MSAADA: Mirathi ikiwa wamebaki wajukuu tu

Bingili

JF-Expert Member
Nov 4, 2019
266
698
Wakuu wanasheria

Mzee Bingili alikuwa na watoto wawili wa kiume, Kibaki na Kaputi. Akafariki na kuacha mashamba ekari 100 lakini hakuwahi kugawa mashamba kwa watoto wake Kibaki na Kaputi ila waliendele kulitumia shamba kila mmoja akawa analima anavyojisikia.

Kibaki ana mke mmoja na watoto watano na sio mlimaji sana akawa yeye na watoto wake analima kama ekari 30. Kaputi ambaye ana wake wawili na watoto 15 akawa analima sehemu kubwa ya shamba kama ekari 70

Miaka ikapita Kibaki na Kaputi na wake zao wakafariki, baada ya muda kivumbi kikaanza kwa wajukuu wa Bingili yaani watoto wa Kibaki na Kaputi

Watoto wa Kaputi wanadai ekari 70 ni mali yao wajukuu 15 na iliobaki ekari 30 ni watoto wa Kibaki, yaani ibaki kama ilivyokuwa mazoea kulima.

Watoto wa Kibaki nao wanadai shamba ligawanywe katikati kwakuwa babu yao Bingili alikuwa na watoto wawili tu hivyo shamba ligawanywe kwa muktadha wa Kibaki nusu na Kaputi nusu.

Ikumbukwe kwamba Kibaki na Kaputi walikuwa wanapendana sana kama Ndugu hadi kufa kwao hawakuwahi kugombana kisa shamba ukizingatia shamba lilikuwa kubwa sana na walidhani kugawa mashamba ya baba yao ni kama kuleta utengano.

Sasa walipokufa watoto wao wamekuwa watu wazima na ardhi imekuwa na thamani na uhitaji zaidi wa kulima kila mmoja ndio maana vita ikalipuka

Mimi nipo upande wa Kibaki mwezi wa 12 tunakutana kijijini kikaeleweke maana uadui umekuwa mkubwa mno hadi ni hatari.

Naombeni ushauri wenu kisheria imekaaje maana wengine tunatoka mjini Dslamu tunategemewa ndio vichwa na wajuaji wa kumaliza kesi 😂

Nisije kusimamia vitu kumbe havipo kisheria nikaonekana kituko

Ushauri wenu please
Imekaaje hii kisheria
 
Wakuu wanasheria

Mzee Bingili alikua na watoto wawili wa kiume, Kibaki na Kaputi
Akafariki na kuacha mashamba ekari 100 lakini hakuwahi kugawa mashamba kwa watoto wake Kibaki na Kaputi ila waliendele kulitumia shamba kila mmoja akawa analima anavyojisikia

Kibaki ana mke mmoja na watoto watano na sio mlimaji sana akawa yeye na watoto wake analima kama ekari 30,
Kaputi ambaye ana wake wawili na watoto 15 akawa analima sehemu kubwa ya shamba kama ekari 70

Miaka ikapita Kibaki na Kaputi na wake zao wakafariki, baada ya muda kivumbi kikaanza kwa wajukuu wa Bingili yaani watoto wa Kibaki na Kaputi

Watoto wa Kaputi wanadai ekari 70 ni mali yao wajukuu 15 na iliobaki ekari 30 ni watoto wa Kibaki, yaani ibaki kama ilivyokua mazoe kulima

Watoto wa Kibaki nao wanadai shamba ligawanywe katika kwakuwa babu yao Bingili alikua na watoto wawili tu hivyo shamba ligawanywe kwa muktadha wa Kibaki nusu na Kaputi nusu

Ikumbukwe kwamba Kibaki na Kaputi walikua wanapendana sana kama Ndugu hadi kufa kwao hawakuwahi kugombana kisa shamba ukizingatia shamba lilikua kubwa sana na walidhani kugawa mashamba ya baba yao ni kama kuleta utengano

Sasa walipo kufa watoto wao wamekua watu wazima na ardhi imekua na thamani na uhitaji zaidi wa kulima kila mmoja ndio maana vita ikalipuka

Mimi nipo upande wa Kibaki mwezi wa 12 tuna kutana kijijini kikaeleweke maana uadui umekuwa mkubwa mmno hadi ni hatari

Naombeni ushauri wenu kisheria imekaaje maana wengine tunatoka mjini Dslamu tunategemewa ndio vichwa na wajuaji wa kumaliza kesi
Nisije kusimamia vitu kumbe havipo kisheria nikaonekana kituko

Ushauri wenu please
Imekaaje hii kisheria
Kila mtu ana mtazamo wake lakini kama nikipewa jukumu la kugawa mali. Mali nitampa mwenye hela kwa sababu pesa huzaa pesa. Nimeona biashara nyingi zinakuwa kwa sababu mrithi hana uzoefu na hela. Kuna mzee alikuwa na kampuni ya ujenzi baada ya kumrithisha mtoto mwenye hela wakamkabidhi mtoto wa mke wa kwanza.

Jamaa anaambiwa kuna hela inahitajika kwa ajili ya mafuta, kulipa vibarua jamaa anakataa kutoa. Mwishowe wakavunjiwa mkataba wa miradi na ikabidi walipe faini juu. Muda si mrefu ile kampuni ikafa, uzembe ulikuwa ni aliyepewa alikuwa hana uzoefu na hela.
 
Kila mtu ana mtazamo wake lakini kama nikipewa jukumu la kugawa mali. Mali nitampa mwenye hela kwa sababu pesa huzaa pesa. Nimeona biashara nyingi zinakuwa kwa sababu mrithi hana uzoefu na hela. Kuna mzee alikuwa na kampuni ya ujenzi baada ya kumridhisha mtoto mwenye hela wakamkabidhi mtoto wa mke wa kwanza. Jamaa anaambiwa kuna hela inahitajika kwa ajili ya mafuta, kulipa vibarua jamaa anakataa kutoa. Mwishowe wakavunjiwa mkataba wa miradi na ikabidi walipe faini juu. Muda si mrefu ile kampuni ikafa uzembe ulikuwa ni aliyepewa alikuwa hana uzoefu na hela.

Haki ya mtu na ujinga wake ni vitu viwili tofauti mkuu

Haki yako ni yako tu labda uwe kichaa au mtoto mdogo usiejiweza ndio watapewa wasimamizi wako kusimamia haki zako
 
Itoshe tu kukwambia kuwa mirathi hairithiwi Mkuu Bingili lakini bado sheria haijaacha mali zipotee kiholela hivyo hii kanuni ya jumla inayo mbadala wake.

Kuna mstari mwembamba sana hapo unaohitaji Mahakama kuelezwa vyema maana kidogo tu inaweza kurudi kwenye dhana ya hapo juu kuwa mirathi hairithiwi.

Ila hiyo mirathi inaweza ikawazungusha Mahakamani hata miaka 20 maana ni mtu mwenye maslahi tu aamue kulianzisha kivyake, na hivi wapo wengi mvurugano hapo sio mdogo Mkuu Bingili
 
Itoshe tu kukwambia kuwa mirathi hairithiwi Mkuu Bingili lakini bado sheria haijaacha mali zipotee kiholela hivyo hii kanuni ya jumla inayo mbadala wake.

Kuna mstari mwembamba sana hwpo unaohitaji Mahakama kuelezwa vyema maana kidogo tu inaweza kurudi kwenye dhana ya hapo juu kuwa mirathi hairithiwi.

Ila hiyo mirathi inaweza ikawazungusha Mahakamani hata miaka 20 maana ni mtu mwenye maslahi tu aamue kulianzisha kivyake, na hivi wapo wengi mvurugano hapo sio mdogo Mkuu Bingili
Hebu tudadavulie hii mkuu
 
Wakuu wanasheria

Mzee Bingili alikua na watoto wawili wa kiume, Kibaki na Kaputi
Akafariki na kuacha mashamba ekari 100 lakini hakuwahi kugawa mashamba kwa watoto wake Kibaki na Kaputi ila waliendele kulitumia shamba kila mmoja akawa analima anavyojisikia

Kibaki ana mke mmoja na watoto watano na sio mlimaji sana akawa yeye na watoto wake analima kama ekari 30,
Kaputi ambaye ana wake wawili na watoto 15 akawa analima sehemu kubwa ya shamba kama ekari 70

Miaka ikapita Kibaki na Kaputi na wake zao wakafariki, baada ya muda kivumbi kikaanza kwa wajukuu wa Bingili yaani watoto wa Kibaki na Kaputi

Watoto wa Kaputi wanadai ekari 70 ni mali yao wajukuu 15 na iliobaki ekari 30 ni watoto wa Kibaki, yaani ibaki kama ilivyokua mazoe kulima

Watoto wa Kibaki nao wanadai shamba ligawanywe katika kwakuwa babu yao Bingili alikua na watoto wawili tu hivyo shamba ligawanywe kwa muktadha wa Kibaki nusu na Kaputi nusu

Ikumbukwe kwamba Kibaki na Kaputi walikua wanapendana sana kama Ndugu hadi kufa kwao hawakuwahi kugombana kisa shamba ukizingatia shamba lilikua kubwa sana na walidhani kugawa mashamba ya baba yao ni kama kuleta utengano

Sasa walipo kufa watoto wao wamekua watu wazima na ardhi imekua na thamani na uhitaji zaidi wa kulima kila mmoja ndio maana vita ikalipuka

Mimi nipo upande wa Kibaki mwezi wa 12 tuna kutana kijijini kikaeleweke maana uadui umekuwa mkubwa mmno hadi ni hatari

Naombeni ushauri wenu kisheria imekaaje maana wengine tunatoka mjini Dslamu tunategemewa ndio vichwa na wajuaji wa kumaliza kesi
Nisije kusimamia vitu kumbe havipo kisheria nikaonekana kituko

Ushauri wenu please
Imekaaje hii kisheria
Kama ni Waislam, jambo jepesi sana hilo.

Kwa wengine huko sifahamu.
 
Itoshe tu kukwambia kuwa mirathi hairithiwi Mkuu Bingili lakini bado sheria haijaacha mali zipotee kiholela hivyo hii kanuni ya jumla inayo mbadala wake.

Kuna mstari mwembamba sana hwpo unaohitaji Mahakama kuelezwa vyema maana kidogo tu inaweza kurudi kwenye dhana ya hapo juu kuwa mirathi hairithiwi.

Ila hiyo mirathi inaweza ikawazungusha Mahakamani hata miaka 20 maana ni mtu mwenye maslahi tu aamue kulianzisha kivyake, na hivi wapo wengi mvurugano hapo sio mdogo Mkuu Bingili

Dhana yako inanipa shida kidogo mkuu na nimewahi kuisikia pia

Hebu jazilizia nyama hapo maana tarehe za kwenda nyumbani zimefika mkuu

Sasa kama warithi hawapo wote ina maana shamba litakuwa la nani sasa?

Na je tukikubaliana kugawana itakuwa haina nguvu kisheria?
 
Kila mtu ana mtazamo wake lakini kama nikipewa jukumu la kugawa mali. Mali nitampa mwenye hela kwa sababu pesa huzaa pesa. Nimeona biashara nyingi zinakuwa kwa sababu mrithi hana uzoefu na hela. Kuna mzee alikuwa na kampuni ya ujenzi baada ya kumridhisha mtoto mwenye hela wakamkabidhi mtoto wa mke wa kwanza. Jamaa anaambiwa kuna hela inahitajika kwa ajili ya mafuta, kulipa vibarua jamaa anakataa kutoa. Mwishowe wakavunjiwa mkataba wa miradi na ikabidi walipe faini juu. Muda si mrefu ile kampuni ikafa uzembe ulikuwa ni aliyepewa alikuwa hana uzoefu na hela.

Hii ni kwa mtazamo wako na sio kisheria

Haki ya mtu haipotei kwa kuwa mjinga
 
Hii ni kwa mtazamo wako na sio kisheria

Haki ya mtu haipotei kwa kuwa mjinga
Uwezo wa kumiliki mali unaendana na uwezo wa kifedha. Nikupatie shamba la ekari mia wakati hela ya kuhudumia hata ekari moja huna. Unataka upewe kampuni ambayo inatumia zaidi milioni mia kujiendesha kwa mwezi. Wakati hata bank haiwezi kukopesha hata milioni moja. Mali akipewa mtu asiye na uwezo inaishia kuuzwa au Kupotezwa. Wazungu walijua hilo ndio maana Uingereza kuna property tax ya asilimia 10. Kama unarithi mali ya 1 billion inalipa milioni mia serikalini.
 
Uwezo wa kumiliki mali unaendana na uwezo wa kifedha. Nikupatie shamba la ekari mia wakati hela ya kuhudumia hata ekari moja huna. Unataka upewe kampuni ambayo inatumia zaidi milioni mia kujiendesha kwa mwezi. Wakati hata bank haiwezi kukopesha hata milioni moja. Mali akipewa mtu asiye na uwezo inaishia kuuzwa au Kupotezwa. Wazungu walijua hilo ndio maana Uingereza kuna property tax ya asilimia 10. Kama unarithi mali ya 1 billion inalipa milioni mia serikalini.

Mkuu wazazi wako wakifa na mkabaki watoto watatu labda wa kiume na akaacha mali basi bila kujali mmoja ni ana Phd ya uchumi na mwingine ni mkulima na mwingine mvuta bangi pale Karume, wote mna haki sawa
Kama mtaamua kugawana mtagawana sawa, na mkiamua kuziendeleza basi hata asiye na mali atakaa nje ya operation lakini atapata mgao wake labda kila mwezi nk

Usichanganye kusimamia na kuwa na haki. Akiamua kwenda mahakamani mali igawanywe basi itauzwa mgawane sawa sawa au mtagawa thamani ya kampuni mara tatu na mtampa haki yake nyie muendelee nayo.

Haki ya mtu haipotei kwa umaaikini wake
 
Mkuu wazazi wako wakifa na mkabaki watoto watatu labda wa kiume na akaacha mali basi bila kujali mmoja ni ana Phd ya uchumi na mwingine ni mkulima na mwingine mvuta bangi pale karume, wote mna haki sawa
Kama mtaamua kugawana mtagawana sawa, na mkiamua kuziendeleza basi hata asiye na mali atakaa nje ya operation lakini atapata mgao wake kabda kila mwezi nk

Usichanganye kusimamia na kuwa na haki
Akiamua kwenda mahakamani mali igawanywe basi itauzwa mgawane sawa sawa au mtagawa thamani ya kampuni mara tatu na mtampa haki yake nyie muendelee nayo

Haki ya mtu haipotei kwa umaaikini wake
Mimi sina shida na mali ya wazee wangu lakini najua kuwa mali za wazee inabidi wapewe wenye uwezo wa kuziendeleza(siyo uwezo wa kielimu bali fedha). Kuna watu hawatakiwi kupewa ijapokuwa wana haki ninajitafutia maisha lakini hata nikifa mali zangu nitawarithisha watoto wangu kadri ya uwezo wao.

Siwezi kumpa mtoto ambaye hajawahi hata kujenga choo ghorofa, mtoto hajui hata tabu ya kugombana na mafundi na gharama za ujenzi. Utakuja kuamka huko kuzimu ndani ya miezi michache vitu vinauzwa vyote. Kama mzazi hajaacha wosia nashauri busara itumike waachiwe wenye uwezo wa kifedha waziendeleze ukipata gawio lako wekeza. Usijifanye kimbele mbele ili uonekane utangukia pua vibaya sana.
 
Bahati mbaya wazazi hawapo sasa basi busara ya mahakama itaamua mali iuzwe halafu igawiwe sawa kwa kila mjukuu

Mkuu hayo mashamba kijijini ndio mtaji wenyewe
Kwani tofauti ya kuwaganisha sawa na kuuza na kugawa pesa tofauti ni nini?
 
Back
Top Bottom