fite fite
Senior Member
- Feb 27, 2017
- 113
- 94
Wanajamvi poleni na majukumu,
Naomba nisiwachoshe sana kwa makala ndefu sana. Naeleza tu kwa ufupi ili niweze kusaidiwa maana hii hali inanitesa sana.
Nimekuja kwenye hili jukwaa nikiamini pengine ni tatizo la kiafya au la, watalaamu wa afya na wengine mnaoelewa zaidi ushauri wenu ni muhimu sana.
Mimi ni kijana mwenye miaka 24. Nina tabia zifuatazo
1. Nimekuwa naishi kwa kujitenga sana, muda mwingi nipo peke yangu na hata nikiwa kwenye mkusanyiko wa watu huwa najitenga na kukaa peke yangu.
2. Sina hata rafiki ninayemwamini wa kuongea masuala ya maana na ya maendeleo (kiufupi sina rafiki positively wa kunishauri nafikiri ni kutokana na jamii inavyoniona ninavyojitenga).
3. Nimekuwa naichukia sana jinsia ya kike imetokea automatically, hata kipindi nikiwa nasoma masomo yaliyofundishwa na walimu wa kike nilifeli yote sio kwa makusudi ilitokea hivyo automatically.
4. Napenda sana kukaa sehemu tulivu isiyo na kelele, sipendi kelele za radio, tv, simu, huwa napata maumivu makali ya kichwa ninapopata hizo kelele.
5. Katika mipango mingi ninayoipanga siimalizi, yaani sijawahi kupanga kufanya jambo na likafanikiwa hata kwa 50%.
6. Nikilala siwezagi kuamka ikitokea hakuna mtu wa kuniamsha naweza kushtuka saa kumi na mbili jioni na huwa bado nina usingizi mzito. Kiukweli nateseka jamani sipendi niwe hivi lakini nipo hivi.
7. Nina tabia ya kulamba sana asali mbichi mpaka nisipolamba naumwa (hili tatizo lilinianza 2012 nikiwa nasoma).
8. Mahudhurio yangu kwenye swala/Ibada ni hafifu sana sababu sipendi kelele zinaniumiza kichwa sana.
9. Nina tabia ya kunywa maji sana mpaka mkojo unakuwa mweupe na kufanana na maji kabsa. Ikitokea nimepitiwa na usingizi bila kunywa maji tumbo linaniuma sana.
10. Sipendi matembezi napenda kukaa nyumbani tu mpaka jamii iliyonizunguka inanichukulia kwa mtazamo hasi.
11. Sina raha na maisha yangu. Sina amani wala furaha ya maisha.
12. Nina shida ya masikio kutosikia kwa uzuri. mbali na hili sina tatizo lolote linaloonekana physically.
Kwa ushauri zaidi/rafiki positively
tuma ujumbe +255676 791 188.
NB: Masikio yangu yana hitilafu, nashauri ujumbe wa meseji tu.
Marejeo ya historical background yangu:
2004 niliwahi kupata matatizo ya macho nikiwa kwenye chumba cha mtihani. Ilinichukua miaka 7 kuyahangaikia na kupata nafuu.
2014 Niliwahi kuvamiwa na watu wasiojulikana wakanizimisha walinipora vitu nilivyokuwa nao. Fahamu inarudi nilishtuka nipo hospitalini madaktari wakasema nilichomwa injection ndio iliyopelekea nipoteze fahamu.
Naombeni msaada wenu, nami nataka niishi kama binadamu wengine niwe na furaha na amani bila kuwa na chuki na jinsia yeyote wala mtu yeyote.
Ujumbe huu ni wa kijana mwenye namba tajwa hapo juu. Hana account JF hivyo naomba ushauri utolewe zaidi kupitia namba yake.
Naomba kuwasilisha kwenu
Asanteni sana.
Naomba nisiwachoshe sana kwa makala ndefu sana. Naeleza tu kwa ufupi ili niweze kusaidiwa maana hii hali inanitesa sana.
Nimekuja kwenye hili jukwaa nikiamini pengine ni tatizo la kiafya au la, watalaamu wa afya na wengine mnaoelewa zaidi ushauri wenu ni muhimu sana.
Mimi ni kijana mwenye miaka 24. Nina tabia zifuatazo
1. Nimekuwa naishi kwa kujitenga sana, muda mwingi nipo peke yangu na hata nikiwa kwenye mkusanyiko wa watu huwa najitenga na kukaa peke yangu.
2. Sina hata rafiki ninayemwamini wa kuongea masuala ya maana na ya maendeleo (kiufupi sina rafiki positively wa kunishauri nafikiri ni kutokana na jamii inavyoniona ninavyojitenga).
3. Nimekuwa naichukia sana jinsia ya kike imetokea automatically, hata kipindi nikiwa nasoma masomo yaliyofundishwa na walimu wa kike nilifeli yote sio kwa makusudi ilitokea hivyo automatically.
4. Napenda sana kukaa sehemu tulivu isiyo na kelele, sipendi kelele za radio, tv, simu, huwa napata maumivu makali ya kichwa ninapopata hizo kelele.
5. Katika mipango mingi ninayoipanga siimalizi, yaani sijawahi kupanga kufanya jambo na likafanikiwa hata kwa 50%.
6. Nikilala siwezagi kuamka ikitokea hakuna mtu wa kuniamsha naweza kushtuka saa kumi na mbili jioni na huwa bado nina usingizi mzito. Kiukweli nateseka jamani sipendi niwe hivi lakini nipo hivi.
7. Nina tabia ya kulamba sana asali mbichi mpaka nisipolamba naumwa (hili tatizo lilinianza 2012 nikiwa nasoma).
8. Mahudhurio yangu kwenye swala/Ibada ni hafifu sana sababu sipendi kelele zinaniumiza kichwa sana.
9. Nina tabia ya kunywa maji sana mpaka mkojo unakuwa mweupe na kufanana na maji kabsa. Ikitokea nimepitiwa na usingizi bila kunywa maji tumbo linaniuma sana.
10. Sipendi matembezi napenda kukaa nyumbani tu mpaka jamii iliyonizunguka inanichukulia kwa mtazamo hasi.
11. Sina raha na maisha yangu. Sina amani wala furaha ya maisha.
12. Nina shida ya masikio kutosikia kwa uzuri. mbali na hili sina tatizo lolote linaloonekana physically.
Kwa ushauri zaidi/rafiki positively
tuma ujumbe +255676 791 188.
NB: Masikio yangu yana hitilafu, nashauri ujumbe wa meseji tu.
Marejeo ya historical background yangu:
2004 niliwahi kupata matatizo ya macho nikiwa kwenye chumba cha mtihani. Ilinichukua miaka 7 kuyahangaikia na kupata nafuu.
2014 Niliwahi kuvamiwa na watu wasiojulikana wakanizimisha walinipora vitu nilivyokuwa nao. Fahamu inarudi nilishtuka nipo hospitalini madaktari wakasema nilichomwa injection ndio iliyopelekea nipoteze fahamu.
Naombeni msaada wenu, nami nataka niishi kama binadamu wengine niwe na furaha na amani bila kuwa na chuki na jinsia yeyote wala mtu yeyote.
Ujumbe huu ni wa kijana mwenye namba tajwa hapo juu. Hana account JF hivyo naomba ushauri utolewe zaidi kupitia namba yake.
Naomba kuwasilisha kwenu
Asanteni sana.
