Step by step
JF-Expert Member
- Apr 28, 2014
- 1,189
- 1,324
Habari ndugu zangu.
Ndugu yenu ninasumbuliwa na hali ambayo siielewi hivyo kama kuna mtu amewahi kupitia changamoto kama hii anipe muongozo.
Mimi ni jinsia ME Umri 33. Ninapokuwa na ratiba mpya au jukumu lolote mbele yangu au nikipokea taarifa yeyote ya kushtua au ngeni kwangu napata hali ifuatayo:-
1. Tumbo la kuhara linanibana hivyo lazima niende toilet.
2. Kichefuchefu cha hatari mate yanajaa mdomoni hali inayopelekea kutapika.
3. Dry throat, kuna muda najiona koo linakuwa kama limekaukiwa hivyo naanza kumeza mate, mate yakifika tumboni tu basi natibuka natapika.
4. Hamu ya kula inapotea, yaani hata nikisikia harufu ya chakula tu najisikia kutapika.
5. Kama taarifa hiyo nimeipata usiku na jukumu natakiwa kulifanya kesho basi usingizi utakata nikilala basi ni kidogo sana.
6. Mwili kuisha nguvu kabisa yaani mtu akiniona tu anaona niko dhaifu kama nimeumwa mwezi mzima.
HATUA NILIZOCHUKUA
Nilienda hospitali nikapima presha, figo, Hpyrol, sukari, Malaria vyote viko sawa na siumwi chochote.
MBINU NAZOTUMIA
Ikitokea nimepata jukumu jipya basi huwa nalikataa tu, siendi au natoa udhuru na ili niwe sawa basi natafuta dawa inayonipa usingizi na hamu ya kula inaitwa PHAMACTIN ya maji. Nikinywa hii baada ya muda nalala, na relax nikiamka nakuwa na nafuu naendelea na majukumu japo kwa udhaifu.
Itanichukua hadi siku nne kurudi kuwa normal kabisa. Hii hali inaniumiza, inanichosha sana naombeni msaada nianzie wapi?
Nawashukuru sana
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndugu yenu ninasumbuliwa na hali ambayo siielewi hivyo kama kuna mtu amewahi kupitia changamoto kama hii anipe muongozo.
Mimi ni jinsia ME Umri 33. Ninapokuwa na ratiba mpya au jukumu lolote mbele yangu au nikipokea taarifa yeyote ya kushtua au ngeni kwangu napata hali ifuatayo:-
1. Tumbo la kuhara linanibana hivyo lazima niende toilet.
2. Kichefuchefu cha hatari mate yanajaa mdomoni hali inayopelekea kutapika.
3. Dry throat, kuna muda najiona koo linakuwa kama limekaukiwa hivyo naanza kumeza mate, mate yakifika tumboni tu basi natibuka natapika.
4. Hamu ya kula inapotea, yaani hata nikisikia harufu ya chakula tu najisikia kutapika.
5. Kama taarifa hiyo nimeipata usiku na jukumu natakiwa kulifanya kesho basi usingizi utakata nikilala basi ni kidogo sana.
6. Mwili kuisha nguvu kabisa yaani mtu akiniona tu anaona niko dhaifu kama nimeumwa mwezi mzima.
HATUA NILIZOCHUKUA
Nilienda hospitali nikapima presha, figo, Hpyrol, sukari, Malaria vyote viko sawa na siumwi chochote.
MBINU NAZOTUMIA
Ikitokea nimepata jukumu jipya basi huwa nalikataa tu, siendi au natoa udhuru na ili niwe sawa basi natafuta dawa inayonipa usingizi na hamu ya kula inaitwa PHAMACTIN ya maji. Nikinywa hii baada ya muda nalala, na relax nikiamka nakuwa na nafuu naendelea na majukumu japo kwa udhaifu.
Itanichukua hadi siku nne kurudi kuwa normal kabisa. Hii hali inaniumiza, inanichosha sana naombeni msaada nianzie wapi?
Nawashukuru sana
Sent using Jamii Forums mobile app