Naomba ushauri wa kisheria kuhusu suala la mgawanyo wa mirathi

jaap

JF-Expert Member
Dec 25, 2018
4,209
5,459
Mzee wetu kasha fariki kaacha wake wawili na watoto 8 kila mke ana watoto wanne. Mzee kaacha nyumba moja na kiwanja kimoja na shamba. Nyumba moja anaishi mke mdogo na kiwanja kimoja, mke mkubwa watoto wake wamejenga nyumba, wanaishi na mama yao, na kwenye shamba wao wanafanya shughuli zao za kiuchumi.

Tatizo linakuja kuhusu kugawana mali za marehemu kwa wake zake wawili. Mke mkubwa anajipa mamlaka ya kugawa mali na kusema nyumba iuzwe na shamba kila mtoto atakayetaka kufanya shughuli za kiuchumi aende kufanya na kiwanja walicho jenga. Watoto wake wawili na familia mbili ziende kuishi pamoja.

Sasa mke mwingine yeye anataka shamba ligawiwe kwa mke mkubwa na mke mdogo, na nyumba kama itauzwa basi na kiwanja walicho jenga watoto wa mke mkubwa nacho kiuzwe. Mke mdogo anashangaa kwanini watoto wanajenga kwenye kiwanja cha baba yao bila ruhusa ya baba yao na wanajua baba yao anawake wawili. Na kuna kiwanja ambacho ni cha familia zote mbili. Naomba ushauri wa kisheria ili kila mke apate haki yake bila mmoja wao kupunjwa.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Mimi haya mambo nasoma komenti tu, nijifunze.

Nasubiria wale wa KATAA NDOA.
 
Shida wakitoa ushauri huku watoto watalala njaa. Kazi yao ndio hiyo unakuta mtu ana watoto wawili au watatu na ndio wanaitegemea. Baba akitoa ushauri wakitaalamu huku jf nani atalisha familia yake sasa. Wa-Tanzania hebu tuamke jamani issue kama hii ulioielezea ni serious nenda kwenye ofisi ya wakili aliyekaribu yako, mlipe consultation fee akushauri the best ways za kudeal na issue yako. Ukizoea free ride huku upewe tu ushauri kuna watu watalala njaa mahali fulani, cz huyo mwenye utaalamu mpaka aingie huku tayari ametumia gharama zake za bundle sasa uje umnyonye na akushauri tena daahh!
 
Kumuona Daktari bingwa mtu yupo radhi kulipa kuanzia 25,000 mpaka 35,000 hata 100,000 lakini wakili mbobevu mnataka free ride mpewe consultation ya bure tu, hii haifai kabisa.
 
Muiambie Mahakama ikawasaidie kugawana
Mfano watoto wa mke mkubwa amejenga nyumba kwenye kiwanja cha familia na wanazidi kuendeleza ujenzi, Mzee alikuwa ana waacha na anasema wanamjengea yeye na wanao jenga wanajua wanajenga nyumba zao.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Aaaaaah, teueni msimamizi wa mirathi, yeye ndiye afanye mgawanyo kwa mjibu wa Sheria.
Mfano kwenye kiwanja cha mzee mtoto wa mke mkubwa kashajenga nyumba za kudumu na anaendelea kuwajengea ndugu zake wengine sasa hapo kwenye kugawana si italeta shida kwasababu kujenga kwenye kiwanja ambacho hajapewa na mzee alikuwa anajua anajengewa yeye.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Mfano kwenye kiwanja cha mzee mtoto wa mke mkubwa kashajenga nyumba za kudumu na anaendelea kuwajengea ndugu zake wengine sasa hapo kwenye kugawana si italeta shida kwasababu kujenga kwenye kiwanja ambacho hajapewa na mzee alikuwa anajua anajengewa yeye.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Kama hicho kilikuwa ni kiwanja kweli Cha mzee na yeye akaamua kijenga bila kipewa na Mzee au na msimamizi wa mirathi. Hiyo siyo sahihi.
 
Kama hicho kilikuwa ni kiwanja kweli Cha mzee na yeye akaamua kijenga bila kipewa na Mzee au na msimamizi wa mirathi. Hiyo siyo sahihi.
Mawazo yao ni mafupi walijua sisi watoto wa mke mdogo hatuta kwenda maisha yote uko kijijini na maisha yote ya mzee wetu tumeishi naye mkoa tofauti na kijijini kwenu, kwayo wao waliianimi eneo la baba ambalo alipewa na Baba yake wataendelea kuwa mali yao, kwasababu sisi hatuja ishi uko miaka mingi, wao kisingizio chao tukigawana mashamba ya uko kijijini tutauza na kwenda kuishi mjini.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Kama hicho kilikuwa ni kiwanja kweli Cha mzee na yeye akaamua kijenga bila kipewa na Mzee au na msimamizi wa mirathi. Hiyo siyo sahihi.
Alikuwa ana jenga tokea mzee yupo hai na mzee alikuwa ana muangalia na tukiwa nae anasema mtoto wake ana mjengea nyumba.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom