Msaada: Mtoto Wangu Amemeza Sarafu ya Sh 50

Msaada: Mtoto Wangu Amemeza Sarafu ya Sh 50

Wana JF, muda mfupi uliopita mtoto wangu wa miaka minne amemeza sarafu ya sh 50. Hasemi kama anapata maumivu yoyote. Nifanyaye kumsaidia?

mpeleke hospital wataitoa,mi kunamtoto wa ndugu yangu alimeza sarafu ya 200 akatolewa,
 
nilishameza sh 1 niliyopewa kama sadaka nikiwa kanisani, nikiwa na umri wa miaka kama 3 na ushee but mpka sasa nipo poa tu na kutokana na kukaa kijijjini mambo mengi huwa yanachukuliwa simpo...mfano ukiumia unaambiwa kojolea na life linaenda....infact my parents walinambia hawakuchukua hatua yoyote na nipo fresh zaid ya miaka 45 now
 
Huyu mpe kiazi mvuringo au ugali ameze bila kutafuna
 
ale tu chakula kama kawaida,muongezee roughages kama matunda na mboga zenye fibres na maji kwa wingi ili asipste constipation,ila ndo muwe mnakagua kinyesi hadi muione hyo hela,ishawahi mtokea my bro akiwa mdogo alimeza sh 20 zile, mama alifanya hvo,unless kama mkiona anaumwa mwahishe hospital
 
Ale mapera ya kufa mtu ila ajiandae kumwaga mchozi!ukishindwa mshindilie ngumi za kufa mtu mgongoni!
 
Mpeleke hospitali apigwe x-ray. Mimi mjukuu wangu alimeza sarafu ya 200, bahati nzuri aliitoa kwa njia ya haja kubwa bila ya matibabu.
 
Atapona tu mimi mwenyewe nilimezaga hamsini nikiwa standard two niliitoa na hakukuwa na madhara yoyote
 
Ale makande yasiyokobolewa kwa wingi halafu asitumie choo cha kivuta.
 
Back
Top Bottom