Mwanamke Asset na Mwanamke Liability

Mwanamke Asset na Mwanamke Liability

Manyanza

Platinum Member
Joined
Nov 4, 2010
Posts
20,579
Reaction score
50,557
UNAPODATE MWANAMKE AMBAYE NI ASSET KWENYE MAISHA YAKO ,

Utakuwa unapata message za aina hizi. 😂😂

(1) Habari za asubuhi mpenzi. Nafurahi ulilala salama. Ukoje leo? Amka ujiandae kwenda kazini. Usisahau kutuma maombi ya ile kazi niliyokwambia jana, na hakikisha unajisitiri vizuri na hali ya hewa .
(2) Mpenzi, nimekumiss sana. Natumaini siku yako itakuwa nzuri. Mimi naelekea kwenye kikao. Tutaongea baadaye, jitunze. Nakupenda.
(3) Ndio mpenzi, nipo dukani nanunua mahitaji ya nyumbani. Wakati mwingine nitakuja na wewe.
(4) Usijiwekee presha mpenzi wangu. Najua utafikia malengo yako. Una msaada wangu wote.
(5) Usisahau kusali kabla hujatoka nyumbani. Kumbuka nguvu zetu ziko kwa Mungu. Nipigie ukiwa tayari kwa maombi ili tuweze kusali pamoja mtandaoni kama utahitaji.
(6) Habari mpenzi, umesharudi kutoka kazini? Siku yako imekuwaje? Natumaini haikuwa ya kuchosha sana. Sasa kunywa kahawa kidogo halafu kaoge upumzike.
(7) Habari za jioni mpenzi. Nilitaka tu kujua una mipango gani kwa ajili ya wikendi yetu.

UNAPODATE MWANAMKE AMBAYE NI MZIGO KWENYE MAISHA YAKO (LIABILITY). 😂😂

(1) Baby itumie elfu kumi haraka.
(2) Habari mpenzi, nakuja kwako tule pizza mchana. Halafu kuna mtu anauza mafuta mazuri, naweza kuchukua moja tafadhali? Nakupenda sana.
(3) Hey handsome, ninunulie data. Pia jirani yangu anauza skinny jeans, viatu vizuri vya Marekani na nywele za Brazilian. Utanijulisha ukiwa tayari kuninunulia hivyo. Nakupenda sana.
(4) Sina nguo ya kuvaa, na marafiki zangu wana birthday wikendi hii Life Power. Ijumaa lazima tuhudhurie zote.
(5) Baby, sijisikii kuongea, tuchat tu.
(6) Mtoto wa Dada angu amemeza sh 50. Nitumie 100k haraka, nikamcheki hospitali.

Mwanaume mwenye busara atachagua kumuoa mwanamke ambaye ni asset kwenye maisha yake, sio Liability.

BINTI

Kama unajiuliza kwa nini wanaume wanakuacha, jiangalie kwanza. Huenda baadhi ya tabia zako zikawa zinachangia changamoto unazokutana nazo katika mahusiano.
 
hongera kama huna tabia mbovu ya kuomba omba hela,

Kama huna mtu nicheki pm tuyajenge 😁
Kiukweli jmn kuomba hela ni kazi asikwambue mtu!nje ya mzazi, kaka, dada ni kipengele...

Napenda mtu yeye aelewe mi ni mwanamke nina matumizi yale ya kawaida tu, anipe yeye mwenyewe sio mpk nimuombe jmn!
Kwanza nikipewa bila kuomba nafurahi najua kuna mtu ananifikiria.

Yaani niombe pale ambapo ss sina namna nimekwama kabisa..
 
Kiukweli jmn kuomba hela ni kazi asikwambue mtu!nje ta mzazi, kaka, dada ni kipengele...

Napenda mtu yeye aelewe mi ni mwanamke nina matumizi yale ya kawaida tu, anipe yeye mwenyewe sio mpk nimuombe jmn!
Kwanza nikipewa bila kuomba nafurahi najua kuna mtu ananifikiria.

Yaani niombe pale ambapo ss sina namna nimekwama kabisa..
Mashallah.....hakika wewe unanifaa
Na appreciate mwanamke wa kaliba yako,

Una mtu?
 
Back
Top Bottom