Msaada: Nyoka wananimalizia mayai ya kuku wangu

Huyo ni nyoka MTU
Hapo naona sio nyoka bali kuna mtu anaiba hayo mayai
Nilikuwa na kuku wengi sana na kulikuwa na joka kubwa sana ambalo ni la miaka lakini hata siku moja hajala mayai
Na ni msaidizi mzuri sana kwa vibaka kwani wanajua uwepo wake hapo na hawasogei
Asubuhi huwa anaota jua kwenye barabara ya kuingilia shambani
We achana na nyoka mwizi yupo hapo mvizie tu


Sent from my iPhone using Tapatalk
Sio jamii zote za Nyoka wanakula mayai.

Kuna jamii maalum ambao hawali kitu kingine ni mayai tu, na wakishajua chimbo wanaweka kambi...Mleta mada anaweza kuwa sahihi ni Nyoka, ila pia inawezekana yanaibiwa na Mtu.
 
Hapo mdau ni kuimarisha banda, kufanya fumigation kwa sababu ni shambani huwezi kujua makazi yapo wapi....
Ila pia wapo wanaoamini chumvi hudhuru tumbo la nyoka...labda jaribu kumwaga chumvi kuzunguka banda...ni mtizamo tu...POLE na kila la heri....



Everyday is Saturday........... :cool:
 
Kuna wadudu fulani ni wakubwa mara mbili au tatu ya sisimizi wakubwa, hao wadudu ni wa kupandikiza kazi yao ni kubugudhi nyoka, nenda kwa watu wa mime au maliasili wata kuelekeza vyema jinsi ya kuwapata.
Pia kuna ukoka fulani majani yake ni mapana yale huwakata nyoka na kuwa bugudhi.
 
Mkuu mi nashangaa maneno meeengi, we chukua chumvi hata ya buku mbili na mwaga kwa wingi eneo unaloona kuna njia ya nyoka, akifika tu nyoka anayeyuka au anakufa na hivyo hakuna nyoka yoyote atakaefika hapo. Nyoka na chumvi hawapatani kabisaa maana anayeyuka au kufa fasta.
Ukiona umeweka chumvi na bado mayai yanaibiwa basi hapo sio nyoka ni binadamu
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu.
Ninafuga kuku wa kienyeji hapa shambani kwangu. Kwa kweli kuku wanastawi vizuri na nilishaanza kufurahia matunda ya jasho langu, lakini ghafla nilianza kuona mayai yakipungua wakati kuku wanataga kila siku. Niliamini pasipo na shaka itakuwa nyoka. Hivi majuzi tukafanikiwa kumdaka nyoka mkubwa akiwa amemvamia kuku anayelalia. Kuku alianza kupiga kelele usiku ndipo tulipokurupuka na kwenda kuangalia, tukamkuta ameshameza mayai mawili tayari. Tulifanikiwa kumwua huyo nyoka.

Lakini hata baada ya kumwua huyo nyoka, bado mayai yameendelea kupungua. Pamoja na jitihada za kumwaga mafuta ya taa mlangoni na maeneo yanayozunguka nyumba lakini ufanisi ni mdogo. Hii mbinu ya kumvizia nayo ni ya kubahatisha. Je naweza kutumia mtego gani kuwamaliza nyoka shambani mwangu? Au nitumie dawa gani?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao wadudu wanaitwa sangara, penye sangara nyoka hasogei...
Kuna wadudu fulani ni wakubwa mara mbili au tatu ya sisimizi wakubwa, hao wadudu ni wa kupandikiza kazi yao ni kubugudhi nyoka, nenda kwa watu wa mime au maliasili wata kuelekeza vyema jinsi ya kuwapata.
Pia kuna ukoka fulani majani yake ni mapana yale huwakata nyoka na kuwa bugudhi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi nawaza nikichukua yai nikatoboa kidogo nikaingiza sumu ya panya. Huyo nyoka atakula? Hebu jaribu hii. Toboa kwa ustadhi ingiza sumu ndani ya yake. Pia wanasema ukilichemsha yai halafu umamtegea. Kwa kuwa analimeza halitakaa lipasuke au kuyeyuka na atakufa.
Umeambiwa ni sumu ya panya sio sumu ya nyoka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mi nashangaa maneno meeengi, we chukua chumvi hata ya buku mbili na mwaga kwa wingi eneo unaloona kuna njia ya nyoka, akifika tu nyoka anayeyuka au anakufa na hivyo hakuna nyoka yoyote atakaefika hapo. Nyoka na chumvi hawapatani kabisaa maana anayeyuka au kufa fasta.
Ukiona umeweka chumvi na bado mayai yanaibiwa basi hapo sio nyoka ni binadamu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu fafanua kwa mechanism ipi nyoka huyayuka?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi nawaza nikichukua yai nikatoboa kidogo nikaingiza sumu ya panya. Huyo nyoka atakula? Hebu jaribu hii. Toboa kwa ustadhi ingiza sumu ndani ya yake. Pia wanasema ukilichemsha yai halafu umamtegea. Kwa kuwa analimeza halitakaa lipasuke au kuyeyuka na atakufa.
Hiyo sumu ya panya si inatoka kwa nyoka! Na mimi nawaza..
 
Hii njia itasaidia nini?? Nyoka ana vimeng'enya vyenye ufanisi mkubwa sana. Kama analainisha mfupa itakuwa egg shell?

Hapo ningekushauri uimarishe Banda lako.Nyoka anarhibitiwa na Mnyama Ndege, Nguchiro au Nyegere.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nyoka akila yai lazima alivunje ateme maganda sasa yai lililochemshwa akilila hawezi kuvunja kulivunja likishaenda tumboni sisi ndio tulivyokua tunawamaliza kenge

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo sumu ya panya si inatoka kwa nyoka! Na mimi nawaza..
Is it? Sina hakika inakotoka maana mmmh sumu ya panya ni kiboko. Kuna mbwa mmoja mmiliki wake alitaka kumuua maana aligeuka tishio mpaka kwa familia. Hivyo anachukua tonge la ugali akaweka sumu panya akampa mbwa. Eeeee Bwana Eeee baada ya muda mfupi mba akawa anatoa udenda tu na taratibu akafa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom