimaliza mzigo mda nahesabu ndio nakuta hizo loss na kibaya zaidi nikiztoa mfukon ili kuhakikisha mahesabu ndio nakuta nimepata loss
 
Wakuu naombeni msaada kwa anaeweza kunisaidia hili au ambae anajua hii inatokana na nini ni vizuri anishauri,
Nimeanzisha biashara yangu ndogo ila cha kushangaza naweza kuchukua mzigo wa kuuza elfu ishirini na nikaumaliza ndani ya masaa mawili au matatu maana huwa nazungusha ila cha ajabu nikifika nyumban najikuta mfukoni nina elfu mbili (2000) au elfu tatu (3000)
Bila kujua huwa hela inaenda wapi siwezi kusema kama ninapoteza hela maana mifuko yangu iko imara sana afu ukilinganisha kwanini zisipotee hela zote? Zinapungua? Tatzo hili limenitokea takriban siku tatu zilizopita na leo nikajaribu kuzungusha mzigo nikiwa makini sana nilichukuwa mzigo wa elfu kumi na baada ya kuumaliza ndani ya lisaa limoja nikarudi geto na kukagua hela nikajikuta nina elfu mbili mia saba (2700)

Wakuu naombeni Msaada wenu kwa anaejua anaweza kunisaidia namna ya kuthibiti hali hii,
Niko dodoma.
Mkuu uwe unatoaga na sadaka ili M/Mungu akulindiage pesa zako
 
Hakuna kitu kinaitwa chuma ulete kwenye biashara wewe mwenyew haufanyi hesabu vizur za mauzo yako
 
Back
Top Bottom