Lungutz1
Member
- Jun 23, 2023
- 33
- 67
Kuna fedha natakiwa kui withdraw kwenye moja ya site za malipo online, ambapo option yake kuu ya ku withdraw ni kupitia Paypal account.
Imekuwa ni kikwazo kikubwa kwangu, maana nimejaribu kutengeneza hiyo account ila account bado haikufanikiwa kukidhi vigezo vya kutumika na kupokea malipo, naambiwa inatakiwa iunganishwe na bank details na hapo ndipo nilipokwama. Maana nimejaribu kuilink na banks details ila taarifa hazifungamani na zinakataliwa.
So, nikachukua hatua ya kuomba msaada online kwa wadau kadhaa wajuaji ambao baadae niliwashtukia kuwa huenda ni matapeli, maana walianza kuomba fedha ili wanitengenezee hiyo account na kutakiwa kuwalipa kabla ya kazi, nikashtuka. Kwanini niwalipe kabla ya kazi? Kwa kumbukumbu zangu nilishawahi kushuhudia mtu flani akitapeliwa kwa mfumo huo huo.
Kwa mwenye nia njema ya kunisaidia naomba anisaidie tuzipate hizo hela na nimpe asilimia 30 ya fedha hiyo nitakayo itoa huko paypal ila kulipa kabla sijahudumiwa ni mtego na siwezi.
Kama upo Dar es Salaam na ni mtaalamu wa mambo haya ya fedha za mtandaoni hasa kuhusiana na malipo kwa kutumia paypal account, njoo PM tuangalie namna ya kufanya.
Pia kama upo Dar es Salaam, tunaweza kuonana ili tuifanye kazi hii tukiwa wote tukifanikiwa tunagawana mzigo kama nilivyobainisha hapo juu, tofauti na hapo basi bora hizo pesa zipotelee huko huko.
Mambo ni magumu, uchumi unasumbua watu wengi na utapeli pia unashamiri kila kukicha... ndiyo maana tunapofanya haya inabidi tuchukue tahadhali kubwa.
Ahsanteni na karibuni kwa ushauri juu ya hilo!
Imekuwa ni kikwazo kikubwa kwangu, maana nimejaribu kutengeneza hiyo account ila account bado haikufanikiwa kukidhi vigezo vya kutumika na kupokea malipo, naambiwa inatakiwa iunganishwe na bank details na hapo ndipo nilipokwama. Maana nimejaribu kuilink na banks details ila taarifa hazifungamani na zinakataliwa.
So, nikachukua hatua ya kuomba msaada online kwa wadau kadhaa wajuaji ambao baadae niliwashtukia kuwa huenda ni matapeli, maana walianza kuomba fedha ili wanitengenezee hiyo account na kutakiwa kuwalipa kabla ya kazi, nikashtuka. Kwanini niwalipe kabla ya kazi? Kwa kumbukumbu zangu nilishawahi kushuhudia mtu flani akitapeliwa kwa mfumo huo huo.
Kwa mwenye nia njema ya kunisaidia naomba anisaidie tuzipate hizo hela na nimpe asilimia 30 ya fedha hiyo nitakayo itoa huko paypal ila kulipa kabla sijahudumiwa ni mtego na siwezi.
Kama upo Dar es Salaam na ni mtaalamu wa mambo haya ya fedha za mtandaoni hasa kuhusiana na malipo kwa kutumia paypal account, njoo PM tuangalie namna ya kufanya.
Pia kama upo Dar es Salaam, tunaweza kuonana ili tuifanye kazi hii tukiwa wote tukifanikiwa tunagawana mzigo kama nilivyobainisha hapo juu, tofauti na hapo basi bora hizo pesa zipotelee huko huko.
Mambo ni magumu, uchumi unasumbua watu wengi na utapeli pia unashamiri kila kukicha... ndiyo maana tunapofanya haya inabidi tuchukue tahadhali kubwa.
Ahsanteni na karibuni kwa ushauri juu ya hilo!