Msaada:- Ndoto hii inaninyima raha

HAYO NI MAPEPO\MIZIMU kutoka kwa mababu yanataka kukulisisha wewe. TUBU dhambi zote futa ndoto kwa damu ya YESU utapona.
 
Pole sana mkuu. Ila usifadhaike sana kupita kiasi. Ndoto mara nyingi inakuwa ni kivuli cha mkusanyiko wa yale uliyokuwa unawaza/tenda katika mchana wa siku husika, ila vilevile inaendana na ulivyouweka mwili wako usiku au muda huo unapoota..usiteseke sana. Ila ngoma inakuwa nzito utakapounganisha ndoto na hisia zako binafsi!
 
Pole sana Gilesi,Imani ni ndani yako mwenyewe na sio kuhusu kanisa gani uombewe,tengeneza imani yako kisha popote unaweza ombewa cz kweli makanisa ya uongo yamejaa lkn wanamuhubiri yesu huyo huyo,kw hy kama imani yako si haba utapokea uponyaji wa kweli popote pale

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
we miss you sheikh yahya hussein..tatizo dogo sana enzi za uhai wake,angekwambia tembea uchi baharini saa kumi alfajiri,fumba macho wakati unarudi nyumbani na usipande gari lolote...!!!!!
 
Kabla ya kulala jana ulikuwa wapi? ulifanya nini? ulikuwa unawaza nini? ulilalaje? Mshukuru Mungu kwa kila jambo, omba ulinzi wake then move on, ndo is a reflection ya hivyo nilivyovitaja hapo juu though na mengine ya kidunia nayo huja hivyo hivyo.
 
Nitajie tarehe na mwezi uliozaliwa na hio ndoto Kama unakumbuka uliota muda gani!! Nitajaribu kukutafsiria
 
Pole sana giLEsi. Ni kweli kuna ulimwengu usio onekana kwa macho na ndio wenye nguvu ktk maisha yetu. ndoto hiyo ina uhusiano na ulimwengu huo (wa roho).mimi bado ni mtoto na msaada wangu pengine ni kukwambia fanya maombi ya rehema kama walivyo shauri ndugu na ukiweza hudhuria mafundisho ya kanisa la Ukombozi kwa Nabii Malisa kama upo dar ni pale tegeta,skanska ilipo shule ya colnelius girls yeye anafanya deliverance . Mungu akusaidie.
 
Nimeota baba yangu mdogo aliye fariki mwaka jana ananiachia nyumba.
Nyumba ni kubwa sana na tupu.
pia kuna shimo kubwa mafano wa kaburi pembeni yake.
Hii ndoto imeniumiza sana kichwa, nimejaribu kutumia hekima za kiuanadamu nimeshindwa kupata majibu.
Naombeni msada ndugu zanguni kwani hata hapa kibaruani leo ufanisi wangu umeshuka mno

Ndungu yangu giLESi,
Wafu hawajui lolote! Ecclesiastes 9:5,10. Ndoto kama hizo ni roho chafu(evil spirits), sometimes zinaweza kutabiri mambo na yakatokea lakini ni roho za shetani na usiusike nazo. Cha kufanya, piga magoti mwambie BWANA kwamba shetani anakusumbua. hakuna haja ya kwenda kwa mchungaji wala mtu yoyote, piga magoti MWAMBIE BABA!
 
Pole sana ndugu yangu kwa hofu ya ndoto ulinayo, nijuavyo mimi ndoto zimegawanyika katika makundi matatu ambayo ni :-

1.Ndoto inayotokana na M/mungu ndoto hizi mara nyingi huwa zinawajia watu wema, yani kuna wakati mungu anawapa maono watu wema kwa njia ya ndoto, mf Nabii Ibrahim alipoteshwa juu ya kumchinja mwanaye wa pekee na akatambua kuwa ilikuwa ni agizo la m/mungu.

2.Kundi la pili ndoto zinazotokana na yale tunayoyawaza mchana, ubongo huwa na kawaida ya kuyarejea katika usingizi mf kuna wakati mtu anaweza kuwa anawaza ana pesa sana, au amesafiri nje ya nchi nk , fikra hizo ambazo unakuwa nazo wakati wa mchana zinaweza kujirudia ukiwa usingizini na kuwa ndoto.

3.ndoto zinazotokana na mapepo( ndoto mbaya kabisa) mf unaweza oteshwa unakimbizwa na mnyama,mf simba ama umegongwa n.k .

kwa mujibu wa maelezo yako unaweza tafakari na kuona ndoto yako imeangukia katika kundi lipi kati ya hizo tatu.

KINGA:
Hapa inatofautiana kwa mujibu wa mafundisho ya imani mbalimbali mf Uislam unafundisha ndoto mbaya zote kuwa ni zao la shetani/pepo kwa hiyo mtu anapaswa kuomba ulinzi kutoka kwa m/Mungu kwa kusema Audhbillah mina shetwan rajemi( yani najikinga kwako M/mungu kutokana madhara ya shetain aliyelaniwa),na wala hatodhulika mtu huyo , lakini pia yoyote mwenye kuota ndoto mbaya anakatazwa kuwahadithia wengine kwa sababu watu wanatofautiana imani ili wasizulike wengine.
kwa upande wa wakristo hakika sina ujuzi juu ya namna gani wanavyoweza kudili na hali hiyo.
 
Ni ndoto tu. Homa uanza na hisia. Na kemea hofu yako kwa jina la aliye juu! Pepo toookaaaa!
 
Pole sana giLEsi. Ni kweli kuna ulimwengu usio onekana kwa macho na ndio wenye nguvu ktk maisha yetu. ndoto hiyo ina uhusiano na ulimwengu huo (wa roho).mimi bado ni mtoto na msaada wangu pengine ni kukwambia fanya maombi ya rehema kama walivyo shauri ndugu na ukiweza hudhuria mafundisho ya kanisa la Ukombozi kwa Nabii Malisa kama upo dar ni pale tegeta,skanska ilipo shule ya colnelius girls yeye anafanya deliverance . Mungu akusaidie.

Hawa manabii mbona huwa hatuoni mwanzo wao? Tunakuja tu kuwaonea huku juu juu?
 
Yaani umeiota serikali ya JK laivu. Ndivyo atakavyoikabidhi nchi huku akiwa amewachimbia kaburi wabongo. Mweeh!
 
Hao wote ni wahuni, nenda kwenye kanisa ulilobatizwa

Mkuu huwa napenda comment zako lakini ktk hili umenihuzunisha,yawezekana kweli
kwa maoni yako unawaona hawa watumishi ni wahuni lakini unajuaje kuwa ktk hao
yawezekana mmoja wao ndiko kanisani alikobatizwa?!!pia kumbuka kama unavyomuamini
na kumheshimu mtumishi anayekuongoza ndivyo kondoo wa hawa watumishi wanavyowachukulia
.
 
Mkuu huwa napenda comment zako lakini ktk hili umenihuzunisha,yawezekana kweli
kwa maoni yako unawaona hawa watumishi ni wahuni lakini unajuaje kuwa ktk hao
yawezekana mmoja wao ndiko kanisani alikobatizwa?!!pia kumbuka kama unavyomuamini
na kumheshimu mtumishi anayekuongoza ndivyo kondoo wa hawa watumishi wanavyowachukulia
.
Inamaana huyajui mambo ya kihuni yaliyofanywa na watumishi waliotajwa hapo?
Baadhi yake ni wizi.
Wizi wa umeme, mwingine ana kashfa ya uzinzi, yaani ni wahuni tu.
Wapo watumishi ambao kweli Roho waq Bwana yuko juu yao.
Ibada zao hazina shaka yoyote.
Kumbuka, hao wanaojiita manabii ni nani aliyewaka mafuta?
Je wanasifa gani za kinabii?
 
Inamaana huyajui mambo ya kihuni yaliyofanywa na watumishi waliotajwa hapo?
Baadhi yake ni wizi.
Wizi wa umeme, mwingine ana kashfa ya uzinzi, yaani ni wahuni tu.
Wapo watumishi ambao kweli Roho waq Bwana yuko juu yao.
Ibada zao hazina shaka yoyote.
Kumbuka, hao wanaojiita manabii ni nani aliyewaka mafuta?
Je wanasifa gani za kinabii?

Mkuu hata neno la Mungu linakwambia "u nani wewe kumhukumu mtumishi wa mwingine?"
yawezekana wewe unatembea umewashikia hati ya mashtaka wakati wamekwisha tubu kwa
hayo unayowahukumu na uzuri wa Mungu amekwisha wasamehe kazi ni kwako unayewahukumu
wengine badala ya kujiangalia wewe je uko tayari Yesu akirudi sasa"
 
Nimeota baba yangu mdogo aliye fariki mwaka jana ananiachia nyumba.
Nyumba ni kubwa sana na tupu.
pia kuna shimo kubwa mafano wa kaburi pembeni yake.
Hii ndoto imeniumiza sana kichwa, nimejaribu kutumia hekima za kiuanadamu nimeshindwa kupata majibu.
Naombeni msada ndugu zanguni kwani hata hapa kibaruani leo ufanisi wangu umeshuka mno

Nadhani inaashiria kuwa kuna mtu atafariki na wewe utakuwa msimamizi wa mali za huyyo mtu atakaye fariki
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom