Msaada: Kwa waliowahi kufunga ndoa ya Serikali

Msaada: Kwa waliowahi kufunga ndoa ya Serikali

KB THE DON

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2013
Posts
250
Reaction score
117
Habari za jioni wakuu, awali natoa pole kwa pilika za kutwa kwa ujumla wake.

Kama mada inavyojieleza hapo juu.

Naomba kufahamishwa kuhusu vigezo na masharti ya kufunga ndoa ya kiserikali.

Zaidi ya yote naomba kujua nani anaifungisha ndoa hizo na ni wapi then unahitaji nini ili uweze kufunga ndoa hiyo.

Natanguliza shukrani
 
Habar za jion wakuu awali natoa pole kwa pilika za kutwa kwa ujumla wake.
Kama mada inavyojieleza hapo juu
Naomba kufahamishwa kuhusu vigezo na masharti ya kufunga ndoa ya kiserikali
Zaidi ya yote naomba kujua nani anaifungisha ndoa hizo na ni wapi then unahitaji nini ili uweze kufunga ndoa hiyo
Natanguliza shukrani
Nami nawahi kiti . Kama itakuwa simple nitafunga pia.
 
Nenda kwa mkuu wa wilaya kila kitu utafahamishwa hapo
 
Ni simple tu unaenda pale na mwenzi wako mnajaza form na mnalipia around elfu hamsini tu...akaunti namba utapewa huko...baada ya hapo mnasubiri siku 21 mtapangiwa siku ya kwenda,then siku mnaenda na wawakilishi ka ni walezi au wazazi yani wewe na mwenzio kila mtu anaenda mwakilishi mnakula kiapo n it is done..mnaua ishu mnapewa cheti kila mtu chake.
 
Ndioo maaana jamaaa kasema kwamba, nenda kwa mkuu wa wilaya utafahamishwa mambo yote, kma inahitajika picha au dole gumba huko ndio kwenye maelezo
 
Mkuu kwanza tafuta barua za kukutambulisha kutoka serikali za mtaa. Barua iwe na picha yako na ya mwenza wako. Majina yenu halisi ni muhimu. Gharama inategemea haraka yako . Kama unataka tangazo lifanywe Mara 3 basi gharama ni 50000 ( hii nadhani inaweza kupanda au kushuka kutokana na wilaya au thamani ya shilingi sins uhakika). Kisha unapeleka halmashauri huko utaambiwa nani ni muhusika. Siku ya ndoa utatakiwa kuwa na mashahidi ( wewe moja na mkeo moja).

Ndoa ya serikalini ni rahisi na husaidia sana hasa kwenye bima kama moja wenu kaajiriwa na mwingine hana ajira. Au kama mkeo Ana ujauzito bima inaokoa sana
 
Ndioo maaana jamaaa kasema kwamba, nenda kwa mkuu wa wilaya utafahamishwa mambo yote, kma inahitajika picha au dole gumba huko ndio kwenye maelezo
Kukuliza uliza ataambiwa hata yasiyo kuwepo kwenda pale utapewa kila kitu
 
Ahsanten sana wakuu wa mawazo yenu in short i'm done nimepata mawazo muhimu sana naomba Mungu awabariki
 
Mkuu kwanza tafuta barua za kukutambulisha kutoka serikali za mtaa. Barua iwe na picha yako na ya mwenza wako. Majina yenu halisi ni muhimu. Gharama inategemea haraka yako . Kama unataka tangazo lifanywe Mara 3 basi gharama ni 50000 ( hii nadhani inaweza kupanda au kushuka kutokana na wilaya au thamani ya shilingi sins uhakika). Kisha unapeleka halmashauri huko utaambiwa nani ni muhusika. Siku ya ndoa utatakiwa kuwa na mashahidi ( wewe moja na mkeo moja).

Ndoa ya serikalini ni rahisi na husaidia sana hasa kwenye bima kama moja wenu kaajiriwa na mwingine hana ajira. Au kama mkeo Ana ujauzito bima inaokoa sana
 
Back
Top Bottom