Hello Mr Suprize!
Katika masuala ya solar ni sharti kuwa na nidhamu hasa katika matumizi. Bila shaka kwa mwaka mzima hukupata shida na sasa ghafula shida imeanza. Inaonekana ungependa kupata umeme usiku lakini haiwezekani. Ingawa hujaeleza system yako ilivyo, maswali yafuatayo yanaweza kukusaidia kupata tena umeme wakati wa usiku. Golden rule kwa solar ni hii: Mchana utatumia nguvu za jua na usiku utatumia AKIBA iliyowekezwa mchana kutwa kwa nguvu za jua katika battery yako! Now the questions:
1. Je panel yako inavuna jua la kutosha kujaza battery yako?
2. Je, afya ya battery yako (servicing) imefanyika kwa ufasaha? -- ni battery ya maji kwahiyo inahitaji service kama cleaning the terminals, checking water level etc
3. Je, battery yako ni A.H ngapi? pengine umetumia wrong battery kwa mwaka mzima na sasa imekufa (haiwezi kutunza/kufanya power banking) ili upate umeme usiku wakati ambapo panel haivuni chochote toka jua.