RODRIGUEZ NORIEGA DUERTET
Member
- Mar 26, 2018
- 72
- 59
Kama kichwa cha habari kinavyoeleza hapo juu, jana nilikuwa kwenye harakati zangu za kutafuta tonge japo niishi, nikatoka Kimara nikawa nimeshuka Magomeni ili niende NIDA kufuatilia kitambulisho changu,nilitoka Kimara na usafiri wa mwendo mkasi nikashuka usalama ili nionane na mtu alafu niende NIDA.
Niliposhuka kwenye mwendokasi nikavuka barabara nikawa natembea kule road reserve kuelekea Magomeni hospitali,nikatoa simu mfukoni niwasiliane na mshkaji kwamba nitampata eneo gani pale?
Nikapiga simu, jamaa akapokea akawa ananielekeza ghafla nikashangaa simu imechukuliwa kutahamaki ni boda boda iliyotokea nyuma yangu,nikakimbiza bodaboda, nikaifuatilia kwa kutumia pikipiki nyingine lkn wapi akanipotea sikujua hata alienda njia gani.
Nina IMEI ya simu yangu, je nitafanyaje niipate simu yangu?
UPDATE 18-05-2018.
Cha kwanza nliamua kwenda police,baada ya kutoa ripoti na kila kitu,nikapangiwa mpelelezi baada ya kupangiwa mpelelezi sasa kila nikienda naambiwa ametoka mara njoo kesho asubuhi mara njoo kesho jioni na mimi nimuajiriwa kwa wachina,sasa mchina ashachoka na excuse zangu,sasa nikaamua kutafuta mtu wa TCRA akaniambia niende pale TCRA kuna kitengo kinashughulikia mambo hayo.na nliiwaambia ukweli police wananipotezea muda na kusababisha kibarua changu kuwa mashakani.
Nikishaenda pale TCRA Nitawaletea mrejesho.
Niliposhuka kwenye mwendokasi nikavuka barabara nikawa natembea kule road reserve kuelekea Magomeni hospitali,nikatoa simu mfukoni niwasiliane na mshkaji kwamba nitampata eneo gani pale?
Nikapiga simu, jamaa akapokea akawa ananielekeza ghafla nikashangaa simu imechukuliwa kutahamaki ni boda boda iliyotokea nyuma yangu,nikakimbiza bodaboda, nikaifuatilia kwa kutumia pikipiki nyingine lkn wapi akanipotea sikujua hata alienda njia gani.
Nina IMEI ya simu yangu, je nitafanyaje niipate simu yangu?
UPDATE 18-05-2018.
Cha kwanza nliamua kwenda police,baada ya kutoa ripoti na kila kitu,nikapangiwa mpelelezi baada ya kupangiwa mpelelezi sasa kila nikienda naambiwa ametoka mara njoo kesho asubuhi mara njoo kesho jioni na mimi nimuajiriwa kwa wachina,sasa mchina ashachoka na excuse zangu,sasa nikaamua kutafuta mtu wa TCRA akaniambia niende pale TCRA kuna kitengo kinashughulikia mambo hayo.na nliiwaambia ukweli police wananipotezea muda na kusababisha kibarua changu kuwa mashakani.
Nikishaenda pale TCRA Nitawaletea mrejesho.