Msaada: Ndoa ya ndugu yangu ipo mashakani

Msaada: Ndoa ya ndugu yangu ipo mashakani

Wanawake tujifunze kujitegemea jamani, ndo haya mambo unakuwa limama but still unakula kwa shikamoo kwenye nyumba ya kaka ako. Afu we ni mwanamke, kwa nini uharibu ndoa ya wifi ako? Inawezekana pia kwa kuwa wewe hujaolewa ndo maana unamletea gubu wifi ako.
Anyway, Karma has no menu, u get served what u deserve. So siku ukiolewa jiandae kabisa na mawifi zako, watakupa headache hadi utafurahi.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Huyo mkubwa alishaolewa na anawatoto wawili alijiashisha
 
Inabidi ifike wakati kila mtu akae kwao kama una baba na mama inakuwaje ukabanane na wifi yako huko na ndoa bado changa?
Tuwatunze ndugu wasio na uwezo tu kuepukana na matatizo katika ndoa zetu
 
Yaan mawifi hata ungewapa niniiii sijawah sikia mtu anapendwa na wifi yake ni wachache mnoo wengi ni chuki na wivu
 
Huyo mkubwa alishaolewa na anawatoto wawili alijiashisha

Unakuta aliachika kwa ugumegume wake huyu, kisirani chake ndo anahamishia kwa mwenzake. Akome tena akomazike na Mungu amsimamie Mariam jamani

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
wewe sikiliza waambie kwanza hao wazazi wako uwezo wa kukupa laana hawana. pili waambie wazazi wako kuwa hao dada zako ni watoto wao waliowazaa wewe haikuhusu. tatu waambie hao dada zako wakukome kabisa kufuatilia asali wako wa moyo. nne tafuta sehemu mbali kabisa ukaishi na mkeo. Katika maisha muda mwingine lazima uwe kauzu.
 
waambie hao yani adui wa mwanamke ni mwanamke mwenzie sijui tukoje mi pia dada yangu ana tabia hzo za kiswaz yani wifi yetu hana amani tena yeye sista kaolewa ila wameshhindwa kupanga wapo home jamank anaingilia ndoa hadi bas wapo sana tena sana mi siwapendi mbwa wa aina hii!

Basi mpenzi geniveros wewe jitahidi tu kusimama upande wa wifi ako, na usichoke kumkemea huyo dada ako. Hapa napata picha labda binti ulilazimisha kuolewa kwenye familia iliyokuwa inakupinga, aisee utalia coz hakuna hata wa kukutetea. Mungu atusaidie tusijekuwa na hatia za kuvunja nyumba za watu. It begins with Me, You and Us

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Yaan mawifi hata ungewapa niniiii sijawah sikia mtu anapendwa na wifi yake ni wachache mnoo wengi ni chuki na wivu

wewe acha tu yaaani muda mwingine unaweza kutoamini. ila uzoefu wangu mawifi ambao hawajaolewa au waliachika ni balaa tupu. mwanamme lazima uwe na msimamo na waambie ndugu zako "black and white"
 
ushauri huyo bibie aachane na huyo mume asiyekuwa na maamuzi.. puuumbafu kabisa sasa anamume anatatizo ndani aii
 
Mmh! Huyo mshikaji anatuaibisha wanaume yani umempenda mtoto wa watu mpaka ukaamua kumuoa halafu unaruhusu mjinga mwingine kukuharibia? Acha ulofa we kidume hebu fanya maamuzi kama mwanaume.
 
Ndiyo shida ya kuolewa na mume anayeshikiwa akili!!!
Umeniwahi tulikuwa na wazo linalofanana. Mwanaume huyo hajitambui zamani walikua wanasema mwanaume asiyeweza kuisimamia nyumba yake vema hata uongozi wa ukoo alikua hapewi tena walikuaga na jina lao wanaume dizaini hii.

Ushauri kwa mtoa mada huyo mume hamfai rafiki yako atamsumbua tu lbd kama kampenda sana basi ajiandae na migogoro . Nafikiri hao wazazi wanamjua mtoto wao ndio maana wanafanya yote hayo.
 
wewe acha tu yaaani muda mwingine unaweza kutoamini. ila uzoefu wangu mawifi ambao hawajaolewa au waliachika ni balaa tupu. mwanamme lazima uwe na msimamo na waambie ndugu zako "black and white"
Nafikiri mawifi huwa si tatizo bali tatizo kubwa huwa liko kwa kaka yao ingawa mara nyingi hatupendi kuliangalia hili. Kama kaka yao ana msimamo basi mawifi lazima watakuheshimu lbd mke aanze kuwanyanyasa vinginevyo huwa kuna amani.
 
Back
Top Bottom